| Picha hii inaonyesha uwanja wa Bora kijitonyama ulivyopata ugeni wa watu wengi mapeam asubuhi ya leo kumshuhudia mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda Emmanuela Okwi (mwenye chupa ya maji) kwa mara ya kwanza akichanganyika na wachezaji wengine wa Yanga mara baada ya mapema wiki hii uongozi wa Yanga kutangaza kumsajili akitokea Sports Club Villa ya Uganda. Okwi aliihama Klabu ya Simba mwezi Januari na kujiunga na Etoile Du Sahel ya Tunisia ambako hakudumu kwa muda mrefu kabla ya kurejea Uganda na kujiunga na Villa. |
No comments:
Post a Comment