KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, September 27, 2010

GERARD HOULLIER AMTAKA EMILE HESKEY KUJIAMINIGerard Houllier ameonyesha matumaini makubwa kwa mshambuliaji wake aliipa ushindi timu yake dhidi ya Wolves Emile Heskey na kumtaka kuongeza kujiamini mwenyewe.

Emile Heskey ameanza kuonyesha uwezo baada ya kufanikiwa kuweka nyavuni jumla ya mbao matatu katika michezo minne iliyopita.

Heskey akitokea benchi katika mchezo wa michuano ya Carling katikati ya wiki alifanikiwa kubadilisha sura ya mchezo dhidi ya Blackburn.

Na katika mchezo wa ligi dhidi ya Wolves ukiwa nimchezo wake wa kwanza wa premier League alifanikiwa kuweka nyavuni bao la ushindi mchezo uliopigwa jumapili na kuipa timu yake ushindi wa mabao 2-1.

GIGGS SASA KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA VALENCIA LIGI YA MABINGWA Sir Alex Ferguson amethibitisha kuwa mkongwe Ryan Giggs atakuwa nje ya dimba kwa eiki kadhaa kufuatia matatizo ya hamstring yaliyotokana na mchezo wa sare ya bao 2-2 dhidi ya Bolton Wanderers.

Giggs alilazimika kupumzishwa katika kipindi cha pili katika dimba la Reebok Stadium na sasa kutokuwepo katika mchezo wa ligi ya mabingwa ulaya dhidi ya Valencia mchezo ambao unatarajiwa kupigwa jumatano pamoja na mchezo mwingine wa ligi kuu ya uingereza mwishoni mwa juma lijalo dhidi ya Sunderland.

Sambamba na hilo mshambuliaji Wayne Rooney licha ya kutolewa katika dakika ya 61ya mchezo katika mchezo huo dhidi Bolton yeye hana mashaka makubwa na kwamba atakuwepo katika utakaopigwa katika dimba la Mestalla kwani anahitaji kuwekewa barafu kidogo ili kuondoa maumivu aliyoyapata.

OWEN AIOKOA MANCHESTER UNITED DHIDI YA BOLTON

Manchester United imefanikiwa kuepuka balaa la kupoteza mchezo na kujiunga na vigogo vingine vya LIgi kuu ya Uingereza vya Chelsea na Arsenal kufuatia bao la mshambuliaji Michael Owen na kuipa United sare ya mabao 2-2 dhidi ya Bolton.

United ilikuwa katika nafasi nzuri ya kujisogeza pazuri katika msimamo wa ligi baada ya vinara wa ligi hiyo kudondokea pua katika mchezo wa jana lakini hata hivyo kujikuta mara mbili wakilazimika kusawazisha mabao ya Bolton.

Zat Knight aliaanza kuipa uongozi wa mchezo Bolton baada ya dakika sita mchezo kuanza baada ya bao la wonderful flick kutoka katika katika eneo la kona kabla ya Nani kufanikiwa kusawazisha katika dakika ya 23 .

Baada ya Ryan Giggs na Wayne Rooney kuondolewa dimbani kutokana na kile kilichoelezwa ya kuwa ni kutokana na kuwa fiti hatimaye Martin Petrov shuti lake lilimbaba tiza Darren Fletcher na kumpita mlinda mlango Edwin van der Sara.


Hata hivyo mshambuliaji Michael Owen akitokea alifanikiwa kusawazisha bao hilo ambalo kwake lilikuwa ni bao lake la 200 tangu kuwa katika career ya soka.

Mchezo mwingine ulikuwa ni ile inayoitwa Sunday's Midlands derby, Emile Heskey ameendelea kuonyesha makali yake akiwa na meneja wake wa zamani wakiti wakiwa pamoja Liverpool namzungumzia Gerard Houllier kufuatia kufunga bao la dakika ya majeruhi dhidi ya Wolves katika mchezo Aston Villa imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika dimba la Molineux.

Stewart Downing aliipa uongozi Villa katika kipindi cha kwanza baada ya kupokea mpira wa cross toka kwa Marc Albrighton kabla ya Matt Jarvis kukutana na cross ndani ya box na kuusu,kuusukumiza mpira wavuni kunako dakika ya 61 ya mchezo 61 minutes.

Katika mchezo mwingine bao la James Perch limepelekea msiba wa pili kwa Newcastle toka kwa Stoke wakitokea nyuma kimatokeo na kufanikiwa kupata ushindi wa mabao 2-1 mchezo uliopigwa katika dimba la St James' Park.

No comments:

Post a Comment