KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, July 20, 2014

Mshahara anao taka Samuel Eto'o ni kikwazo cha kujiunga kwake na QPR

Samuel Eto'o ameonyesha bado anaweza kufunga mabao katika Premier League na kwasasa yuko huru
QPR imeweka dhamira ya kumsajili mshambuliaji wa zamani wa Chelsea Samuel Eto'o lakini inaonekana kushindwa kufikia kiwango cha mshahara ambacho mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Cameroon.
Eto'o mwenye umri wa miaka 34 kwasasa yuko huru baada ya kumaliza mkataba wake wa mwaka mmoja Stamford Bridge kiangazi hii.
Harry Redknapp ameweka wazi kuwa anahitaji huduma ya mpiga mabao huyo wa zamani wa Barcelona kwa lengo la kutengeneza safu nzuri ya ushambuliaji lakini mshahara anao utaka Eto'o unakuwa kipingamizi.
Chini ya Jose Mourinho msimu uliopita mshambuliaji huyo ambaye anadhaniwa kuwa ni mkongwe aliifungia Chelsea mabao 12 katika michezo 35 ikiwemo 'hat-trick' dhidi ya Manchester United.
Bit of a blow: But Harry Redknapp believes he would be better spending Eto'o's wage money elsewhere
Harry Redknapp anaamini anaweza kutumia mshahara anaotaka Eto'o kwingineko.

No comments:

Post a Comment