KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, July 20, 2014

STARS YAVURUNDA UWANJA WA TAIFA MBELE YA MSUMBIJI INAHITAJI USHINDI AU SARE ILIYOSHIBA UGENINI KUFUZU HATUA YA MAKUNDI

Kikosi cha Stars
Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars imejiweka katika mazingira magumu ya kufuzu kwa hatua ya makundi ya fainali za mataifa ya Afrika(AFCON), fainali ambazo zitafanyika mwakani nchini Morroco.
Ikiwa katika uwanja wake wa nyumbani wa Taifa, mbele ya maelfu ya mashabiki wake aliokuwa nyuma yao, Stars imelazimishwa sare ya bao 2-2, ambapo sasa watalazimika kushinda au kupata sare ya kuanzia mabao 3-3 ugenini katika mchezo wa marudiano utakaopigwa Agosti 1 na 3 mwaka huu nchini Msumbiji.
Stars ilikuwa imesheheni wachezaji wake wote muhimu akiwemo kiungo Mwinyi Kazimoto, Thomas Ulimwengu, Mbwana Samatta na mlinzi kitasa Shomari Kapombe ambapo imeonekana dhahiri kuwa inahitaji mbinu mpya ya kuweza kufanya ulinzi wa kipolisi inapokuwa inashambulia ili kuzuia madhara langoni mwao. Golini alikuwa Deogratius Munish Dida ambaye kutokana na umakini mdogo wa walinzi wake waliokuwa wakiongozwa na nahodha Nadir Haroub Canavaro walijikuta wakifungwa bao la pili kizembe muda mfupi baada ya shambulizi zuri la Thomas Ulimwengu. 
Mabao ya Stars yametiwa kwenye kamba na kiungo Khamis Mcha maarufu kama ‘Vialli’ aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Mrisho Ngassa. Viali alifunga mabao hayo katika dakika za 65 na bao la pili dakika ya 71 kwa njia ya penati.
Mabao ya Msumbiji yamefungwa na Elias Pelembe na Isaack Carvalho aliyeingia kipindi cha pili.
Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars imejiweka katika mazingira magumu ya kufuzu kwa hatua ya makundi ya fainali za mataifa ya Afrika(AFCON), fainali ambazo zitafanyika mwakani nchini Morroco.
Ikiwa katika uwanja wake wa nyumbani wa Taifa, mbele ya maelfu ya mashabiki wake aliokuwa nyuma yao, Stars imelazimishwa sare ya bao 2-2, ambapo sasa watalazimika kushinda au kupata sare ya kuanzia mabao 3-3 ugenini katika mchezo wa marudiano utakaopigwa Agosti 1 na 3 mwaka huu nchini Msumbiji.
Stars ilikuwa imesheheni wachezaji wake wote muhimu akiwemo kiungo Mwinyi Kazimoto, Thomas Ulimwengu, Mbwana Samatta na mlinzi kitasa Shomari Kapombe ambapo imeonekana dhahiri kuwa inahitaji mbinu mpya ya kuweza kufanya ulinzi wa kipolisi inapokuwa inashambulia ili kuzuia madhara langoni mwao. Golini alikuwa Deogratius Munish Dida ambaye kutokana na umakini mdogo wa walinzi wake waliokuwa wakiongozwa na nahodha Nadir Haroub Canavaro walijikuta wakifungwa bao la pili kizembe muda mfupi baada ya shambulizi zuri la Thomas Ulimwengu. 

Mabao ya Stars yametiwa kwenye kamba na kiungo Khamis Mcha maarufu kama ‘Vialli’ aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Mrisho Ngassa. Viali alifunga mabao hayo katika dakika za 65 na bao la pili dakika ya 71 kwa njia ya penati.
Mabao ya Msumbiji yamefungwa na Elias Pelembe na Isaack Carvalho aliyeingia kipindi cha pili.




No comments:

Post a Comment