KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, July 31, 2012

KIMATAIFA:Kundi la mashabiki wa United wagomea mpango wa kuuza hisa wa Glazers family,Ramires arejeshwa kikosini Brazil kwa ajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Sweden,Diarra:nitacheza sehemu yoyote Mourinho atakayo nihitaji na nyingine.

De Bruyne: Nataka kuondoka Chelsea.
De Bruyne kinda wa Chelsea mwenye umri wa miaka 21 amesema kwasasa anafikiria kuondoka Stamford Bridge kwa muda ili kusaka timu ambayo atapata nafasi katika kikosi cha kwanza wakati ambapo uhamisho wa kueleka  Werder Bremen kwa mkopo ukitarajiwa kukamilika wiki hii
Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka Belgium na Germany mchezaji huyo huenda akatambulishwa mbele ya waandishi wa habari kesho jumatano kabla ya kuanza mazoezi ka kikosi chake kipya baadaye wiki hii.
Amenukuliwa De Bruyne akiongea na Bild akisema
"kocha Roberto Di Matteo anaelewa hali ilivyo , nataka kuelekea Werder ni timu nzuri"
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Belgium alijiunga na Chelsea kwa ada ya pauni milioni £7 mwezi January toka Genk lakini aliendelea kuwepo kwa mkopo na klabu yake ya zamani mpaka kumalizika msimu.
Hivi karibuni ameichezea Chelsea katika michezo miwili ya matayarisho ya msimu dhidi ya Seattle Sounders na Paris Saint-Germain.
Mabingwa wa sola Ulaya Chelsea kwasasa wamebadilisha kikosi chao kwa lengo la kukijenga upya wakiwasajili Marko Marin, Eden ,Thorgan Hazard Oscar baada ya kuwaacha Didier Drogba na Salomon Kalou.

Kundi la mashabiki wa United wagomea mpango wa kuuza hisa wa Glazers family
Wamiliki wa Manchester United wamekuwa katika wimbi kubwa la ukosoaji baada ya kuonyesha kutaka kutumia nusu ya mpango wao wa IPO kutumika kupunguza madeni makubwa ya klabu hiyo.
Glazer family wanamatumaini ya kuongeza uwezo wao kifedha mpaka kufikia pauni milioni £200 kwa kuuza zaidi ya asilimia 10% ya soko la hisa la New York lakini haitatumia pesa kupunguza madeni ya United mbayo kwasasa yamefikia pauni milioni £437.
Endapo watakamilisha hilo Glazers wameonekana wazi kutaka kutumia nusu ya kiasi hicho kwa ajili ya madeni ya klabu hiyo ambayo yaliyotokana na malumbano makubwa ya wakati huo wakiichukua klabu kwa pauni milioni £800 mwaka  2005, ambayo sehemu kubwa ya fedha hizo walikopa.
Mashabiki wa United walikuwa katika kampeni yao maarufu kama utamaduni wao wa 'green and gold' katika msimu ulipiota wakibariki rangi zao za zamani kama Newton Heath, kuashiria kutokufurahishwa na umiliki wa Glazers ndani ya Old Trafford.
Amenukuliwa  Duncan Drasdo mtendaji mkuu wa mfuko wa mashabiki wa Manchester United (MUST) akisema "mashabiki wanakasirishwa sana na hili, Glazers wameigharimu United zaidi ya pauni milioni £550 kama deni linahusiana na ada, na sasa wanatuingiza katika janga lingine ambalo wao ndio watanufaika nalo kupunguza nusu ya mpango wa IPO”.
"ni wazi kabisa hili halina faida kwa Manchester United zaidi ya kuipa Glazers njia ya kujipatia fedha kwa mgongo wa matumizi ya klabu."
Ramires arejeshwa kikosini Brazil kwa ajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Sweden
 Ramires Santos do Nascimento kifupi ‘Ramires’ ameitwa tena katika kikosi cha timu ya taifa ya Brazil cha kocha  Mano Menezes ikiwa ni sehemu ya maandalizi yao ya kombe la dunia 2014 dhidi ya Sweden.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 25 alikuwa msaada mkubwa katika timu ya Chelsea ambao ni mabingwa wa kombe la FA na vilabu bingwa ulaya msimu uliopita licha ya kutokuwepo katika kikosi cha Brazil maarufu kama ‘Selecao’ tangu kuwepo katika kikosi hicho kwenye Copa America 2011.
Menezes ameamua kumkaribisha tena kiungo huyo na atakuwa akiungana na wenzake wa timu moja David Luiz na Oscar Dos Santos.
Timu hiyo inaonekana kama kikosi kile kile kinachoshiriki michezo ya Olympic jijini London wakati ambapo Dede na  David Luiz wakionekana kuipa nguvu katika eneo la ulinzi wakati ambapo Marcelo akiwa mapumziko.
Kiungo wa gharama kubwa wa Corinthians Paulinho pia ameitwa nah ii itakuwa ni kama kupata nafasi ya kuitumikia timu hiyo kwa mara ya pili.
Mshambuliaji wa Valencia Jonas huenda akapata nafasi ya kuichezea timu hiyo kwa mara ya kwanza tangu alipotoa huduma katika kikosi hicho mara ya mwisho akitokea benchi katika mchezo dhidi ya Bosnia na Herzegovina mwezi February.
Mchezo dhidi ya Sweden utapigwa August 15.
Diarra:Nitacheza sehemu yoyote Mourinho atakayo nihitaji
Lassana Diarra amekanusha taarifa kuwa hataki kucheza upende wa ulinzi wa kulia katika timu yake ya Real Madrid.
Taarifa ziliarifu kuwa mfaransa huyo alimwambia kocha wake Jose Mourinho kuwa anataka kucheza sehemu ya kiungo tu lakini kiungo huyo amekanusha juu ya hilo na kusema kwa yeye ni mwenye furaha kucheza popote pale kocha wake atakapo taka.
amenukuliwa Diara kupitia mtandao wa klabu akisema.
"nacheza popote Mourinho atakapo mimi nicheze. mimi ni mfanyakazi nisiyechoka ambaye natumia uwezo wangu wote kwa ajili ya timu".
Madrid haiko vizuri kwasasa katika sehemu ya ulinzi ya kulia kufuatia kuondoka kwa Daniel Carvajal ambaye ameelekea Bayer Leverkusen, wakati ambapo Sergio Ramos anatumika sehemu ya ulinzi ya kati.
Kwasasa Alvaro Arbeloa ndiye chaguo pekee la Mourinho sehemu ya ulinzi wa kulia.
Aidha , Diarra anaonekana kuwa tayari kuziba nafasi hiyo endapo Mourinho atataka kumtumia kufuatia maoni yake hayo.

No comments:

Post a Comment