Pages - Menu

Thursday, August 23, 2012

SIMBA :YONDANI NA TWITE WASIJADILIWE NA MADEGA,NCHUNGA NA MGONGOLWA.

Klabu ya simba ya jijini Dar es Salaam imewasilisha barua yake shirikisho la soka nchini TFF la kutaka kuondolewa kwa baadhi ya wajumbe wa kamati ya katiba ,sheria na hadhi ya wachezaji katika kushughulikia suala la usajili wa wachezaji wawili Kelvin Patrick Yondani na Mbuyi Twite kuhusu .
Simba katika barua hiyo imewataja baadhi ya wajumbe hao kuwa ni pamoja na Iman Madega , Alex Mgongolwa na Lyod Nchunga ambao ni wanachama na wamewahi kuwa viongozi wa Yanga kwa nyakati tofauti.
Akiongea na Rockersports afisa habari wa Simba Ezekiel Kamwaga amesema kimsingi huwezi kupeleka kesi ya namna hiyo katika kamati ambayo ina wajumbe wengi ambao wanamapenzi na klabu ambayo ndiyo inayoshitakiwa ukategemea haki kutendeka.
Amesema Madega na Nchunga wameshawahi kuwa kwenye nafasi ya mwenyekiti ya Yanga wakati ambapo Alex Mgongolwa inaaminika kuwa ni mwanachama mkereketwa wa klabu hiyo.
Kamati ya katiba ,sheria na hadhi ya wachezaji inaongozwa na mwenyekiti Alex Mgongolwa, makamu mwenyekiti Husein Mwamba na wajumbe Imani Madega,Venance Mwamoto,Omari Gumbo ,Ismail Aden Rage na Lloyd Nchunga.
Suala la kujiuliza ni je vipi kuhusu Aden Rage na Omari Gumbo ambao nao ni wanachama wa Simba?
Kwasasa Rage ndio Mwenyekiti na Omari Gumbo kabla ya Uongozi wa sasa alikuwa makamu mwenyekiti wa klabu hiyo.
BOFYA HAPA
 

No comments:

Post a Comment