KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, November 4, 2014

Hatma ya Morocco kuandaa AFCON kujulikiana Nov 11

Shirikisho la soka barani Afrika limesema linatambua juu ya mlipuko wa ugonjwa Ebola barani Afrika licha ya kugomea ombi la kuahirishwa kwa fainali za mataifa ya Afrika 2015.

Waandalizi wa mwezi Januari nchi ya Morocco italazimika kusubiri mpaka Jumamosi kuamua kama bado wanataka kuendelea kuandaa fainali hizo ama laa.

Hapo kabla walionyesha wasiwasi ya kuendelea na maandalizi hayo kufuatia kuripuka kwa ugonjwa huo kwa kasi kubwa katika ukanda wa Afrika Magharibi.

Katibu mkuu wa Caf Hicham El Amrani amesema
"tunafahamu juu ya hali ya mambo ilivyo, na si hali nzuri kwa kila mmoja wetu.
"tunajua juu ya tahadhari inayopaswa kuchukuliwa na mataifa lakini ni muhimu kuongeza hofu.

Yafuatayo ni madhara tayari ya Ebola katika soka la AfrikA

Sierra Leone imesimamisha shughuli zote za soka

Caf imezifungia Guinea, Liberia na Sierra Leone kuandaa michezo ya kimataifa
Seychelles imeondoa mchezo wake wa kufuzu AFCON dhidi ya Sierra Leone

FIFA yagomea mchezo wa kimataifa wa Uganda na Sudan wakisema ni kinyume na taratibu

Shirikisho la soka duniani (FIFA) imetaka mchezo uliopangwa baina ya Uganda na Sudan kuondolewa katika mpango wa kuchezwa. Katende Malibu, afisa habari wa Uganda Cranes amesema.
"Hatutacheza mchezo wa kirafiki na Sudan kwa amri ya FIFA, hivyo mchezo wetu dhidi ya Ethiopian uko kama ulivyopangwa"
Shirikisho la soka la Uganda(FUFA) lilipanga mchezo dhidi ya Sudan uchezwe Jumanne Novemba 11 2014 ikiwa ni siku mbili baada ya mchezo wao dhidi ya Ethiopia tarehe 9 Novemba 2014
Mchezo wa Ethiopia uliandaliwa na Serikali ya nchi hiyo kupitia wizara mbili za Elimu na Wizara ya michezo na Afya.

Taarifa kutoka Zurich zimesema kuwa michezo miwili ya kujipima nguvu ilikuwa imepangwa kuchezwa kinyume na sheria za FIFA na kwamba hilo halitaruhusiwa ndani ya siku mbili.
Kuelekea mchezo dhidi ya Ethiopia kocha mkuu wa timu ya taifa ya Uganda, Milutin ‘Micho’ Sredojevic tayari ameshakamilisha orodha ya wachezaji watakaocheza mchezo huo na wengi wakitokea katika ligi ya nchi hiyo "Uganda Premier League".
Wachezaji watano wanaochezea katika ligi za Kenya na Ethiopia pia wamejumuishwa kikosini ambapo Rais wa nchi hiyo Yoweri Kaguta Museveni atakuwa mgeni wa heshima na hakutakuwa na kiingilio.

Yaliyomkuta Yaya Toure baada ya Derby ya Manchester ni kubaguliwa mtandaoni

Taasisi inayopambana na ubaguzi wa rangi wa 'Kick It Out' imelitahadharisha jeshi la polisi  juu ya ujumbe wa kibaguzi wa rangi kupitia akaunti ya twitter ya kiungo wa Manchester City Yaya Toure baada ya mchezo wa Jumapili dhidi ya wapinzani wao wa jiji la Manchester Manchester United.

Kiungo huyo alilazimika kuufunga kwa muda ukurasa wake huo kabla ya kurudishia uhai Jumatatu ikiwa ni siku moja baada ya mchezo wa ushindi wa 1-0 dhidi ya Manchester United.

Kiungo huyo wa kimataifa wa Ivory Coast aliandika katika ukurasa wake huo

 "Great to be back on Twitter after a good win yesterday. Now my focus is on the next game...Happy Monday everyone!!"

Katika taarifa yake Jumanne ya leo, Kick It Out imesema kuwa  Toure alipokea ujumbe wa kumbagua muda mfupi baada ya kutupia ujumbe ambapo ulionekana kuwakwaza baadhi ya wanaomfuata.

Msemaji wa Kick It Out amesema "tumepokea malalamiko kutoka katika jumbe mbili za tweeter zikimdhihaki kwa rangi Yaya Toure usiku wa jana.

"tumewaarifu polisi kupitia 'True Vision', kwa njia ya mtandao na tayari wamewatahadharisha Twitter.

Kocha wa Ajax Frank de Boer: tunawaheshimu na sio kuwaogopa Barcelona

Kocha wa Ajax Frank de Boer amesema kikosi chake kinapaswa kuwaheshimu na sio kuiogopa Barcelona"respect, but not fear" wakati wakijiandaa kukutana na wapinzani wao hao katika mchezo wa ligi ya mabingwa Ulaya katika dimba la Amsterdam ArenA hapo kesho Jumatano.
Wadachi hao walichapwa bao 3-1 katika mchezo wa mzunguko wa kwanza mwezi uliopita na De Boer anasema hawataweza kurudia tena mwanzo huo mbaya.
Akiongea katika mkutano waanahabari amesema 
"tunachopasw kufanya ni kucheza na kuwa na mpira wakati wote, tunapaswa kuwa makini zaidi tangu mwanzo wa mchezo kitu ambacho ni muhimu katika mchezo huo.
Huu utakuwa ni mchezo wa pili kwa Luis Suarez kuichezea Barcelona katika ligi ya mabingwa Ulaya atakapo kuwa dimbani Amsterdam ArenA Jumatano ya kesho kuvaana na Ajax katika mchezo wa kundi F.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 aliwahi kuichezea Ajax frontman kwa miaka mitatu na nusu kwa mafanikio kiasi kuwa mchezaji bora mara mbili wa Ajax kabla ya kuelekea Liverpool mwaka 2011

Aleksandar Kolarov nje mwezi mzima, Eliaquim Mangala kuikabili CSKA Moscow

Meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini amethibitisha kuwa Aleksandar Kolarov atakosekana katika kipindi cha takribani mwezi mzima kufuatia matatizo ya msuli.

Mlinzi huyo alipatwa na majeraha katika maandalizi ya kupasha misuli joto kabla ya mchezo dhidi ya Manchester Jumapili iliyopita na nafasi yake kuchukuliwa na Gael Clichy kabla ya kukabiliana na kikosi cha Louis van Gaal.

Nyota huyo wa kimataifa wa Serbia sasa atakuwa katika kipindi mapumziko ingawa Pellegrini kuwa mlinzi Eliaquim Mangala atakuwa safi katika mchezo dhidi ya CSKA Moscow.

"Kolarov alipatwa na matatizo ya msuli atakuwa nje kwa mwezi mzima" amewambia waandishi wa habari "Mangala atakuwepo katika orodha ya wachezaji katika mchezo wa kesho."

Diafro Sakho wa West Ham kuhusika katika mchezo dhidi ya Aston Villa

Mfungaji anayeongoza katika klabu ya West Ham Diafro Sakho imeelezwa kuwa yuko fiti kuelekea katika mchezo wa Jumamosi wa Premier League dhidi ya Aston Villa baada ya kuponya majeraha yake ya bega.

Sakho alikutana na tatizo hilo katika dakika za mwisho kabisa za mchezo wa ushindi wa bao 2-1 dhidi ya Manchester City mwezi uliopita ambapo aliukosa pia mchezo wa jumamoso iliyopita dhidi ya Stoke City.

Lakini hata hivyo mshambuliaji huyo ambaye alisajiliwa hivi karibuni ambaye amekuwa akifunga karibu kila mchezo wa ligi kuu kwasasa yuko fiti kukichezea kikosi cha meneja  Sam Allardyce's watakapo kuwa safarini Villa Park.

Allardyce pia anategemea kuwa na Winston Reid baada ya mlinzi huyo kutolewa katika mchezo dhidi ya Stoke, licha ya kumkosa Guy Demel mwenye matatizo ya paja.

Sunday, November 2, 2014

Huenda Steven Gerrard akaelekea nchini Marekani kiangazi

Steven Gerrard huenda akahamia nchini Marekani majira ya kiangazi
Gerrard ametanabaisha kuwa endapo Liverpool itashindwa kumpatia mkataba mpya baada ya msimu huu angependelea kuhamia sehemu nyingine huku mwanga ukiangazia kuwa huenda akaelekea katika soka la Marekani ambalo linazidi kudumaa
Gerrard (right) has been at Liverpool since making his debut in 1998
Gerrard (kulia)  amekuwepo Liverpool tangu mwaka1998

New York Cosmos ambayo inafanya vizuri katika soka la Amerika ya Kaskazini huenda ukawa ndio muelekea mpya wa Gerrard.
Gerrard shakes hands with Rick Parry in 2004 after signing a new Liverpool deal. A year later, he led the club to a famous Champions League victory in Istanbul
Gerrard akipeana mikono na Rick Parry mwaka 2004 baada ya kusaini mkataba mpya na Liverpool mwaka uliofuata akaisaidia klabu yake kushinda taji la klabu bingwa mjini Istanbul

Rais Jakaya Kikwete amezindua ujenzi wa kituo cha vijana cha michezo cha kimataifa mjini Dar es Salaam.

Afisa Mtendaji wa Sunderland Margaret Byne (kulia) Mkurugenzi wa biashara Sunderland (katikati) na Stewart Hall aliyekuwa kocha wa Azam Fc ya Tanzania
Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete jana amezindua ujenzi wa kituo cha vijana cha michezo cha kimataifa mjini Dar es Salaam.
Mwandishi wa BBC Baruan Muhuza aliyehudhuria shughuli hiyo amesema kuwa mradi huo unagharamiwa kwa pamoja na kampuni ya nishati ya umeme Symbion Power ya Marekani na klabu ya soka ya Sunderland inayoshiriki ligi kuu ya England.
Katika sherehe za uzinduzi huo kwenye eneo la Kidongo Chekundu Mnazi Mmoja Rais huyo aliungana kwa pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa Sunderland Margaret Bryne na Afisa Mtendaji Mkuu wa Symbion Power Paul Hinks.
Akizungumza katika shughuli hiyo Bryne alisema “Tunafurahia kuwa hapa Tanzania leo na kuona maendeleo yanayofanywa na mradi huu.
Uwanja huu wa michezo ni sehemu ya msingi wa ushirikiano wa kipekee kati yetu na kandanda ya Tanzania, ni furaha kuona kituo hiki kikijengwa.”
Kituo hicho kitakapokamilika mwezi machi 2015 kitakuwa na uwanja mkubwa wa soka wenye nyasi za bandia za kiwango cha kimataifa cha 3G, uwanja wa wachezaji watano kila upande, viwanja viwili vya mchanga na uwanja wa mpira wa kikapu na wavu.
Katika mradi huu kampuni ya Symbion Power inagharamia ujenzi wa kila kitu katika kituo hicho huku Klabu ya Sunderland ikitoa wataalamu wa ufundi na mafunzo ya soka kwa watoto na vijana.
Akihutubia umma wa watu waliojitokeza katika shughuli ya uzinduzi huo, Rais Kikwete alieleza matumaini yake ya matunda yatakayotokana na mradi huo, huku akielezea jinsi alivyopata wazo la kuanzishwa kwa kituo hicho ambacho kimepewa jina lake.

Entente Satif bingwa wa vilabu Afrika

Kilabu ya Entente Satif kutoka Algeria imeshinda ubingwa wa kilabu bora barani Afrika kwa mara ya kwanza katika miaka 26 baada ya kuishinda kilabu ya AS Vita Club kutoka jamhuri ya kidemokrasia ya Congo kutokana na mabao ya ugenini kufuatia sare ya 3-3 siku ya jumamosi.
Raundi ya pili ya fainali katika uwanja wa Mustapha Tchaker mjini Blida ilikamilika kwa sare ya 1-1,siku sita baada ya sare ya 2-2 katika mechi ya kwanza iliochezwa mjini Kinshasa.
Setif ilianza kuona lango na wapinzani wao dakika nne katika kipindi cha pili kupitia Sofaine Younes ambaye alifunga bao kupitia pasi ya El Hadi Belameiri.
Lakini wageni hao walisawazisha dakika tano baadaye kupitia Lema mabidi aliyepiga mkwaju kutoka nje ya eneo la kupigia penalti ili kuimarisha matumaini ya timu yake.
Mabidi pia alikuwa ameifungia kilabu hiyo mabao yake mawili katika raundi ya kwanza ya mchuano huo wikendi iliopita.
Bao hilo lilisababisha mechi hiyo kuwa ngumu ambapo Vita ilionyesha mchezo mzuri ikilinganishwa na wapinzani wao Setif waliojaribu kutumia mbinu chafu za kupoteza mda huku mashabiki wa kilabu hiyo wakitaka mchezo huo kukamilishwa kuanzia dakika ya 75.

Sergio Aguero apeleka kilio kwa United

Ilikuwa ikionekana ni ngumu leo kumfunga David de Gea. Kwa upande wake Sergio Aguero haikuwa hivyo kwani alidhihirisha kuwa yeye ni noma alipoifungia bao pekee kwa timu yake na kuipa ushindi City dhidi ya United.

Tayari dakika 63 zilikwisha kupita wakati Aguero akifunga goli hilo na kudhihirisha kuwa yeye ndiye shujaa wa 'derby' ya Manchester hii leo.

Wasiwasi ulitanda tangu mapema kufuatia United kupungua na kusali kumi kunako dakika ya 39 wakati Chris Smalling alipoondoshwa uwanjani na mwamuzi kwa makosa mawili huku pia Marcos Rojo akiumia bega.
Sergio Aguero converts Gael Clichy's low cross from the left to put Manchester City 1-0 ahead in the Manchester derby
Sergio Aguero akiunganisha krosi ya Gael Clichy kutoka kushoto na kuwapa uongozi Manchester City wa bao 1-0 dhidi ya majirani zao Manchester United

Juhudi za Aguero zikionekana katika picha akipiga mpira unaomzidi David de Gea kunako dakika ya 63 uwanja wa Etihad

Aguero (third from left) is mobbed by his team-mates after giving Manchester City the lead against their local rivals United
United players (from left to right) Paddy McNair, Wayne Rooney and Luke Shaw appear dejected following City's goal