Pages - Menu

Monday, March 11, 2013

FRANK RIBERY KUWAKOSA ARSENAL JUMATANO.



FRANK RIBERY
Kocha wa kikosi cha Bayern Munich Jupp Heynckes atalazimika kumkosa winga wake Frank Ribery katika mchezo dhidi ya Arsenal ukiwa ni mchezo wa marudiano wa hatua ya 16 bora wa ligi ya mabingwa Ulaya dhidi ya Arsenal.
Ribery alikuwepo dimbani dakika zote 90 za mchezo wa ligi kuu ya nchini Ujerumani dhidi ya Fotuna Dusseldorf mchezo uliofanyika mwishoni mwa juma ambapo Munich ilishinda kwa jumla ya mabao 3-2 na yeye ndiye aliyefunga bao la kusawazisha na kufanya matokeo kuwa 2-2 kunako dakika ya 73.
Ribery alionekana kulalamika kuwa anajisikia maumivu ya enka ya mguu wake ya kushoto ambapo baada ya vipimo kufanya hatimaye klabu hiyo ikathibitisha kumkosa mchezaji huyo katika mchezo wa jumatano.
kuumia kwa Ribery ni pigo lingine kwa kocha Heynckes, ambaye pia atamkosa Bastian Schweinsteiger na Jerome Boateng kufuatia kusimamishwa.
Bayern itakuwa ikilinda ushindi wake wa kwanza uiliochezwa katika uwanja wa Emirate ambapo waliiibuka na ushindi wa magoli 3-1.

No comments:

Post a Comment