Kiungo wa
zamani wa kimataifa wa Ufaransa na klabu ya Real Madrid Zinedine Zidane amepata
kazi ya kufundisha timu ya vijana ya Real Madrid (cantera) wakati akipata sifa
ya kufundisha hizi zikiwa ni taarifa mpya toka kwamabingwa hao wa ligi ya Hispania
‘Liga’ klabu hiyo imetangaza.
Akiwa na
umri wa miaka 40 kwasasa na akiwa ametangaza rasmi kustaafu soka mwaka 2006, sasa
ameweka wazi dhamira yake ya kuingia katika uongozi akiwa tayari ameshajiunga
na mafunzo ya kufundisha soka katika chuo kimoja alichokuwepo kocha wa zamani
wa Ufaransa Laurent Blanc mwaka jana.
Tangu atundike
daruga , Zidane amekuwa akifanya kazi ya kumshauri Rais wa Madrid Florentino
Perez na kocha Jose Mourinho, na sasa atakuwa na nafasi yake katika academy
ya klabu hiyo.
Taarifa ya
klabu hiyo imesema
"Zinedine
Zidane ameanza mafunzo ya kufundisha wakati huo huo atakuwa akifundisha vijana
katika academy Real Madrid"
"mwaka
huu atakamisha kupata cheti cha team-management mafunzo ambayo
alianza miezi michache iliyopita.
"hiyo
itamsaidia kujenga uwezo na mafunzo ambayo yatamfanya kuwa kukamilisha kiu yake
kama alivyotangaza katika mkutano na waandhishi wa habari wakati akistaafu
kucheza soka mwezi April mwaka 2006"
Zidane
anatarajiwa kumrithi Alberto Giraldez kama kiongozi wa kituo cha vijana na atakuwa
na kazi ya kujenga upya idara hiyo.
No comments:
Post a Comment