KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, November 24, 2012

UGANDA CRANES WAANZA VEMA KUTETE TAJI LA MICHUANO YA CHALLENGE. NAO ETHIOPIA WAANZA VEMA LICHA YA KIWANGO KIDOGO.

Geoffrey Kizito anaecheza soka Vietnam akipongezwa baada ya kufunga goli pekee la ushindi dakika ya 74 ya mchezo wa Cranes dhidi ya Harambee Stars.


Timu za taifa ya Ethiopia na wenyeji Uganda zimefanikiwa kuanza vizuri michezo yao ya mwanzo ya michuano ya kombe la Challenge iliyoanza hii leo mjini  Kampala nchini Uganda.

Hii ni michezo ya kundi la A ambapo mchezo wa mapema timu ya taifa ya Ethiopia ambao mwezi Januari watakuwa wakielekea nchini Afrika Kusini waliwachapa Sudani Kusini kwa bao 1-0.

Mshambuliaji Yonathan Kebede alifunga bao hilo pekee kunako dakika ya 60 kufuatia mpira wa krosi kutoka mashariki ya uwanja wa Nambole.

Nahodha Leon Khamis alipata nafasi mbili nzuri pengine kama angezitumia vizuri basi pengine wangechomoza na ushindi mnono zaidi.

Hata hivyo kocha msaidizi wa Ethiopia Seyoum Kebede, amesema pamoja na ushindi huo kikosi chake kitalazimika kuongeza jitihada zaidi.

“ni vizuri tumeshinda mchezo wetu wa kwanza wa michuano hii lakini tunalazimika kuongeza jitihada zaidi”.

Katika mchezo wa pili ambao Rais wa shirikisho la soka barani Afrika Issa Hayatou alikuwa akiushuhudia wenyeji Uganda wamefanikiwa kuanza vema kampeni yao ya kutete taji hilo wakianza na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wapinzani wao wakubwa Harambee Stars ya Kenya.

Mchezaji nyota anayechezea soka nchini Vietnam Geoffrey Kizito alifunga goli hilo pekee zikiwa zimesalia dakika 16 mchezo kumalizika.

Goli hilo lilikuja mfupi baada ya mlinda mlango namba moja wa Uganda ‘The Cranes’ Abel Dhaira akipelekwa katika gari la wagonjwa baada ya kugongana na mlinzi wa Harambee stars katika harakati za kuokoa mpira wa shambulizi.

Michezo mingine ya kundi A itaendelee tena jumanne ambapo Ethiopia wataanza mchezo wa mapema dhidi ya Uganda na baadaye Kenya kukutana na Sudani Kusinin.

Michuano hiyo itaendelea tena hapo kesho kwa michezo ya kundi B ambapo mchezo wa mapema Burundi wataanza na Somalia na baadaye Kilimanjaro stars watakuwa wakishuka dimbani dhidi ya Sudan.

No comments:

Post a Comment