ROCKERSPORTS

Pages - Menu

▼

Thursday, May 8, 2014

Siku chache kuelekea world cup, Polisi wa Brazil wagomea mazingira


Polisi nchini Brazil wanafanya mgomo wa saa 24 wakidai mazingira bora ya utendaji kazi, ikiwa ni siku 37 pekee kabla ya nchi hiyo kuandaa dimba la Kombe la Dunia. Polisi imetishia tena kugoma wakati wa tamasha hilo la soka la kimataifa. Polisi wamegoma katika miji kadhaa itakayoandaa Kombe la Dunia pamoja na mji mkuu Rio, ambao utaandaa mechi saba ikiwemo fainali ya dimba hilo mnamo Julai 13. Wamefanya maandamano ya amani, wakati kocha wa timu ya taifa Luiz Felipe Scolari akikizindua kikosi chake kitakachoshiriki kwenye kinyang'anyiro hicho.

Share

No comments:

Post a Comment

‹
›
Home
View web version
Powered by Blogger.