KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, November 25, 2012

RONALDO DE LIMA: PEP GUARDIOLA ANA VIGEZO VYOTE VYA KUINGOZA BRAZIL . CARLO ANCELOTTI BADO ANAMTAMANI ALEXANDRE PATO. BRANDAN ROGERS ANASEMA LIVERPOOL MATAJI BADO KIDOGO NA BAADA YA KUSHINDWA KUWAFUNGA ASTON VILL WENGER ANASEMA WALICHOSHWA NA MONTPELLIER.


 Ronaldo De Lima ambaye kwasasa ana heshima kubwa nchini kwake Brazil amesema kocha wa zamani wa  Barcelona Pep Guardiola ndiye chaguo lake la kwanza kurithi nafasi ya Mano Menezes aliyetimuliwa kazi hivi karibuni.

Kocha Menezes alitimuliwa kazi ijumaa baada ya kile kilichoelezwa kuwa hakuwa na matokeo mazuri katika michezo mbalimbali ya timu ya taifa hilo wakati huu ambapo Brazil ambayo inaandaa michuano ya kombe la dunia 2016.

Japo kwamba Ronaldo hakubaliani na maamuzi ya kufukuzwa kazi Menezes, amesema itakuwa ni vema kumsaka kocha ambaye ana vigezo sahihi ambayo ni kama alivyo navyo kocha wa zamani wa Barcelona Pep Guardiola.

Akiongea na Globo, amesema.
"kila mtu anapapara, lakini kila siku unatakiwa kuangalia kwa picha kubwa. Siwezi kufanya maamuzi hayo, lakini  Brazil inahitaji kurejea tulikokuwa tena,"
"tuna makocha wakubwa Brazil, na tunahitaji mtu ambaye anaonyesha utulivu ndani ya timu,
"Guardiola ni kocha bora duniani kwasasa. Alifanya kazi nzuri Barcelona na anaweza kuwa chaguo bora kwa Brazil. Hebu tuone kama mashabiki watampenda ama laa"


Rodgers: Liverpool itatwaa mataji muda si mrefu.
Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers amesema miaka michache ijayo klabu yake italeta changamoto mpya ya kutwaa mataji ya ligi ya England.

Kwasasa Liverpool iko katika 12 katika msimamo wa ligi kuu ambapo kuelekea kweny mchezo dhidi ya Swansea City kocha huyo anayetokea Ireland ya kaskazini anasena anamatumaini kuwa mazuri.

Liverpool haiajawahi kumaliza ligi kuu ya England ikiwa katika nafasi ya kucheza michuano ya klabu bingwa Ulaya tangu Rafa Benitez alipokuwa akiiongoza na kwasasa iko nyuma ya kikosi cha kocha wao huyo wa zamani kwa alama tisa ambapo Chelsea iko katika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi ya England.

Rodgers anasisitiza kuwa pamoaj na kwamba kujenga kikosi ni muhimu lakini pia ina weza ikato changamoto muda mfupi ujao na kuwapa raha mashabiki wake.

"sioni sababu ya kwanini tusitoe changamoto katika kipindi cha miaka michache ijayo. Wakati mwingine unaweza kudondoka kwa hatua chache kabla ujaanza kujijenga upya"

Kwasasa Luis Suarez wa Liverpool anaongoza orodha ya wafungaji wa Premier League akiwa tayari amefunga jumla ya mabao 10 baada ya michezo 12 ya msimu huu ambapo Rodgers amesema ataendelea kumtumia mruguayi ambaye yuko kwenye fomu.

Ancelotti: Pato anastahili kuchezea Paris Saint-Germain.
 Carlo Ancelotti amezidi kutia utambi tetesi za Paris Saint-Germain kuwa huenda waanzisha tena mpango wao wa kumtaka mshambuliaji wa AC Milan Alexandre Pato akidai kuwa mshambuliaji huyo ana vigezo vyote vinavyotakiwa.

Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa iliaminika kuwa alikiwa karibu kukamilisha uhamisho wake wa euro milioni 35 kuelekea Parc des Princes mwezi Januari lakini baadaye mpango huo ukaonekana kwenda kombo.

Hata hivyo kuna taarifa kuwa pande mbili hizo zinaelekea kukubaliana kutokana na kile kinachoelezwa kuwa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 23 hana raha na maisha ya soka ndani ya klabu ya AC Milan.

Wakati hayo yakiwa hivyo, Ancelotti ambaye alimfundisha mshambuliaji huyo kule Rossoneri kati hya miaka ya 2007 na 2009 ameeleza kuwa nyota huyo kutoka Marekani ya Kusini anafanana na hadhi ya PSG na shaka yoyote uwezo wake.

"hajawahi kunipigia simu. Mimi si rafiki yake alikuwa mchezaji wangu nilipokuwa Milan, lakini kiukweli ana vigezo vya kuichezea PSG"
"ni mfungaji mzuri lakini hatuwesi kusaini wafungaji wote wazuri duniani. Tuna wachezaji katika nafasi hiyo kama vile Jeremy Menez, Ezequiel Lavezzi na Zlatan Ibrahimovic."

Wenger ajitetea baada yua kushindwa kuwafunga Aston Villa.
 Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amesema kuwa kilicho wafanya washindwe kuifunga Aston Villa na kwenda sare ya bila mabao ni mchoko.

Washika mtutu walishinda kutengeneza nafasi dhidi ya Villa na kulazimika kugawana alama moja kila upande matokeo ambayo yamewaweka mbele kwa tofauti ya alama moja dhidi ya Chelsea katika msimamo wa ligi.

Mchezo wa katikati ya wiki dhidi ya Montpellier ilipelekea meneja huyo kuwapumzisha vijana wake kutoka katika jiji la London Jack Wilshere, Bacary Sagna na Thomas Vermaelen katika mchezo huo.

Wenger anaamini mchezo wa katikati ya wiki ulikuwa ni sehemu ya sababu za vijana wake kucheza chini ya kiwango jambo ambalo hakulipinga kuwa walikuwa chini ya kiwango.

Arsenal imefunga goli moja tu katika michezo mitatu iliyocheza ugenini.

Matokeo hayo yanamfanya wenger kusema
"ni kweli. Ila sijui sababu ni nini. Tuna timu nzuri ya ulinzi na tuna wachezaji wazuri wazuiaji sehemu ya kiungo na tuna washambuliaji watatu, lakini hii inaweza kutokea iliwakutokea huko nyuma ni tofauti unapocheza nyumbani na ugenini."

No comments:

Post a Comment