KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, May 24, 2013

MABADILIKO YA KANUNI ZA LIGI KUU YA SOKA TANZANIA BARA .............SOMA KWA MAKINI MDAU WA SOKA



 UTANGULIZI
Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania limezifanyia marekebisho kadhaa baadhi ya Kanuni za Ligi Kuu ya Vodacom ili kuondokana na migogoro isiyokuwa ya lazima. Mabadiliko haya lengo lake kuu ni kuwa na Ligi iliyo bora zaidi, ambayo itaweza kuleta ushindani  kwa timu shiriki na pia kutoa burudani zaidi kwa watazamaji, pamoja na kuchochea wadhamini zaidi kujitokeza kwa ajili ya kudhamini ligi na timu shiriki.

Ligi iliyo bora, itawezesha kupata wachezaji bora watakaounda timu bora ya Taifa itakayoweza kufanya vizuri katika medani ya kimataifa na pia tutaweza kupata klabu zitakazotuwakilisha vyema katika mashindano ya kimataifa kwa ngazi ya klabu.  Mafanikio haya yataweza kukuza na kuendeleza kiwango cha soka katika nchi yetu na pia kuijengea heshima Tanzania katika ulimwengu wa soka.

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania linafahamu na linaamini kuwa mpira wa miguu ni mchezo wenye nguvu, unaopendwa na watu wengi duniani na unaoweza kuvutia watu wengi kuwekeza iwapo kanuni, taratibu na sheria za mchezo huu zitafuatwa na kuheshimiwa na pia kanuni za ‘fair play’ zitazingatiwa na wachezaji, makocha, waamuzi, viongozi, washabiki, na wengine wote ambao kwa njia moja au nyingine wanahusika na mchezo wa soka.

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania linaagiza kilabu, makocha, na waamuzi kuzisoma kwa makini kanuni hizi na kuhakikisha zinaeleweka na kufuatwa kwa faida ya mchezo wa mpira wa miguu.  Shirikisho linapenda kuwakumbusha watu wote kuwa soka kama ilivyo michezo mingine yote inalindwa na sheria pamoja na kanuni.  Bila sheria michezo itakuwa ni vurugu tupu.  Shirikisho linaziomba kilabu kuhakikisha kuwa kanuni hizi pia zinaeleweka vizuri kwa wachezaji na washabiki wake, kwani itasaidia kuwafanya 

wafahamu kanuni na taratibu za mpira wa miguu vizuri zaidi na kwa kuzifahamu kanuni  zaidi,  zitawafanya wawe wachezaji bora zaidi na wataepuka kuadhibiwa kwa makosa ambayo yanaweza kuepukika.

Kanuni na sheria huwekwa kwa ajili ya kuufanya mchezo uwe na ladha katika kuucheza na pia uwe na ladha katika kuuangalia na hivyo kuufanya uwe na burudani zaidi.  Tukitumia nguvu na ‘spirit’ ya soka inavyotakiwa, tutaweza kujenga jamii na dunia bora yenye afya zaidi, upendo, amani, furaha na usawa.

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania siku zote litahakikisha mchezo wa soka unakuwa na heshima kwa kusimamia kwa uadilifu kanuni na sheria za mchezo huu, kutoa adhabu inapobidi, kuelimisha na kuhakikisha siku zote mshindi anapatikana uwanjani kwa kufuata kanuni na taratibu za mchezo na siyo kwa kutumia njia chafu zisizokubalika.

MICHEZO NI FURAHA NA AJIRA
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA
YALIYOMO

Na                                                                   Kanuni                                                           Ukurasa


SURA YA KWANZA
Kuundwa, Matumizi na Tafsiri

1.         Kuundwa                                                                                                                     7

2.        Matumizi na Tafsiri                                                                                                       7

SURA YA PILI
Daraja, Aina na Namna ya Uendeshaji Ligi

3.        Daraja la Ligi                                                                                                                8

4.        Namna ya Uendeshaji wa Ligi Kuu ya Vodacom                                                          8

5.        Uwanja wa Nyumbani na Ugenini                                                                                 9

6.        Mshindi wa Ligi                                                                                                                        9

7.        Msimu wa Ratiba ya Ligi                                                                                               10

SURA YA TATU
Taratibu za Mchezo

8.        Taratibu za Mchezo                                                                                                      10

9.        Kuahirisha Mchezo                                                                                                       16

10.      Waamuzi                                                                                                                       16

SURA YA NNE
Huduma ya Kwanza na Bima

11.      Huduma ya Kwanza                                                                                                     17

12.      Bima                                                                                                                             17

SURA YA TANO
Ada ya Ushiriki na Usimamizi wa Ligi

13.      Ada ya Ushiriki na Usimamizi wa Ligi                                                                          18

14.      Usimamizi wa Ligi                                                                                                        18

15.      Kamati ya Nidhamu                                                                                                      18


SURA YA SITA

16.      Kamati ya Rufaa                                                                                                           18

17.      Rufani na Utaratibu Wake                                                                                            18

18.      Utaratibu wa Kuwasilisha Malalamiko                                                                         19

19.      Ada na Rufaa                                                                                                                20

SURA YA SABA

20.      Mgawanyo wa Mapato                                                                                                  20

21.      Gharama za Mchezo                                                                                                     21

SURA YA NANE

22.      Kujitoa Katika Ligi                                                                                                       22

23.      Kutofika Kituoni/Uwanjani                                                                                         23

24.      Kuvuruga Mchezo                                                                                                        24

25.      Kupanga Matokeo                                                                                                        25

SURA YA TISA
Udhibiti wa Mienendo na Adhabu kwa Wachezaji, Waamuzi na Viongozi


26.      Uchezaji wa Kiungwana (Fair Play)                                                                              25

27.      Udhibiti wa Wachezaji                                                                                                  29

28.      Udhibiti na Adhabu kwa Waamuzi                                                                               30

29.      Udhibiti wa Kamishna                                                                                                  31

30.      Udhibiti wa Mtathimini                                                                                                32

31.      Udhibiti wa Walimu                                                                                                      33

32.      Udhibiti wa Viongozi                                                                                                    34

33.      Adhabu kwa Klabu                                                                                                       35

34.      Viwango na Utaratibu wa Adhabu kwa Wachezaji                                                       36




SURA YA KUMI
Usajili na Uhamisho wa Wachezaji

35.      Kipindi cha Usajili                                                                                                        37

36.      Hadhi ya Wachezaji                                                                                                      38                                                       
37.      Kupata Upya Hadhi ya Ridhaa                                                                                     38

38       Kuacha Shughuli                                                                                                           38

39.      Usajili                                                                                                                            39

40.      Vipindi vya Usajili                                                                                                        39

41.      Pasi ya Wachezaji                                                                                                         40

42.      Maombi ya Usajili                                                                                                         40

43.      Hati ya Uhamisho ya Kimataifa                                                                                                41

44.      Kuazimwa kwa Mkopo Wachezaji wa Kulipwa                                                                       41

45.      Wachezaji Wasiosajiliwa                                                                                                           42

46.      Masharti Maalum Yanayohusu Mikataba kati ya Wachezaji wa Kulipwa na Klabu      42

47.      Usajili na Uhamisho wa Wachezaji                                                                               44

48.      Uthibitisho wa Usajili                                                                                                   44

49.       Majina ya Wachezaji                                                                                                    44

50.       Idadi ya Wachezaji                                                                                                      44

51.       Klabu/Wachezaji Wanaositisha au kumaliza Mikataba                                                          45

52.       Wachezaji Waliopandishwa                                                                                         45

53.       Wachezaji Huru                                                                                                           45
          
54.       Wachezaji wa Kuhamishwa                                                                                         45

55.       Wachezaji Kutoka Nje ya Nchi                                                                                   46

56.       Ngazi za Uthibitisho wa Usajili                                                                                               46

57.       Kutengua Uthibitisho wa Usajili                                                                                 46

58.       Katazo                                                                                                                         47

59.       Uhamisho wa Mchezaji                                                                                               47

60.       Uhamisho Kwenda Zanzibar                                                                                       48


SURA YA KUMI NA MOJA
Adhabu Zihusuzo Usajili na Uhamisho

61.      Adhabu Zinazohusu Usajili na Uhamisho                                                                     49

62.      Uhamisho Nje ya Nchi                                                                                                  50

SURA YA KUMI NA MBILI
Mengineyo

63.      Mwalimu wa Timu                                                                                                        51

64.      Daktari wa Timu                                                                                                           51

65.      Timu za Pili na Watoto                                                                                                 52

66.    Adhabu zisizokatiwa rufaa                                                                                             52

67.      Udhamini                                                                                                                      52

68.      Lesseni ya kushiriki ligi kuu                                                                                          52

69.      Utumiaji wa madawa ya kuongeza nguvu                                                                     53

70.      Ufafanuzi                                                                                                                      53

71.      Tafsiri                                                                                                                           53

72.      Marekebisho ya Kanuni                                                                                                            53

73.      Kufuta Kanuni                                                                                                              53

74.      Mambo Yasiyomo Kwenye Kanuni Hizi                                                                      54


NYONGEZA
Jedwali la Kwanza


18 (5) Ada za Usajili na Uhamisho wa Wachezaji                                                                   55

19 (B) Mgawanyo wa Ada za Usajili na Uhamisho wa                                                             56
           Wachezaji Kutoka Tanzania Bara Kwenda Tanzania Zanzibar                                                                       


SURA YA KWANZA
KUUNDWA, MATUMIZI NA TAFSIRI


KANUNI YA 1

KUUNDWA

Kanuni hizi zimeundwa chini ya Ibara ya 34 (1.K) ya katiba ya TFF ya mwaka 2006 na zitatumika Tanzania Bara.
KANUNI YA PILI 2
MATUMIZI NA TAFSIRI

Katika Kanuni hizi isipokuwa pale ambapo imeainishwa vinginevyo:-

“FIFA” tafsiri yake ni “Federation Internaltionale de Football Association” ikiwa na maana ya Shirikisho la Kimataifa la Vyama vya Mpira wa Miguu.

“CECAFA” tafsiri yake ni: Council of East and Central Africa Football Associations” ikiwa na maana ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu la Nchi za Afrika Mashariki na Kati.

“TFF” tafsiri yake ni Tanzania Football Federation”, ikiwa na maana ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania.

“Kamati ya Utendaji” maana yake ni Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania.”

“ZFA” tafsiri yake ni: “Zanzibar Football Association”, ikiwa na maana ya Chama cha mpira wa Miguu Zanzibar.

 “FRAT” tafsiri yake ni “Football Referees Association of Tanzania”, ikiwa na maana ya Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu Tanzania.

“TAFCA” tafsiri yake ni “Tanzania Football Coaches Association” ikiwa na maana ya Chama cha Walimu wa Mpira wa Miguu Tanzania.

“TASMA” tafsiri yake ni Tanzania Sports Medicine Association ikiwa na maana ya Chama cha Wataalamu wa Tiba kwa Wanamichezo Tanzania.

 ‘Sputanza’ Soccer Players Union of Tanzania tafsiri yake chama cha wachezaji wa soka Tanzania

“Kilabu” maana yake ni kilabu cha mpira wa miguu.

“Timu” maana yake ni Timu ya Mpira wa Miguu

“Mpira” maana yake ni Mpira wa Miguu.

SURA YA PILI
DARAJA, AINA NA NAMNA YA UENDESHAJI LIGI

KANUNI YA 3
DARAJA LA LIGI
Kanuni hizi ni kwa ajili ya Ligi Kuu.

KANUNI YA 4
NAMNA YA UENDESHAJI WA LIGI KUU YA VODACOM

Ligi Kuu itashirikisha timu kumi na nne (14) tu yaani timu tisa (11) zilizobaki toka msimu uliopita na timu tatu (3) zilizopanda daraja. 

·      Vilabu vinatakiwa kusajili timu za vijana TFF kabla ya Ligi kuu kuanza;
·      Timu zitacheza Ligi ya mikondo miwili nyumbani na ugenini;
·      Timu tatu (3) za mwisho katika msimamo wa Ligi zitashuka daraja.


KANUNI YA 5
UWANJA WA NYUMBANI NA UGENINI
(1)         Uwanja wa nyumbani ni ule uliochaguliwa na timu husika na uwanja wa ugenini ni ule ambao timu pinzani imekaribishwa kucheza.

(2)         Kutoka na sababu za kiusalama au uwanja kutofikika au sababu nyingine yeyote ya msingi. TFF kwa kushauriana na timu husika Endapo timu yoyote haina uwanja wa nyumbani unaofaa kwa mashindano ya Ligi, timu husika inaweza kuchagua kwa idhini ya TFF, uwanja mwingine wowote, hata nje ya mji huo au Mkoa ili mradi Uwanja huo uwe jirani na mkoa wa timu husika ndani ya Tanzania Bara na uwe na sifa zinazokubalika.

KANUNI YA 6
MSHINDI WA LIGI
(1)         Mshindi katika mchezo wowote wa ligi atapatikana kwa kufunga magoli mengi zaidi ya timu pinzani.

(2)         Mshindi atapata pointi tatu (3)

(3)         Endapo timu zitatoka sare ya aina yoyote, kila timu itapata alama moja.

(4)         Timu itakayoshindwa itakosa pointi.

(5)         Mshindi katika ligi ni timu iliyopata pointi nyingi zaidi ya timu zote zilizoshiriki katika Ligi hiyo.

(6)               Ikiwa timu mbili zitalingana kwa pointi baada ya michezo mshindi atapatikana kwa tofauti bora ya magoli ya kufungwa na kufunga, na kama tofauti hiyo haitoi mshindi, mshindi atakuwa ni mwenye magoli mengi ya kufunga, kama pia magoli ya kufunga hayatoi mshindi; basi mshindi atakuwa ni yule atakayekuwa na pointi nyingi kwenye michezo miwili iliyohusisha timu hizi mbili, na kama pia michezo hiyo haitoi mshindi, mshindi atakuwa yule aliyefunga magoli mengi zaidi katika mchezo wa ugenini uliozihusisha timu hizi mbili, iwapo bado haitoi mshindi, mshindi atakuwa aliyefunga magoli mengi ya ugenini katika msimu mzima, iwapo bado haitoi mshindi timu hizi zitacheza mchezo mmoja katika uwanja utakaochaguliwa na TFF, na taratibu zote za kupata mshindi zitafuatwa kama mchezo wa fainali.

(7)               Mshindi wa kwanza wa Ligi atakuwa bingwa wa Ligi kuu ya Tanzania Bara na atapewa kikombe cha ubingwa.

(8)               Mshindi wa kwanza wa LIGI KUU atawakilisha Tanzania Bara katika mashindano ya Kilabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati.

(9)                Mshindi wa kwanza wa LIGI KUU ataiwakilisha Tanzania Bara katika mashindano ya Kilabu Bingwa Afrika (Champions League). Mshindi wa pili atawakilisha katika kombe la Mabara kwa vilabu iwapo hakutakuwa na FA Cup.

(10)           Wawakilishi wa mashindano ya Kilabu bingwa na Kombe la shirikisho watashiriki katika mchezo wa ufunguzi wa msimu wa ngao ya hisani.

(11)           Timu yeyote itakayochaguliwa kucheza mashindano yatakayoandaliwa ama kuidhinishwa na TFF kutokana na nafasi yao katika ligi kuu itawajibika kucheza.    

KANUNI YA 7
MSIMU WA RATIBA YA LIGI
1.      Kamati ya Utendaji ya TFF itatangaza tarehe za kuanza na kumalizika kwa msimu wa Ligi Kuu.

2.      Ratiba ya Ligi itaandaliwa na kutolewa na TFF angalau mwezi mmoja kabla ya Ligi kuanza.

3.      Ratiba ya Ligi ikishatolewa haitabadilishwa isipokuwa kama kuna dharura au sababu nzito na za msingi.
SURA YA TATU
KANUNI YA 8
TARATIBU ZA MCHEZO
(1)      Kutakuwa na mkutano wa kitaalamu wa maandalizi kabla ya mchezo (pre-match meeting) ambao utafanyika kabla ya mchezo. Mkutano huu utafanyika saa 4.00 asubuhi siku ya mchezo. Kwa sababu maalum, mkutano huu unaweza kupangiwa muda, siku na mahali pengine kama itakavyopendekezwa na Chama cha Mpira cha Mkoa na kuidhinishwa na TFF. Timu zinazocheza siku hiyo pamoja na waamuzi na kamisaa wanatakiwa kuhudhuria.

(2)      Timu yoyote itakayochelewa kufika kwenye Mkutano wa kitaalamu wa maandalizi ‘Pre match meeting’ au itakayoleta watu wasiohusika au wasiokuwa na vitambulisho itatozwa faini ya TShs 100,000/= na timu itakayoshindwa kufika kwa sababu zisizo za msingi itatozwa faini ya TShs 200,000/=.

(i)                 Taarifa ya ukiukwaji wa vipengele hivi itawasilishwa na Kamisaa na Msimamizi wa Kituo.
(ii)               Faini zote zitalipwa mara tu baada ya mchezo kumalizika kwa kukata kwenye mapato ya timu. Endapo mapato ya timu ya mchezo huo hayatoshi watakatwa kwenye mchezo unaofuata.
(3)      (a) Wafuatao ndio wanaotakiwa kufika kwenye mkutano wa maandalizi na vitambulisho vyao vilivyotolewa na TFF, asiyekuwa na kitambulisho hicho hatoruhusiwa kuhudhuria kikao  :-
(i)                Mwalimu msaidizi
(ii)             Mtunza vifaa wa Timu
(iii)           Daktari wa Timu.
(iv)            Meneja wa Timu
.
(b)  Kila timu inatakiwa kufika na vitu vifuatavyo:-
(i)                 Seti moja ya jezi za wachezaji wa ndani pamoja na jezi mbili za walinda milango zenye namba kubwa zinazosomeka zinazoanzia na nambari 1 hadi 52. Endapo rangi za sare za timu zote mbili zitafanana, timu ngeni italazimika kubadilisha sare yake. Endapo moja ya jezi za timu itafanana na jezi za waamuzi, waamuzi watalazimika kubadilisha. Taratibu za mabadiliko ni lazima zijulikane kwenye mkutano wa maandalizi tu.

(4)      Jezi ya mlinda mlango isifanane rangi na jezi za wachezaji wa ndani lakini inaweza kufanana na jezi ya mlinda mlango wa timu pinzani.

(5)      Mchezaji atakayevaa jezi isiyokuwa na nambari mgongoni ama itakayobandikwa kwa plasta au kitu chochote kile hataruhusiwa kucheza.

(6)      Viwanja vyote vitakavyotumika kwa michezo yote vitaidhinishwa na TFF.

(7)      TFF ina madaraka ya mwisho ya kuhamisha mchezo au kubadilisha kituo cha mchezo kwa sababu inazoona zinafaa kwa mchezo au mashindano husika.

(8)      Manahodha wa timu zinazoshindana wanatakiwa kuvaa vitambulisho vya rangi tofauti na jezi zao kwenye mikono ya jezi zao.
(9)      Kila mchezaji ni lazima avae kizua ugoko “shinguard” kwenye miguu yote miwili.

(10)  Wachezaji wanaruhusiwa kushangilia goli kwa wastani. Ushangiliaji wa kupitiliza, kiasi cha kupoteza muda hasa kutoka uwanjani na kufanya ishara yoyote isiyokuwa ya kiuanamichezo au ya kashfa au matusi kwa timu pinzani au watazamaji hairuhusiwi. Mchezaji/wachezaji watakaofanya vitendo hivyo  wataadhibiwa kwa kufungiwa michezo isiyozidi mitatu au faini ya laki moja au vyote kwa pamoja. Mchezaji atakayevua jezi kushangilia ataonyeshwa kadi ya njano.

(11)  Michezo yote ya ligi itachezwa kwa vipindi viwili vya jumla ya dakika tisini (90) kila kipindi kikiwa na dakika arobaini na tano (45) na mapumziko ya dakika zisizopungua tano (5) na zisizozidi kumi tano (15) kati ya vipindi hivyo.

(12)  Timu zinatakiwa kufika kiwanjani si chini ya dakika (60) kabla ya wakati uliopangwa kuanza mchezo. Michezo inayoonyeshwa moja kwa moja na Luninga muda utapangwa kulingana na muda uliokubaliwa na pande zote za mchezo wa siku hiyo na warushaji.

(13)   Timu itakayochelewa kufika kwa mujibu wa masharti ya Kanuni ya 8 Kifungu cha 12; itatozwa faini ya sh. 300,000/=.

(14)  Timu zitakaguliwa kwenye vyumba vyao vya kuvalia na endapo rangi za sare za timu zote zitafanana timu ambayo haikufika kwenye kikao cha maandalizi italazimika kubadili jezi.
(i)                 Kila kilabu itasajili TFF rangi ya jezi zake kwa mechi za nyumbani na ugenini kabla ya kuanza msimu wa Ligi.  Kilabu itakayokiuka itatozwa faini ya Tshs. 300,000/=

(ii)               Vyumba vya kuvalia wachezaji vitapangwa na msimamizi wa kituo, kwa timu ya nyumbani na ugenini. Sehemu ya kufanyia mazoezi na benchi la wachezaji wa akiba itakuwa upande ule ule wa vyumba vya kuvalia.  Kilabu itakayokiuka itatozwa faini ya shilingi za  300,000/=.

(iii)             Ni marufuku kwa viongozi kuingia uwanjani kinyume na taratibu za mchezo kabla, wakati au baada ya mchezo.  Timu itakayokiuka kipengele hiki itatozwa faini ya shilingi 300,000/=.

(iv)             Ni marufuku kwa mashabiki kuingia uwanjani kabla, wakati au baada ya mchezo. Timu itakayokiuka kipengele hiki itatozwa faini ya sh. 300,000/=.

(15)  Endapo timu zitakaguliwa na mgeni rasmi kiwanjani kwa kupeana naye mikono, au timu kupeana mikono zenyewe na waamuzi zitalazimika kufanya hivyo  kwa heshima zote zinazostahili.  Timu itakayokosa kupeana mkono na mgeni rasmi na/au msafara unaoongozana na mgeni rasmi, na/au waamuzi na/au timu pinzani kwa sababu yeyote itatozwa faini ya Tshs. 500,000/=.

(16)  Wakati wa mapumziko, timu zitalazimika kwenda kupumzika kwenye vyumba vyao vya kuvalia.  Timu zinalazimika kupitia kwenye milango/mageti na siyo vinginevyo.  Timu itakayokiuka itatozwa faini ya Tshs. 500,000/=.

(17)  Timu yoyote hairuhusiwi kuruka ukuta wa nje ili kuingia uwanjani (“Stadium”) ama kuruka  uzio wa ndani unaotenga watazamaji na Uwanja (“Pitch”), ama kupita katika mlango wowote usio rasmi.   Endapo timu itafanya hivyo itatozwa faini ya sh. 500,000/=.

(18)  Pamoja na adhabu iliyoainishwa katika Kanuni ya 8 (14, 15, 16 na 17), Shirikisho linaweza kutoa adhabu ikiwemo ya timu husika kupoteza mchezo na kumfungia mchezaji, kiongozi, au shabiki yeyote wa timu husika kwa kipindi kisichopungua miezi mitatu.

(19)   Mwalimu mkuu au mwalimu msaidizi wa timu anatakiwa kuwasilisha kwa Kamishina wakati wa kukaguliwa orodha iliyo na wachezaji 18 na viongozi watano ambao wameorodheshwa katika fomu maalumu iliyoandaliwa na TFF kwa madhumuni hayo. Formu hiyo italazimika kujazwa kwa unadhifu na ukamilifu.

(20)  Timu itatumia wachezaji walioorodheshwa katika fomu hiyo tu, mchezaji ambaye hakuoorodheshwa hatahesabika kama mchezaji wa siku hiyo.

(21)  Wachezaji wote watatambulika kwa kutumia vitambulisho vyao vilivyoidhinishwa na TFF; katika mashindano hayo. Mchezaji yeyote ambaye hatakuwa na kitambulisho hatoruhusiwa kushiriki katika mchezo.

(22)  Iwapo itathibitika bila kujali kukatwa au kutokatwa Rufaa, kupitia taarifa za mchezo za Kamisaa ama kwa njia yoyote kuwa timu imechezesha mchezaji/wachezaji ambao si halali au ni batili kiusajili (non qualified) timu hiyo itapoteza mchezo na ushindi kupewa timu pinzani.

(23)  Timu ambayo itawasilisha fomu isiyo kamili itachukuliwa kuwa haijawasilisha fomu hiyo.

(24)  Endapo timu imeshindwa kuwasilisha fomu iliyotajwa katika Kanuni ya 8 (20) itakuwa imekiuka Kanuni hiyo na timu husika itatozwa faini ya Sh. 100,000/= ambazo zitalipwa kutokana na mchezo au michezo ya timu husika.

(25)  Wanaoruhusiwa kukaa kwenye benchi la wachezaji wa akiba ni wachezaji saba (7) wa akiba na viongozi watano (5) ambao ni mwalimu Mkuu, mwalimu Msaidizi, Daktari, Mchua misuli na Mtunza vifaa  wa Timu.

(26)  Mwamuzi atalazimika kutoanzisha mchezo hadi masharti ya Kanuni ndogo ya (25) ya Kanuni hii yametekelezwa.

(27)  Endapo hata baada ya Mwamuzi kuitaka timu itekeleze masharti ya Kanuni ya 8 (25) timu husika ikashindwa kufanya hivyo; basi timu hiyo itatozwa faini ya sh. 500,000/=. Mwamuzi ataomba msaada wa wanausalama kuwaondoa wasiohusika kabla ya kuanzisha mchezo.

(28)  Mwamuzi na Kamishna wa mchezo wanatakiwa kutoa taarifa zao za maandishi kwa TFF, endapo hali iliyoelezwa katika Kanuni ndogo ya (27) ya Kanuni hii itatokea.

(29)  Chama cha Mpira cha ngazi husika kitapeleka kiwanjani mipira miwili au zaidi yenye sifa zinazokubalika kisheria itakayotumika kwa ajili ya mchezo.  Kila timu inatakiwa kufika kiwanjani angalau na mpira mmoja wenye sifa hizo hizo.

(30)  Ni marufuku kwa timu yoyote kukataa kuchezea mpira wowote uliochaguliwa na mwamuzi.

(31)  Mwamuzi ataanzisha mchezo iwapo tu kama kuna mipira miwili au zaidi yenye sifa zinazokubalika kisheria.

(32)  Endapo timu yoyote itakataa kuchezea mpira wowote uliochaguliwa na mwamuzi na kusababisha mchezo huo kuvunjika, timu hiyo itapoteza mchezo huo na timu pinzani itapata ushindi wa pointi tatu na magoli matatu.

(33)  Endapo timu yoyote itakataa kuchezea mpira wowote uliochaguliwa na mwamuzi na kusababisha mchezo huo kuchelewa kuanza na baadaye mchezo ukalazimika kuvunjwa kabla ya dakika tisini (90) kwisha kwa sababu ya giza timu iliyosababisha mchezo kuvunjika itapigwa faini ya 500,000/=, itapoteza mchezo huo na timu pinzani itapata ushindi wa pointi tatu (3) na magoli matatu (3). 

(34)  Mwamuzi ataanzisha mchezo iwapo kila timu ina wachezaji 11.  Endapo timu yoyote haitimizi wachezaji 11, mchezo unaweza kuanzishwa ikiwa tu wachezaji wa kila timu hawapungui saba (7) mmoja wao akiwa mlinda mlango.  Lakini Kanuni hii haitahusu timu iliyosalia na wachezaji pungufu ya saba kutokana na baadhi yao kuumia au kutolewa nje na mwamuzi wa mchezo.

(35)  Timu inaruhusiwa kubadilisha wachezaji watatu (3) tu wa akiba kutoka kwenye orodha ya wachezaji saba (7) wa akiba.

(36)  Timu zote zinazoshiriki Ligi Kuu pamoja na waamuzi, endapo watapewa na mdhamini, jezi na suti za michezo, timu pamoja na waamuzi wanatakiwa wahakikishe wanavaa vifaa hivi kwenye michezo yote ya Ligi Kuu.

(37)  Iwapo kutakuwa na mdhamini wa ligi Kuu, Nembo ya mdhamini itawekwa mikononii .Wadhamini wengine wote nembo zao zitawekwa mgongoni na kifuwani. Hata hivyo mdhamini binafsi wa klabu ataweka nembo yake kifuani. Timu itakayokuwa na jezi zake italazimika kuweka nembo ya mdhamini katika jezi hizo kwa kufuata utaratibu huo na hairuhusiwi kuweka matangazo ya kampuni nyingine ambayo ina ushindani wa moja kwa moja kibiashara na mdhamini wa Ligi kuu. Matangazo au mabango ya wadhamini  wa klabu yatawekwa kwenye uwanja wa nyumbani (Timu mwenyeji) tu na si uwanja wa ugenini isipokuwa kwa makubaliano maalum kati ya klabu ngeni na mwenyeji.

(38)  Kila Kilabu kinalazimika kuheshimu Mikataba ya udhamini inayowekwa na TFF.  Timu itakayoshindwa kutekeleza kipengele namba 36 na 37 cha kanuni hizi itatozwa faini isiyopungua 1,500,000/= kwa kila mchezo na pia inaweza kuchukuliwa hatua zingine zaidi zikiwemo kupoteza sifa ya kushiriki Ligi kuu  na kufungiwa.

(39)  Mwamuzi ambaye hatovaa jezi na suti ya michezo yenye nembo ya mdhamini ataondolewa katika orodha ya waamuzi wanaochezesha ligi kuu.

(40)  Kilabu chochote kinachotaka kuingia mkataba na mdhamini kinalazimika kuwasilisha rasimu ya mkataba huo kwa TFF kabla ya kutia sahihi.

(41)  Timu itakayokosa kufika uwanjani na kusababisha mchezo kutofanyika baada ya kushiriki kikao cha maandalizi ya mchezo, itatozwa faini ya shilingi 5,000,000/=, kulipa fidia ya uharibifu wowote unaoweza kijitokeza kushushwa daraja na viongozi waliosababisha watachukuliwa hatua zaidi za kinidhamu.
KANUNI YA 9
KUAHIRISHA MCHEZO
Mchezo unaweza kuahirishwa kutokana na sababu yoyote kati ya zifuatazo:-
(a)      Endapo timu ya Taifa ina mchezo.
(b)      Endapo timu inashiriki katika mashindano ya Kimataifa na ina muda usiozidi siku sita kufikia mchezo wa Kimataifa;
(c)      Sababu yoyote ya dharura au/ na yenye msingi itakayokubaliwa na TFF.
(d)      Matukio yasiyotarajiwa wala kusababishwa na timu husika.
(e)      Mchezo wowote ulioahirishwa chini ya kipengele 9 (a),(b) na (c) utapangwa tena katika tarehe itakayoamuliwa na TFF isipokuwa kama utaahirishwa chini ya kipengele 9 (d) utachezwa siku inayofuata iwapo ratiba inaruhusu.
(f)       Iwapo mchezo ulishaanza na kuvunjika kwa sababu ya matukio ya dharura yasiotarajiwa wala kusababishwa na timu husika, utapangwa kurudiwa kwa muda uliosalia, magoli yaliyofungwa katika mchezo huo, Kadhalika kadi walizoonyeshwa wachezaji katika mchezo uliovunjika zitaendelea kuhesabika.
(g)      Taarifa ya maombi ya kuahirisha mchezo ni lazima itolewe kwa maandishi si chini ya siku 14 kabla ya siku ya mchezo, isipokuwa kwa sababu zilizo nje ya uwezo wa binadamu.

KANUNI YA 10
WAAMUZI
Katika mchezo wowote Uamuzi wa Mwamuzi wa mchezo ni wa mwisho.

Kila Mwamuzi atawasilisha TFF mara tu baada ya mchezo taarifa ya mchezo aliouchezesha iliyojazwa katika fomu maalum katika muda usiozidi saa 24.

Taarifa ya Mwamuzi iliyotajwa katika Kanuni ya 10 (2) inatakiwa ijazwe kwa unadhifu na ukamilifu.

Mwamuzi atakayeshindwa kutoa taarifa sahihi ya mchezo kwa mujibu wa Kanuni ya 10 (2) ataondolewa katika orodha ya waamuzi wanaochezesha Ligi kuu na atafungiwa kwa muda usiozidi miezi kumi na mbili (12).

Waamuzi wa mchezo watapangwa na TFF na klabu chochote hakiruhusiwi kumkataa mwamuzi yeyote.

Waamuzi watakaochezesha Ligi ni wale wa Daraja la FIFA na Daraja la kwanza waliofaulu jaribio la utimamu wa mwili (“Physical Fitness Test”) na kuteuliwa kuchezesha ngazi ya Ligi Kuu.

Kutafanyika jaribio la utimamu wa mwili (“Physical Fitness Test”) kila mwaka kabla ya Ligi kuanza ikiambatana na mtihani wa kuandika na mahojiano.

SURA YA NNE
KANUNI YA 11
HUDUMA YA KWANZA NA BIMA
Chama cha Mpira ngazi husika ni lazima kihakikishe kuwa katika mchezo wowote wa Ligi Kuu panakuwepo huduma ya kwanza na gari la wagojwa, kadhalika kihakikishe katika kila mchezo kunakuwepo na Daktari.

KANUNI YA 12
BIMA
(1)      Viongozi na wachezaji wote lazima wawekewe bima na vilabu vyao hati ya bima iwasilishwe pamoja na fomu za usajili wa wachezaji.  Kilabu kitakachokiuka Kanuni hii hakitashirikishwa katika michuano yoyote inayosimamiwa na TFF.

(2)      Chama cha Walimu wa Mpira wa Miguu (TAFCA) kihakikishe kwamba wanachama wake wanawekewa Bima na Vilabu husika.

(3)      Chama cha Madaktari wa Michezo Tanzania (TASMA) kihakikishe kwamba wanachama wake wanawekewa Bima na Vilabu husika.

(4)      Chama cha Wachezaji (SPUTANZA)  kihakikishe kwamba wanachama wake wanawekewa Bima na Vilabu husika.

SURA YA TANO
KANUNI YA 13
ADA YA USHIRIKI NA USIMAMIZI WA LIGI
1.      Ada ya ushiriki wa Ligi Kuu ni TShs 300,000/=.

2.      Kutakuwa na fomu za maombi ya kushiriki kwenye Ligi, tarehe ya mwisho kuthibitisha itatangazwa na TFF. Maombi hayo yataambatana na ada ya ushiriki, maombi yasiyo ambatana na ada hayatapokelewa. Klabu itakayoshindwa kuthibitisha kushiriki hadi kufikia tarehe ya mwisho ya kufanya hivyo itakuwa imejiondoa yenyewe kwenye Ligi na kujishusha daraja.

KANUNI YA 14 A
USIMAMIZI WA LIGI
1.      Ligi kuu itasimamiwa na chombo maalum kilichopewa mamlaka hayo na Kamati ya utendaji ya Shirikisho. Kwa kipindi cha mpito cha kuunda chombo hicho madaraka ya usimamizi wa ligi yatakuwa kwa kamati ya ligi.
KANUNI YA 15 B
KAMATI YA NIDHAMU
Kamati ya nidhamu itatoa maamuzi kwa masuala yote ambayo hayaja ainishwa katika kanuni ya sitini na nne (64).

SURA YA SITA
KANUNI YA 16
KAMATI YA RUFAA
Rufaa zote zinazohusiana na maamuzi ya kamati ya nidhamu zitasikilizwa na kamati ya rufaa:

(1)   Ni marufuku kupeleka malalamiko yoyote dhidi ya TFF kwa masuala yahusuyo soka katika mahakama za sheria. Klabu au mtu yeyote atakayepeleka malalamiko yake katika mahakama za sheria atachukuliwa hatua kali ikiwamo kufutwa kabisa kujishughulisha na mchezo wa soka.

(2)   Endapo mrufani/mrufaniwa hakuridhika na maamuzi ya kamati ya rufaa apeleke shauri lake ‘CAS’

(3)   Muda wa kukata rufaa kwenye Kamati ya Rufaa iwapo mrufani au mrufaniwa hajaridhika na maamuzi ya Kamati ya Nidhamu ni si zaidi ya siku tano za kazi.

KANUNI YA 17 B
RUFANI NA UTARATIBU WAKE

Rufaa zote zinazohusiana na Ligi ya Kuu ya Vodacom zitasikilizwa na kamati ya Rufaa ya TFF chini ya utaratibu ufuatao:        
(1)   Kamati ya Rufaa itasiliza rufaa zote zinazopinga maamuzi ya kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya TFF.
(2)   Ni, marufuku kupeleka malalamiko yoyote  dhidi  ya chama cha mpira ngazi yoyote kwa masuala yahusuyo soka katika mahakama za sheria. Kilabu au mtu yeyote atakayepeleka malalamiko yake katika mahakama za sheria atachukuliwa hatua kali ikiwamo kufutwa kabisa kujishughulisha na mchezo wa soka.
(3)   Muda wa kukata rufaa kwenye Kamati ya Rufaa iwapo mrufani au mrufaniwa hajaridhika na maamuzi ya Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ni si zaidi ya siku tano za kazi baada ya kupata maamuzi ya kamati ya Nidhamu na Usuluhishi.
(4)   Rufani ya kupinga maamuzi ya kamati ya Nidhamu na Usuluhishi iwasilishwe kwa maandishi kwenye ofisi za  Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania sio zaidi ya siku tano za kazi baada ya kupata maamuzi ya kamati ya nidhamu na usuluhishi na iwe imeambatanishwa na ada ya rufaa pamoja na vielelezo vyote vya shauri hilo.
(5)   Rufani yeyote itayowasilishwa bila ya vielelezo haita sikilizwa.
(6)   Rufani yeyote ambayo haitalipiwa ada haitasikilizwa.
(7)   Rufani yoyote itakayowasilishwa baada ya muda uliowekwa chini ya kanuni hii, haitasikilizwa na ada ya rufaa haitarudishwa kwa mrufani.

KANUNI YA 18
UTARATIBU WA KUWASILISHA MALALAMIKO.
(a)      Malalamiko dhidi ya matukio  ya mchezo yawasilishwe kwa maandishi kwa Kamishna wa mchezo au ofisi ya TFF sio zaidi ya masaa 24 baada ya mchezo kumalizika.

(b)     Kamishna wa mchezo atawasilisha kwenye Sekretarieti ya TFF sio zaidi ya saa ishirini na nne (24) tangu kupokea malalamiko hayo.

(c)      Kamati husika itaketi kusikiliza na kuyatolea uamuzi malalamiko hayo katika kipindi kisichozidi wiki moja,  baada ya kupata vielelezo husika. Mlalamikaji atawasilisha vielelezo kuhusu malalamiko yake na malalamiko yasiyokuwa na vielelezo hayatasikilizwa.

(d)     Malalamiko yoyote yatakayowasilishwa baada ya muda uliowekwa chini ya kanuni hii, hayatasikilizwa.

KANUNI YA 19
ADA ZA RUFAA

Ada ya rufaa katika Kamati ya Rufaa ni TShs 500,000/=

SURA YA SABA
KANUNI YA 20
MGAWANYO WA MAPATO

Kila timu itajihudumia yenyewe, timu zilizocheza zitagawana asilimia 59 ya mapato ya mchezo baada ya kutoa gharama za awali.

Mgawanyo wa mapato ya mchezo utakuwa kama ifuatavyo:-
 Jumla ya Pato                                                                                   xxxx
 Toa 18% VAT                                                                                    xxxx
Toa: Usafiri wa ndani na Posho ya waamuzi, kamisaa,
msimamizi wa waamuzi na msimamizi wa   kituo                             xxxx
Maandalizi ya uwanja                                                                                    xxxx
  Gharama za Tiketi                                                                             xxxx    
                Baki ya Pato                                                                                  xxxx
             9% Gharama za mchezo;                                                                    xxxx                            
             9% Msimamizi wa Ligi Kuu                                                               xxxx
             4.5% FDF;                                                                                         xxxx
             15% Uwanja;                                                                                      xxxx
               3.5% FA (M)                                                                                                xxxx
              29.5% Klabu ngeni                                                                            xxxx
              29.5% klabu mwenyeji                                                                      xxxx

3.      Endapo timu moja itahamia uwanja wa Mkoa mwingine mbali ya ule wa nyumbani sehemu ya mapato ya 3.5% ya Chama cha Mpira cha Mkoa  itagawanywa kama ifuatavyo:
(a)    Mkoa unaotoka timu husika utapata nusu ya 1.75%
(b)    Mkoa utakaohusika na uwanja utapata nusu ya 1.75%

4.      Msimamizi wa Kituo atawasilisha taarifa ya mapato na fedha za mchezo husika kwa TFF katika muda usiozidi masaa 24. Kiongozi au Msimamizi atakayeshindwa kuwasilisha atachukuliwa hatua kwa mujibu wa Kanuni za TFF.

5.      ( i)        Gharama za Waamuzi na kamisaa ni nauli ya kutoka kwenye Kituo alichotokea,
usafiri wa treni Daraja  la Pili, Basi au Meli.
(ii)        Usafiri wa ndani wa Waamuzi kwa ujumla wao Sh. 20,000/= na kamisaa 20,000/=.
(iii)       Chakula na malazi 70,000/= kwa kila mwamuzi na kamisaa.
(iv)       Mwamuzi wa mezani atalipwa Sh. 50,000/=.
(v)               Kamisaa atalipwa posho ya mchezo Sh. 100,000/=
(vi)             Mwamuzi na wasaidizi wawili (2) watalipwa posho ya mchezo Sh. 100,000/= kwa kila mmoja.
(vii)           Posho zilizotajwa kwenye kipengele No . (i) hadi (iv) cha kanuni hii zitalipwa kutoka katika mapato ya mchezo. Posho zilizotajwa kwenye kipengele No. (v) na (vi) zitalipwa na mdhamini wa ligi.

KANUNI YA 21
GHARAMA ZA MCHEZO
1.  Asilimia 9% ya gharama za mchezo itatumika kulipia gharama zifuatazo:-
(i)                 Gharama za msimamizi wa kituo.
(a)     Msimamizi kutoka nje ya kituo atalipwa gharama za kula na kulala 70,000/= na nauli kutoka kituo chake na kurudi.

(ii)               Malipo ya ulinzi, vijana wanaookota mipira, huduma ya kwanza, vinywaji, wasimamizi, wauzaji na wachanaji tiketi, matangazo na “stationari”.

(iii)             Msimamizi mkazi atalipwa shilingi laki moja (100,000/=) za posho na shilingi elfu ishirini (20,000/=) kama usafiri wa ndani. Msimazi kutoka nje atalipwa shilingi 100,000/=, usafiri wa ndani shilingi  20,000/= na nauli ya kwenda na kurudi.

2.  Mtiririko wa gharama hizo utaonyeshwa kwenye Fomu ya Mapato, msimamizi wa kituo atawajibika na usimamizi wa gharama za mchezo.

Malipo yatalipwa kwa hundi kama Kanuni za fedha zinavyosema isipokuwa waamuzi na makamisaa.

Iwapo gharama halisi ni pungufu ya 9% zilizokatwa kama gharama za mchezo, fedha zitakazobaki zitagawanywa nusu kwa nusu kati ya vilabu na TFF, yaani TFF itachukua 50% na vilabu vitagawana 50% nyingine.  Mgawanyo wa fedha hizi unatakiwa uandikwe kwenye fomu ya gharama za mchezo isainiwe na msimamizi wa kituo kwa niaba ya TFF na wawakilishi wa vilabu kwa niaba ya vilabu vyao.

SURA YA NANE
KANUNI YA 22
KUJITOA KATIKA LIGI
(1)      Endapo Kilabu chochote kina nia ya kujitoa katika Ligi kwa sababu zozote zile za msingi ni lazima itoe taarifa ya maandishi kwa TFF kikieleza sababu zinazokilazimisha kilabu hicho kijitoe, siku thelathini kabla ya ligi kuanza.
(2)      Endapo TFF imekubali kujitoa kwa kilabu chochote, klabu kingine ambacho awali kilikuwemo katika daraja hilo lakini kiliteremka kwa mujibu wa msimamo wa Ligi, kitarudishwa kuziba pengo.  Kilabu hicho ni kile kilicho katika nafasi ya juu kuliko vilabu vingine vyote vilivyoteremka daraja katika msimu huo.

(3)      Kilabu kilichojitoa kitateremka daraja.

(4)      Kilabu chochote kitakachojitoa katika Ligi baada ya Ligi kuanza au kushindwa kucheza mchezo mmoja katika msimu mmoja wa Ligi kitakabiliwa na adhabu zifuatazo:

(a)      Kitateremka daraja na kufungiwa kucheza Ligi kwa misimu 2. Kamati ya Utendaji ya TFF pia inaweza kukichukulia hatua zaidi klabu hicho/viongozi au wachezaji iwapo itathibitika kuwa kimejitoa kwa madhumuni ya kuhujumu msimamo wa Ligi au hujuma nyingine yoyote.

(b)      Iwapo klabu zitakazojitoa au kushindwa kumaliza Ligi kwa sababu yoyote ile zitakuwa ni zaidi ya tatu (3) kama kanuni za Ligi za timu kushuka daraja zinavyosema; timu zote hizo zitashuka daraja na timu zaidi zitapanda kutoka daraja la kwanza ili kujaza nafasi na idadi ya timu za Ligi kuu kuendelea kuwa 14.

(c)      Matokeo ya michezo yote iliyowahi kuchezwa yatafutwa lakini kitakuwepo kwenye orodha ya msimamo wa ligi.

(d)      Magoli yaliyofungwa na wachezaji wa timu iliyojitoa katika ligi yatafutwa na hivyo wachezaji wake hawataweza kushindana katika ufungaji bora hata kama walifunga magoli mengi lakini magoli yaliyofungwa na wachezaji wa timu pinzani dhidi ya timu iliyojitoa kwenye ligi hayatafutwa na hivyo yataendelea kuonekana katika idadi ya magoli yaliyofungwa na wachezaji hao lakini hayataonekana katika idadi ya magoli yaliyofungwa na klabu zao 

KANUNI YA 23
KUTOFIKA KITUONI/UWANJANI
Timu yoyote itakayokosa kufika kituoni na kusababisha mchezo usifanyike itakabiliwa na adhabu zifuatazo:
(a)      Itapoteza ushindi na kushushwa madaraja mawili na matokeo ya michezo yake yote yatafutwa ili kutoa uwiano sahihi kwa timu zilizobaki kwenye mashindano, na endapo timu ilikuwa kwenye kushuka daraja timu hiyo husika itashushwa madaraja mengine.

(b)     Itatozwa faini ya TShs 3,000,000/= ambazo kati ya hizo Tshs 1,500,000/= itaenda TFF na TShs 1,500,000/= itaenda kwa timu pinzani.

(c)      Itapoteza haki ya kuchukua sehemu yake ya mapato ya mchezo huo.

(d)     Kiongozi yeyote atakayebainika kuwa alishiriki, alishawishi au alikuwa chanzo cha mgomo huo atafungiwa kwa kipindi cha miezi kumi na miwili.

(e)      Inaweza ikakabiliwa na adhabu zaidi kama ambavyo Kamati ya Utendaji itaona inafaa.

(f)       Timu yoyote iliyopewa adhabu ya faini chini ya aya ya (b) ya Kanuni hii haitaruhusiwa kucheza hadi itakapotekeleza adhabu hiyo kwa daraja ambalo itakuwa ipo.

KANUNI YA 24
KUVURUGA MCHEZO
1.       Wachezaji na viongozi wa timu itakayosababisha mchezo kuvurugika na hatimaye kuvunjwa, itapoteza mchezo huo hata kama ilikuwa inaongoza kwa magoli na timu pinzani itapewa ushindi wa pointi tatu na magoli matatu, iwapo timu pinzani inaongoza kwa magoli zaidi ya matatu, itabakia na idadi ya magoli hayo iliyokwishafunga.

2.       Magoli yaliyofungwa na wachezaji wa timu iliyosababisha mchezo kuvunjika yatafutwa lakini magoli yaliyofungwa na timu pinzani hayatofutwa na yataendelea kuonekana katika idadi ya magoli yaliyofungwa na wachezaji wa timu hiyo wakati wa kutafuta mfungaji bora.

3.       Endapo itatokea vurugu ya aina yoyote ile na kusababisha mchezo kusimama, mwamuzi atasubiri kwa dakika zisizozidi kumi na tano, na endapo hali ya vurugu bado inaendelea mwamuzi atavunja mchezo na kuwasilisha taarifa ya mchezo kwa kamati ya Usimamizi ya ngazi husika.

4.       Timu iliyosababisha vurugu itapoteza mapato yote ya mchezo.

5.       Timu iliyosababisha kuvurugika kwa mchezo italipa faini ya shilingi 1,000,000/=.

6.            Faini hiyo italipwa kabla ya mchezo unaofuatia.

7.            Mchezaji/wachezaji na kiongozi/viongozi watakao bainika kusababisha vurugu zilizopelekea mchezo huo kuvunjika watafungiwa kujihusiha namasuala yote ya mpira kwa kipindi cha miaka mitano.


8.            Endapo uvunjikaji wa mchezo utakuwa nje ya kanuni ya 22(3), mchezo huo utarudiwa kama inavyoainishwa katika kanuni ya 9(e) na utachezeshwa na waamuzi wengine katika siku itakayo pangwa na chombo husika.

KANUNI YA 25
KUPANGA MATOKEO
1.       Endapo timu zozote zitabainika kuwa zimepanga kwa namna yoyote ile matokeo ya mchezo wowote waliocheza kwa madhumuni yoyote yale zitachukuliwa hatua zifuatazo:-

2.       Matokeo ya mchezo huo yatafutwa; na kila timu itatozwa faini ya shilingi millioni tano (5,000,000/=).

3.       Timu zitateremshwa hadi ligi ya wilaya;

4.       Viongozi wa timu hizo waliohusika na njama za kupanga matokeo watafungiwa kwa kipindi cha miaka mitano;

5.       Iwapo timu husika itashindwa kulipa faini basi timu hiyo haitapangwa katika mchezo wa ligi msimu unaofuata.

SURA YA TISA
UDHIBITI WA MIENENDO NA ADHABU KWA WACHEZAJI, WAAMUZI NA VIONGOZI

KANUNI YA 26
UCHEZAJI WA KIUNGWANA (FAIR PLAY)

Wachezaji wanatakiwa kuzingatia kanuni za mchezo wa kiungwana ‘fair play’ ndani na nje ya uwanja wa mchezo. Kanuni 10 za FIFA za mchezo wa kiungwana ni kama ifuatavyo:

i.      Cheza Kiungwana – Ushindi hauwezi kuwa na thamani iwapo umepatikana katika njia isiyo halali au kwa udanganyifu. Kudanganya ni rahisi lakini haileti raha ya ushindi. Kucheza kiungwana inahitaji moyo na tabia njema. Pia hufurahisha zaidi. Mchezo wa kiungwana siku zote una malipo yake hata kama utapoteza mchezo. Kucheza kiungwana kunakujengea heshima wakati kudanganya kunaleta aibu. Kumbuka kuwa mpira wa miguu ni mchezo na mchezo wowote hauwezi kuwa na maana kama hautochezwa kiungwana kwa kuzingatia kanuni na taratibu ili mshindi halali aweze kupatikana.

ii.      Cheza kwa nia ya kutafuta ushindi lakini pia kuwa tayari kukubali kushindwa – Kushinda ndiyo lengo la kushiriki katika mchezo wowote ule. Siku zote usijiandae kushindwa. Iwapo huchezi kwa nia ya kushinda utakuwa unawadanganya wapinzani wako, unawadhulumu watazamaji na pia unjifanya mwenyewe kuwa ni mjinga. Usikate tamaa hata siku moja unapombana na wapinzani wenye nguvu zaidi lakini pia usidharau hata siku moja unapombana na wapinzani dhaifu. Ni kumkosea adabu mpinzani unapocheza chini ya kiwango chako. Cheza kwa nia ya kutafuta ushindi hadi dakika ya mwisho lakini kumbuka hakuna anayeshinda wakati wote. Siku nyingine utashinda na siku nyingine utashindwa. Jifunze kukubali kushindwa. Usitafute visingizio unapofungwa. Sababu za kweli siku zote zitadhihirika. Wapongezi washindi bila kinyongo. Usilaumu waamuzi wala mtu mwingine yoyote. Jizatiti kufanya vizuri zaidi wakati mwingine. Walioshindwa na kukubali wanapata heshima kubwa kuliko washindi wanaolazimisha.

iii.      Heshimu sheria za mchezo – Michezo yote inalindwa na sheria. Bila sheria itakuwa ni vurugu. Sheria za mpira wa miguu ni nyepesi na rahisi kujifunza. Hakikisha unajifunza; itakusaidia kuufahamu mpira wa miguu vizuri zaidi. Kuufahamu mchezo zaidi itakufanya uwe mchezaji bora zaidi. Pia ni muhimu kufahamu madhumuni ya sheria zilizowekwa. Zimekusudiwa kuufanya mchezo uwe na ladha katika kuucheza na pia uwe na ladha katika kuuangalia. Kwa kufuata sheria, mchezo wa mpira wa miguu utakuwa na burudani zaidi.

iv.      Heshimu wapinzani, wachezaji wenzako, waamuzi, viongozi na watazamaji – Mchezo wa kiungwana unamaanisha kuheshimu wapinzani. Bila ya wapinzani kutakuwa hakuna mchezo. Kila mmoja ana haki sawa, ikiwemo haki ya kuheshimiwa. Wachezaji wa timu moja ni wenza. Tengeneza timu ambayo kila mmoja kwenye timu atakuwa na haki sawa. Waamuzi wapo kuhakikisha nidhamu na mchezo wa kiungwana unadumishwa. Siku zote kubali maamuzi yao bila ya ulalamishi, na wasaidie waweze kuwafanya washiriki wote waufurahie zaidi mchezo. Viongozi pia ni sehemu ya mchezo na wanatakiwa wapewe heshima wanayostahili. Watazamaji wanaufanya mchezo uwe na msisimko. Wanahitaji kuuona mchezo ukichezwa kiungwana kwa kuzingatia kanuni, lakini pia wanatakiwa kuwa waungwana na kujiheshimu.

v.      Dumisha Maslahi ya mchezo wa mpira wa miguu – Mpira wa miguu ndiyo mchezo unaoongoza duniani kwa kuwa na wapenzi wengi. Lakini siku zote unahitaji msaada wa kila mmoja kuufanya uendelee kuwa mchezo wenye kupendwa zaidi. Fikiria maslahi ya mpira kabla ya maslahi yako mwenyewe. Fikiria ni vipi vitendo vyako vinaweza vikaupaka matope mchezo wa mpira wa miguu. Zungumzia mambo mazuri ya mchezo wa mpira wa miguu. Shawishi watu wengine kuuangalia na kuucheza kiungwana. Wasaidie wengine kupata burudani ya kutosha katika mchezo wa mpira wa miguu kama unayoipata wewe. Kuwa balozi wa mchezo wa mpira.   

vi.      Waheshimu wale wanaolinda heshima ya mchezo wa mpira wa miguu – Jina zuri la mchezo wa mpira wa miguu limeendelea kudumu kwa sababu idadi kubwa ya watu wenye kuupenda mchezo huu ni wakweli na waungwana. Wakati mwingine mtu hufanya jambo kubwa ambalo linastahili tulitambue. Watu kama hawa wanastahili kutuzwa na mambo mema waliyofanya yatangazwe. Hii itashawishi wengine kuiga mifano yao. Saidia kuendeleza mpira wa miguu kwa kuyatangaza mazuri yake.

vii.      Kataa rushwa, madawa, ubaguzi, fujo, kamari na mambo mengine ya hatari kwa mchezo wetu – Umaarufu mkubwa wa mchezo wa mpira wa miguu wakati mwingine huufanya uwe rahisi kuathiriwa na mambo mabaya ya nje. Jichunge na vishawishi vitakavyokufanya ushawishike kushiriki kwenye kudanganya au kutumia madawa yaliyokatazwa. Madawa yaliyokatazwa hayana nafasi katika soka wala mchezo mwingine wowote na jamii kwa jumla. Sema hapana kwa madawa ya kulevya. Saidia kuupiga teke ubaguzi kwenye soka. Wachukulie wachezaji wote na wengineo kuwa ni sawa bila kujali dini, kabila, jinsia au utaifa wao. Usivumilie hata kidogo kamari katika michezo unayoshiriki. Inaporomosha kiwango chako cha uchezaji na inasababisha hali ya mgongano wa maslahi. Thibitisha kuwa soka haihitaji fujo, hata kutoka kwa washabiki wako wenyewe. Soka ni mchezo na michezo huleta amani.

viii.      Wasaidie wengine kupambana na mashinikizo ya upokeaji rushwa – Wakati mwingine unaweza kusikia wachezaji wenzako au watu wengine unaowafahamu wanashawishiwa wadanganye kwa njia moja au nyingine au washiriki katika vitendo visivyokubalika katika mchezo wa soka. Wanahitaji msaada wako. Usisite kusimama upande wao. Wape nguvu ya kukataa vishawishi. Wakumbushe wajibu wao kwa wenzao na kwa mchezo wenyewe. Tengeneza umoja wenye mshikamano, kama ngome ngumu kabisa kwenye mchezo wa soka.

ix.      Wabainishe wale wanaojaribu kuuchafua mchezo wetu – Usione aibu kusimama dhidi ya yoyote yule ambaye una hakika anashawishi wengine kudanganya au kushiriki katika vitendo vingine visivyokubalika. Ni vyema kuwafichua waovu wote ili waweze kuondolewa kabla ya kuleta madhara. Ni uovu kushirikiana na watu waovu. Usiseme tu hapana, wafichue wanaotaka kuichafua soka kabla hawajafanikiwa kuwashawishi wengine.

x.      Tumia soka kujenga dunia bora zaidi – Soka ina nguvu ya ajabu ambayo inaweza kutumika kuifanya dunia hii ikawa sehemu bora zaidi ya kuishi. Tumia nguvu hii kudumisha amani, usawa, afya na elimu kwa wote. Ifanye soka iwe bora zaidi, ipeleke kwa jamii na utakuwa unajenga dunia bora zaidi.
Pamoja na kanuni za Fair Play za FIFA, kadhalika wachezaji wanatakiwa kuzingatia yafuatayo:

a)      Nidhamu – kudumisha tabia njema nje ya uwanja na wakati wote wa mchezo kwa kucheza bila ya kuwaumiza au kuhatarisha usalama wa wachezaji wa timu pinzani.

b)      Mchezo wa kiungwana – Kutodanganya kuumia au kufanyiwa rafu, kutotumia mbinu zisizo za kiungwana mchezoni au kujiingiza katika vitendo visivyokuwa vya kiunamichezo kama vile kutukana kwa maneno, ishara au kujihusisha na vitendo vyovyote vya kibaguzi.

c)     Kutorejeshea kutorejeshea ‘retaliation’ iwapo mchezaji atafanyiwa rafu au kukashifiwa.

d)     Malalamiko – Ni nahodha pekee ambaye anaruhusiwa kuzungumza na waamuzi. Iwapo patatokea malamiko yoyote wakati wa mchezo wachezaji wengine wote wanatakiwa wawe hatua zisizopungua kumi kutoka kwa mwamuzi.

e)     Kumheshimu Kocha – Mchezaji wakati wote anatakiwa atii maagizo ya kocha wake. Mchezaji anatakiwa akubali kubadilishwa uwanjani na kuadhibiwa kutokana na vitendo vya utovu wa nidhamu au visivyokuwa vya kiuanamichezo.
f)       Kumheshimu nahodha – Mchezaji anatakiwa amheshimu na atii maagizo ya nahodha wake nje na ndani ya uwanja hususan katika masuala yahusuyo timu na tabia njema kwa jumla.
g)     Kuheshimu wachezaji – Mchezaji anatakiwa awaheshimu wachezaji wenzake na awatie hamasa nje na ndani ya uwanja. Mchezaji anatakiwa asimkashifu mchezaji mwenzake mwenye kufanya makosa.
h)     Kuheshimu wapinzani – Mchezaji anatakiwa awape wachezaji wa timu pinzani heshima yao, awe tayari kutoa msaada kwa mchezaji aliyeumia na kushikana mikono kabla na baada ya mchezo.      
i)       Kuheshimu waamuzi – Mchezaji anatakiwa wakati wote kuheshimu maamuzi ya waamuzi na kutozozana nao au kutumia lugha ya matusi au kashfa dhidi yao.
j)       Kujiheshimu mwenyewe – Mchezaji anatakiwa ajiheshimu mwenyewe na ajitunze na asitumie madawa yaliyokatazwa.

KANUNI YA 27
UDHIBITI WA WACHEZAJI

(1)      TFF itadhibiti mienendo ya wachezaji kwa kuchukua hatua kama ifuatavyo:-
(a)      Mchezaji atakayetolewa nje kwa kadi nyekundu baada kupata kadi mbili za njano katika mchezo wa ligi hataruhusiwa kucheza mchezo mmoja unaofuata wa timu yake.

(b)     Mchezaji atakayetolewa nje kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja (straight red) atakosa michezo miwili.

(c)      Mchezaji atakayetolewa nje kwa kadi nyekundu kwa kosa la kupiga/kupigana atasimama kushiriki michezo (3) mitatu inayofuata ya kilabu yake na atalipa faini ya shilingi za laki (500,000/=) tano za kitanzania.

(d)     Timu ambayo wachezaji wake wataonyeshwa kadi zaidi ya tano katika mchezo mmoja itatozwa faini ya shilingi za kitanzania laki tano (500,000/=).    

(e)      Mchezaji atakayeonywa kwa kadi ya njano katika michezo mitatu hataruhusiwa kucheza mchezo mmoja unaofuata.

(f)        Kilabu itakayomchezesha mchezaji mwenye kadi 3 za njano au kadi nyekundu itapoteza mchezo na timu pinzani itapewa ushindi wa pointi 3 na magoli 3, iwapo mchezaji atacheza akiwa anatakiwa kutocheza kwa ajili ya kadi tatu za njano au kadi nyekundu timu yake itapoteza mchezo. Endapo kilabu haina uhakika au inataka taarifa ya idadi ya kadi zake itaomba kwa maandishi toka TFF.

(g)      Mchezaji yeyote atakayefanya jambo lolote kati ya haya yafuatayo ataadhibiwa kwa kufungiwa michezo isiyopungua mitatu (3) na faini isiyopunguwa Tshs; 500,000/=:

(i)              Kuto kujiunga na Timu ya Taifa kwa sababu yoyote isiyo ya msingi  .

(ii)            Kupigana/kupiga kabla au mara tu baada ya mchezo kumalizika.

(iii)          Kumshambulia mwamuzi, kiongozi, mtazamaji au mtu  yoyote kwa namna yoyote ile, iwe kwa matusi au kwa vitendo.

(iv)          Kufanya kitendo chochote cha aibu, kama vile kukojoa kiwanjani, kukataa kupeana mkono na mgeni rasmi, waamuzi na wachezaji wa timu pinzani, kutoa matusi au kuonyesha ishara yoyote inayoashiria matusi;  

(v)               Kusababisha kuvurugika kwa amani kiwanjani kabla au baada ya mchezo;

(vi)      Kufanya vitendo vyenye kuonyesha imani za ushirikina na uchawi hadharani; kama vile kuvunja nazi, kupasua mayai, kufukia hirizi na kumwaga maji ya makombe n.k.

 (vii)     Kufanya kitendo chochote kinyume cha maadili ya mchezo wa mpira. Kwa mfano kuruka uzio badala ya kupita kwenye mlango maalum.

(viii)         Timu yoyote itakayomchezesha mchezaji aliye chini ya adhabu kwa mujibu wa Kanuni hii itapoteza mchezo huo na timu pinzani itapewa ushindi.
(ix)              Mchezaji sugu atafungiwa kushiriki mashindano yeyote kwa miezi isiyopunguwa mitatu (3) na faini isiyopunguwa Tshs: 1,000,000/= (milioni moja)

(h)    Mchezaji yoyote atakayetakiwa kufanya vipimo vya dawa za kulevya au kuongeza nguvu, anawajibika kufanya hivyo, endapo atagundulika/atakataa kuwa anatumia madawa ya kulevya au kuongeza nguvu/kufanya hivyo atafungiwa kwa kipindi cha miezi kumi na mbili (12).

KANUNI YA 28
UDHIBITI NA ADHABU KWA WAAMUZI

1.   Mwamuzi yeyote atakayefanya jambo lolote kati ya haya yafuatayo ataadhibiwa kama ilivyoainishwa katika Kanuni hii:-

(a)      Akishindwa kumudu mchezo kwa uzembe, woga au kutozingatia sheria kiasi cha kuvuruga mchezo, kuhatarisha amani, atafungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi sita (6) na kisichozidi miezi kumi na miwili (12).

(b)     Akichelewa kwa zaidi ya saa ishirini na nne (24) kutuma taarifa ya mchezo bila sababu za msingi ataadhibiwa kwa mujibu wa kanuni ya 10 kipengele cha 4.

(c)      Akibainika kuwa anadai hongo au amepokea/ametoa hongo /au kuhusika na matendo yeyote yanayo ashiria hongo ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa ya mpango wa hongo, kutoa taarifa ya mchezo isiyo sahihi kwa makusudi atafungiwa miaka mitatu au maisha.

(d)     Akishindwa kufika au akichelewa kufika bila sababu ya msingi au kutotoa taarifa, kwenye kituo cha mchezo alichopangiwa kiasi cha kusababisha ratiba ya waamuzi kurekebishwa au mchezo kuahirishwa, ataondolewa kwenye orodha ya waamuzi na atafungiwa kwa kipindi kati ya miezi 3 - 12.

(e)      Akifanya kitendo chochote ambacho ni kinyume cha maadili ya taaluma ya uamuzi kama vile kuhudhuria kikao cha maandalizi ya awali ya mchezo husika/au kuchezesha mchezo husika akiwa amelewa atafungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi kumi na miwili (12).

(f)       Mwamuzi atakayemaliza mchezo kabla ya wakati/au atakayeongeza muda wa mchezo bila ya sababu za msingi atafungiwa kati ya miezi 6 – 12.

(g)      Mwamuzi atakaebainika kushirikiana na Kamisaa kuandika taarifa ili kuficha ukweli ataondolewa katika orodha ya waamuzi wa Ligi Kuu na atafungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi 24.

(h)     Mwamuzi akitoa visingizio visivyokua na msingi ili kukwepa mchezo aliopangiwa atondolewa kwenye orodha ya waamuzi wa Ligi Kuu na Kamati inaweza kutoa adhabu nyingine itakavyoona inafaa.

KANUNI YA 29
UDHIBITI WA KAMISHINA
1.   Kamishina yeyote atakayefanya jambo lolote kati ya haya yafuatayo ataadhibiwa kama ilivyoainishwa katika Kanuni hii:-

(a)                Kamishna atakayeshindwa kutoa taarifa ya mchezo ikiwemo taarifa ya mchezaji bora wa mchezo husika au akitoa taarifa isiyokuwa sahihi, ataondolewa kwenye orodha ya makamishna wa michezo na atafungiwa kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja.

(b)               Kamishna atakayeshindwa kutoa taarifa katika muda wa saa 24 ataondolewa katika orodha ya makamishna wa michezo na atafungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi sita (6).

(c)                Akibainika kuwa anadai hongo au amepokea/ametoa hongo /au kuhusika na matendo yeyote yanayo ashiria hongo ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa ya mpango wa hongo, kutoa taarifa ya mchezo isiyo sahihi kwa makusudi atafungiwa miaka mitatu au maisha.

(d)               Kamishna atakayebainika kukataa kupokea Rufaa kwa sababu zisizokuwa za msingi kwa njia yoyote ile, atafungiwa kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja.

(e)                Akifanya kitendo chochote ambacho ni kinyume cha maadili ya taaluma ya ukamishina kama vile kuendesha kikao cha maandalizi ya awali ya mchezo husika/au kusimamia mchezo husika akiwa amelewa atafungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi kumi na miwili (12).

(f)                 Kamisaa atakaye bainika kushirikiana na mwamuzi kuandika taarifa ili kuficha ukweli ataondolewa katika orodha ya Makamisaa na atafungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi 24.

(g)                Kamisaa atayebainika kuendesha kikao cha matayarisho na viongozi wa timu wasiohusika (kanuni 8(3)) ataondolewa kwenye orodha ya makamisaa.

(h)               Kamisaa akitoa visingizio visivyokua na msingi ili kukwepa mchezo aliopangiwa atondolewa kwenye orodha ya makamisaa wa Ligi Kuu na Kamati inaweza kutoa adhabu nyingine itakavyoona inafaa.

KANUNI YA 30
UDHIBITI WA MTATHIMINI WA WAAMUZI
(“REFEREE  ASSESOR’’)
1.   Mtadhimini wa waamuzi yeyote atakayefanya jambo lolote kati ya haya yafuatayo ataadhibiwa kama ilivyoainishwa katika Kanuni hii:-

(a)                Mtathimini atakayeshindwa kutoa taarifa ya mchezo au akitoa taarifa isiyo sahihi, ataondolewa kwenye orodha ya watathimini wa michezo na atafungiwa kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja.

(b)               Mtathimini atakayeshindwa kutoa taarifa katika muda wa saa 24 ataondolewa katika orodha ya watathimini wa michezo na/au atafungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi sita (6).

(c)                Akibainika kuwa anadai hongo au amepokea/ametoa hongo /au kuhusika na matendo yeyote yanayo ashiria hongo ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa ya mpango wa hongo, kutoa taarifa ya mchezo isiyo sahihi kwa makusudi atafungiwa miaka mitatu au maisha.

(d)               Mtathimini atakaye bainika kushirikiana na mwamuzi/kamisaa kuandika taarifa ili kuficha ukweli ataondolewa katika orodha ya watathimini na atafungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi 24.

(e)                Akifanya kitendo chochote ambacho ni kinyume cha maadili ya taaluma ya utathimini wa waamuzi  kama vile kuhudhuria kikao cha maandalizi ya awali ya mchezo husika/au kufanya tathimini ya mchezo husika akiwa amelewa atafungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi kumi na miwili (12).

(f)                Mtathimini akitoa visingizio visivyokua na msingi ili kukwepa mchezo aliopangiwa atondolewa kwenye orodha ya watathimini wa michezo na Kamati inaweza kutoa adhabu nyingine itakavyoona inafaa.

KANUNI YA 31
UDHIBITI WA WALIMU
1.      Mwalimu yeyote atakayefanya jambo lolote kati ya haya yafuatayo ataadhibiwa kwa mujibu wa Kanuni hii:-
(a)      Akimshambulia mwamuzi, mchezaji au kiongozi yeyote, kwa maneno au vitendo, kabla, wakati au baada ya mchezo, atatozwa faini isiyopungua shilingi laki tano (500,000/-) na kufungiwa michezo isiyopungua mitatu (3), bila ya kujali adhabu yoyote iliyotolewa na mwamuzi kiwanjani.

(b)     Akitoa kauli au ishara inayoashiria au kushawishi shari kabla, wakati au baada ya mchezo atatozwa faini isiyopungua laki tano (500,000/=) na kufungiwa michezo isiyopungua mitatu (3).

(c)      Akibainika kuwa anadai hongo au amepokea/ametoa hongo /au kuhusika na matendo yeyote yanayo ashiria hongo ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa ya mpango wa hongo, kutoa taarifa ya mchezo isiyo sahihi kwa makusudi atafungiwa miaka mitatu au maisha.

(d)     Akijishirikisha na vitendo vyovyote vile vinavyoashiria imani za uchawi au ushirikina atatozwa faini isiyozidi shilingi laki tatu (300,000/=) na kufungiwa michezo isiyopungua miwili (2).

(e)      Akifanya kitendo chochote ambacho ni kinyume cha maadili ya taaluma ya ualimu wa mpira wa miguu kama vile kuhudhuria kikao cha maandalizi ya awali ya mchezo husika/au kusimamia benchi la ufundi katika mchezo husika akiwa amelewa atafungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi kumi na miwili (12).

(f)       Akibainika kugushi sahihi ya mchezaji au kufanya tendo lolote kwa lengo la kukamilisha zoezi la usajili kwa udanganyifu atafutwa katika ordha ya waalimu, leseni yake itatwaliwa na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
(g)      Mwalimu atakayebainika kusababisha timu kutofika uwanjani na kukosa mchezo, baada ya kuhudhuria kikao cha maandalizi, atatozwa faini ya shilingi 1,000,000/= na kufungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi kumi na mbili (12).

KANUNI YA 32
UDHIBITI WA VIONGOZI

1.  Kiongozi yeyote atakayefanya jambo lolote kati ya haya yafuatayo, ataadhibiwa kwa mujibu wa Kanuni hii:-

(a)      Akibainika kuwa anadai hongo au amepokea/ametoa hongo /au kuhusika na matendo yeyote yanayo ashiria hongo ikiwa ni pamoja na kushawishi waamuzi au wachezaji wa timu yake/timu pinzani kupokea/kutoa hongo atafungiwa miaka mitatu au maisha.

(b)     Akimshambulia Mwamuzi, mchezaji au kiongozi mwingine yoyote, kwa maneno au vitendo, kabla, wakati au baada ya mchezo atafungiwa kwa kipindi kisichozidi miezi sita.

(c)      Akifanya kitendo chochote kinachoashiria imani ya uchawi atafungiwa kwa kipindi cha miezi sita.

(d)     Akifanya kitendo chochote ambacho ni kinyume cha maadili ya taaluma ya uongozi wa mpira wa miguu kama vile kuhudhuria kikao cha maandalizi ya awali ya mchezo husika/au kusimamia shughuli za mchezo husika akiwa amelewa atafungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi kumi na miwili (12).

(e)      Akishindwa kutoa taarifa zinazohitajika TFF kwa mujibu wa maagizo husika atafungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi mitatu (3).

(f)       Akitoa taarifa isiyo sahihi kiasi cha kupotosha maamuzi ya TFF atafungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi kumi na miwili.

(g)      Akitoa matamshi au ishara za matusi dhidi ya mashabiki, akitoa matamshi, ishara za matusi yenye nia ya kumdhalilisha kiongozi mbele ya jamii awe wa TFF, KILABU au TAIFA atatozwa faini ya Sh. Milioni moja (1,000,000/=) na kufungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi mitatu (3).
(h)     Kiongozi au Kilabu itawajibika kufuata na kutii maamuzi au maagizo ya TFF. Kiongozi atakayeshindwa kutii maamuzi au maagizo hayo atafungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi mitatu (3) na kutozwa faini ya Sh. Milioni moja (1,000,000/=). Kilabu itashindwa kutekeleza maamuzi/maagizo husika itaondolewa kwenye mashindano na kushushwa Daraja.

(i)       Ni marufuku kwa kiongozi wa Kilabu kushutumu au kutoa matamshi yenye lengo la kumkashifu au kumdhalilisha kiongozi wa TFF/Chama cha Mpira cha ngazi husika kwenye vyombo vya habari. Kiongozi atakaye kwenda kinyume na kanuni hii atafungiwa kwa kipindi kati ya miezi sita (6) mpaka kumi na miwili (12) na faini ya shilingi miliono moja (1,000,000/=).

(j)       Kiongozi akibainika kuhudhuria kikao cha maandalizi ya mchezo kwa kujisingizia cheo kisicho kuwa chake atatozwa faini ya shilingi 500,000/= na kufungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi mitatu (3).

(k)     Uongozi ukibainika kugushi sahihi ya mchezaji au kufanya tendo lolote kwa lengo la kukamilisha zoezi la usajili kwa udanganyifu, kiongozi/viongozi husika wa klabu husika atafungiwa/watafungiwa kwa kipindi kisichopungua miaka mitano na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake/yao.

(l)       Kiongozi atakayebainika kusababisha timu kutofika uwanjani na kukosa mchezo, baada ya kuhudhuria kikao cha maandalizi, atatozwa faini ya shilingi 1,000,000/= na kufungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi kumi na mbili (12).

KANUNI YA 33
ADHABU KWA KLABU

(1)   Kilabu kina wajibu na jukumu la kuhakikisha kuwa wachezaji, viongozi, wanachama na wapenzi wake wanajiheshimu na hawajihusishi na vitendo vyovyote vya utovu wa nidhamu kama vile matusi, vitisho, vurugu, vitendo vinavyoashiria imani za kishirikina na vitendo vyovyote vingine visivyokuwa vya kimichezo kwenye viwanja vya michezo. Kilabu ambacho washabiki wake watafanya vitendo hivyo kitatozwa faini ya TShs. 500,000/=. Mshabiki atakayekamatwa akifanya vitendo hivyo atachukuliwa hatua za kisheria na atakayepatikana na hatia atafungiwa kuingia uwanjani kwa kipindi kisichopungua miezi 3 na kisichozidi miezi 12.

(2)   Kilabu kitapoteza mchezo ambao utavunjika kutokana na vurugu za washabiki wake.

(3)   Kilabu pia zitawajibika kulipa gharama za matibabu na kulipa gharama za mali zilizoharibika kwa waathirika wa vurugu za washabiki wake zitakazofanyika kabla, wakati au baada ya mchezo.

(4)   Kilabu zinatakiwa zihakikishe viongozi wa kilabu husika waliosimamishwa na TFF kwa sababu moja au nyingine kujishughulisha na uongozi wa klabu wanatii adhabu zao. Shirikisho litachukua hatua itakayoona inafaa ikiwemo kuisimamisha klabu kushiriki katika ligi iwapo klabu hiyo itaruhusu viongozi wake waliosimamishwa kujishughulisha na masuala ya uongozi ndani ya kipindi cha adhabu.

(5)   Kilabu kitakachoshindwa kuleta timu uwanjani baada ya kuhudhuria kikao cha maandalizi ya mchezo kitatozwa faini ya shilingi milioni tano (5,000,000/=) na kushushwa daraja na, kiongozi aliyeshiriki kutoleta timu uwanjani atafungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi kumi na mbili (12), kutojishirikisha na masuala yote ya mpira wa miguu na atatozwa faini ya shilingi milioni moja (1,000,000/=).

KANUNI YA 34
VIWANGO NA UTARATIBU WA ADHABU KWA WACHEZAJI

(1)      Kilabu chochote kinaweza kutoa adhabu yoyote inayostahili dhidi ya mchezaji wake yeyote.

(2)      Adhabu zote zitakazotolewa na vilabu ni lazima zithibitishwe na TFF kabla adhabu hiyo haijaanza kutekelezwa.

(3)      Kilabu hakitakuwa na mamlaka ya kumfungia mchezaji kwa kipindi kinachozidi msimu wa ligi husika au kwa mchezaji mwenye mkataba, zaidi ya kipindi cha mkataba wake na klabu.

(4)      Kilabu hakitakuwa na mamlaka ya kumfungia mchezaji yoyote nje ya nchi.

(5)      TFF, pamoja na kuthibitisha adhabu yoyote iliyotolewa na klabu, inaweza kufuta, kupunguza au kuongeza adhabu hiyo ikiwa ni pamoja na kumfungia mchezaji huyo nje ya Nchi.

(6)      Kabla Kilabu chochote hakijatoa adhabu yoyote ni lazima mchezaji anayehusika apewe nafasi ya kujitetea.

(7)      Kilabu chochote kitakachotoa adhabu kwa mchezaji wake na kutuma taarifa hiyo TFF ili adhabu hiyo ithibitishwe, kitalazimika kutuma TFF vielelezo vyote vinavyohusika ikiwa ni pamoja na Muhtasari wa Kikao kilichotoa adhabu hiyo.

(8)      Endapo mchezaji yeyote anaamini ameonewa kutokana na adhabu aliyopewa na kilabu chake na ikathibitishwa na TFF, anarushusiwa kukata rufaa, kupinga adhabu hiyo, kwa chombo husika.

SURA YA KUMI
HADHI USAJILI NA UHAMISHO WA WACHEZAJI

KANUNI YA 35
KIPINDI CHA USAJILI
(1)      Usajili wa wachezaji ni suala la kiufundi kama ilivyo kanuni ya 8 (3). Mwalimu Mkuu wa timu atawajibika kutambua wachezaji wanaotakiwa kusajiliwa.  Katibu Mkuu atafanya masuala ya utawala, atakamilisha zoezi la usajili wa wachezaji na kuwasilisha mikataba na fomu ya majina TFF kwa wakati.

(2)      Vilabu vinawajibika kutumia mikataba iliyotayarishwa na Shirikisho kuhamisha/kuazima na kusajili wachezaji wake, mikataba mingine yote haitatambulika.

(3)      Kutangaza wachezaji ambao kilabu inasitisha mikataba yao, uhamisho na usajili wa wachezaji utafanywa na walimu wa vilabu katika kipindi kitakachotangazwa na TFF.

(4)      Kutakuwa na vipindi vingine viwili vya usajili, kipindi cha kwanza kitakuwa baada ya kumalizika Ligi na kipindi cha pili kitakuwa katikati ya msimu wa Ligi Kuu.  Tarehe za usajili wa vipindi vyote viwili zitatangazwa na TFF. (kanuni Na 37 )


KANUNI YA 36
HADHI YA WACHEZAJI
WACHEZAJI WA RIDHAA NA WA KULIPWA

(1)   Wachezaji wanaoshiriki katika Soka rasmi ni wa ridhaa au wa  
        kulipwa.

(2)     Mchezaji wa kulipwa ni mchezaji mwenye mkataba wa maandishi na kilabu na analipwa zaidi ya gharama halisi anazoingia kutokana na shughuli zake za soka.  Wachezaji wengine wote wanahesabiwa kuwa ni wa Ridhaa.

KANUNI YA 37
KUPATA UPYA HADHI YA RIDHAA

1        Mchezaji aliyesajiliwa kama Mchezaji wa kulipwa hawezi kusajiliwa tena kama wa ridhaa mpaka zipite angalau siku 30 baada ya mechi ya mwisho aliyoecheza kama wa kulipwa.

2.       Hakuna fidia inayolipwa kwa kupata upya hadhi ya ridhaa.  Iwapo mchezaji anasajiliwa upya kama wa kulipwa katika kipindi cha miezi 30 ya kurudishiwa hadhi ya Ridhaa, Klabu yake mpya italipa fidia ya mafunzo kwa mujibu wa Ibara ya 20 ya kanuni ya FIFA.                                     

KANUNI YA 38
KUACHA SHUGHULI

1.       Wachezaji wa Kulipwa wanaomaliza muda wao wa mkataba na wachezaji wa Ridhaa wanaomaliza muda wao, watabaki kuwa wamesajiliwa katika Chama cha Mpira cha Nchi ambacho Klabu yao waliochezea mwisho kwa kipindi cha miezi 30.

2.       Kipindi hiki kinaanza siku ambayo mchezaji atachezea Klabu mara ya mwisho katika mechi Rasmi.

KANUNI YA 39
USAJILI

1.       Mchezaji lazima asajiliwe na Chama cha Soka ili kuchezea klabu kama mchezaji wa Kulipwa au wa Ridhaa kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 2 ya kanuni za FIFA.  Ni wale wachezaji waliosajiliwa tu ndio wanaostahili kushiriki katika Soka rasmi.  Kwa kujisajili, ina maana mchezaji anakubali kufuata Sheria na Kanuni za Shirikisho la Soka Duniani (FIFA).  Mashirikisho na Vyama vya Soka.

2.       Mchezaji anaweza kusajiliwa na kilabu moja tu kwa wakati huo.

3.       Wachezaji wanaweza kusajiliwa katika kilabu hadi tatu kwa kipindi cha tarehe 01 Julai hadi 30 Juni cha mwaka unaofuata.  Katika kipindi hicho, mchezaji anastahili kuchezea Mechi Rasmi katika kilabu mbili tu.
                     

KANUNI YA 40
VIPINDI VYA USAJILI

1.       Wachezaji wanaweza kusajili tu kati moja ya vipindi viwili vya Usajili vya mwaka vilivyopangwa na Chama cha Soka kinachohusika.  Jambo la pekee katika Sheria hii, mchezaji wa kulipwa ambaye Mkataba wake umekwisha kabla ya Kipindi cha Usajili anaweza kusajiliwa nje ya Kipindi cha Usajili.  Vyama vya Soka vinaruhusiwa kusajili wachezaji hao wa kulipwa alimradi tu uzingativu unaotolewa kwa kuaminika kimichezo kwa mashindano yanayohusika.  Iwapo kuna sababu za msingi za kuvunjika kwa mkataba, FIFA inaweza kuchukua hatua za muda ili kuepuka ukiukaji na kwa mujibu wa Ibara ya 22 ya kanuni za FIFA.

2.       Kipindi cha kwanza cha Usajili kitaanza baada ya kukamilika kwa msimu na kwa kawaida hukamilika kabla Msimu Mpya haujaanza.  Kipindi hiki hakizidi majuma kumi na mawili.  Kipindi cha Pili cha Usajili kwa kawaida kitatokea katikati ya Msimu na hakitazidi majuma manne.  Vipindi Viwili vya Usajili kwa Msimu vitaarifiwa FIFA angalau miezi 12 kabla ya kuanza kutumika.  FIFA itaamua tarehe kwa Chama chochote cha Soka kitakachoshindwa kuwasilisha kwa wakati.

3.       Wachezaji watasajiliwa tu itokeapo hali ya upekee kama ilivyotabiriwa na Ibara ya 6, aya ya 1 ya kanuni za uhamisho wa wachezaji za FIFA.  Iwapo maombi ya Kilabu yatawasilishwa kwa wakati kwa Chama kinachohusika wakati wa Kipindi cha Usajili.

4.       Masharti yanayohusu Vipindi vya Usajili hayatumiki kwa mashindano ambayo Wachezaji wa Ridhaa tu wanashiriki.  Kwa mashindano ya aina hiyo, Chama kinachohusika kitabainisha vipindi ambapo wachezaji watasajiliwa, alimradi uzingativu utawekwa kwa kuaminika kwa mashindano yanayohusika.

KANUNI YA 41
PASI YA WACHEZAJI

Chama kinachosajili kinawajibika kukipa Kilabu alikosajiliwa mchezaji pasi yenye taarifa za mchezaji husika, pasi ya Mchezaji itaonyesha kilabu alikosajiliwa tangu msimu wake wa miezi 12 ya kwanza.  Iwapo mwisho wa miezi 12 unaishia kati kati ya Msimu, mchezaji ataorodhesha katika pasi ya mchezaji kwa klabu aliyokuwa amesajiliwa katika Msimu uliomalizika katika miezi yake 12.

KANUNI YA 42
MAOMBI YA USAJILI
Maombi ya Usajili wa Mchezaji wa Kulipwa lazima yawasilishwe pamoja na fomu ya usajili ya mchezaji, nakala ya mkataba wa mchezaji, cheti cha utimamu wa afya, cheti cha kuzaliwa, historia ya uchezaji wake wa mpira wa miguu baada ya kutimiza miaka kumi na mbili (12) (player’s passport). Ni ridhaa ya chombo cha uamuzi kinachohusika kuzingatia marekebisho au nyongeza yoyote ya mikataba ambayo hayakuwasilishwa ipasavyo kwa chombo hicho.
KANUNI YA 43
HATI YA UHAMISHO YA KIMATAIFA

1.    Maombi ya ITC kwa wachezaji wa kigeni wa kulipwa yata wasilishwa kupitia mtandao wa kompyuta kwa kutumia programu ya “Transfer Matching System” (TMS) baada ya vilabu vinavyo husika na mchezaji huyo/hao kukubaliana nje ya mtandao.
2.     Maombi ya ITC kwa wachezaji wa kigeni wasio wa kulipwa yatawasilishwa kwa barua TFF baada ya vilabu vinavyo husika na mchezaji/wachezaji huyo/hao kukubaliana. Chama cha soka kinachotoa ITC kwa njia hii kitapeleka nakala FIFA.
3.     ITC haihitajiki kwa mchezaji mwenye umri wa chini ya miaka12  

KANUNI YA 44
KUAZIMWA KWA MKOPO WACHEZAJI WA KULIPWA

1.    Mchezaji wa kulipwa anaweza kuazimwa kwa mkopo kwa kilabu nyingine kwa msingi wa makubaliano ya maandishi kati yake na klabu zinazohusika.  Uazimwaji huo kwa mkopo utafuata sheria zilezile zinazotumika katika uhamisho wa wachezaji, yakiwemo masharti ya fidia ya mafunzo na utaratibu wa mshikamano.

2        Kufuatana na Ibara ya 5, aya ya 3, ya kanuni za FIFA kipindi cha chini cha kuazima kwa mkopo mchezaji kitakuwa muda kati ya Vipindi Viwili vya Usajili.

3.       Kilabu itakayompokea mchezaji kwa msingi wa kuazimwa kwa mkopo haina haki ya kumhamishia katika klabu nyingine bila ya idhini ya maandishi ya kilabu iliyomwachia mchezaji kwa mkopo na ya mchezaji anayehusika.

4.        Mchezaji anayeazimwa kwa mkopo hatoruhusiwa kwenda zaidi ya daraja la kwanza.

5.      Kilabu haitoruhusiwa kutoa au kupokea wachezaji zaidi ya watano (5) wa mkopo katika msimu  mmoja.

KANUNI YA 45
WACHEZAJI WASIOSAJILIWA

Iwapo mchezaji asiyesajiliwa na Chama cha Soka anacheza mechi rasmi yoyote ya Kilabu, mchezaji huyo atahesabiwa kucheza kinyume cha sheria.  Bila ya kuathiri hatua yoyote inayotakiwa kurekebisha athari inayosabishwa na kucheza huko, vikwazo vinaweza kuwekwa kwa mchezaji na/au kilabu.  Haki ya kuweka vikwazo hivyo kimsingi iko mikononi mwa Chama cha Soka husika au mtayarishaji wa Mashindano yanayohusika.
KANUNI YA 46
MASHARTI MAALUMU YANAYOHUSU MIKATABA KATI YA
WACHEZAJI WA KULIPWA NA KLABU

1.       Iwapo wakala anahusika katika mapatano ya mkataba, naye atatajwa katika Mkataba.

2.       Muda wa chini wa Mkataba utakuwa kuanzia tarehe ya kuanza kutumika hadi mwisho wa msimu, wakati ambapo muda wa juu wa Mkataba utakuwa miaka mitano.  Mikataba ya muda mwingine wowote itakubaliwa tu kama inalingana na Sheria za nchini.  Wachezaji chini ya umri wa miaka 18 haruhusiwi kuingia mkataba wa mchezaji wa kulipwa kwa kipindi kinachozidi miaka mitatu, sharti lolote linalotaja kipindi kirefu zaidi halitatambuliwa.

3.       Kilabu inayotarajia kuingia mkataba na mchezaji wa kulipwa haina budi kuiarifu klabu yake ya sasa kwa maandishi kabla ya kufanya makubaliano na mchezaji huyo wa kulipwa.  Mchezaji wa kulipwa atakuwa huru tu kuingia mkataba na klabu nyingine iwapo mkataba wake na Kilabu yake ya sasa umekwisha au utakwisha baada ya miezi sita.  Uvunjaji wowote wa sharti hili utastahili vikwazo vinavyofaa.

4.    Uhalali wa Mkataba hautahesabiwa mpaka kuwe na matokeo mazuri ya upimaji afya na kutolewa kwa kibali cha kufanya kazi.

5.    Iwapo mchezaji wa Kulipwa ataingia katika mkataba zaidi ya mmoja unaohusu kipindi kimoja masharti yaliyowekwa katika Sura ya IV ya kanuni za FIFA yatatumika.

KANUNI YA 47
USAJILI NA UHAMISHO WA WACHEZAJI

1.       ‘Electronic system’ ya usajili wa wachezaji kwa kutumia Licence+ itatolewa na TFF kabla ya kipindi cha kwanza cha usajili.

2.       Kutakuwa na leseni ya usajili wa mchezaji yenye nembo ya TFF na ‘Win Africa With Africa’ na namba maalum itakayotolewa na TFF, ambayo itakuwa na taarifa zote muhimu za mchezaji husika. (kanuni 38)

3.       Kila mchezaji ataonyesha leseni hiyo wakati wa mchezo.

4.       Mchezaji ana uhuru wa kujisajili na Kilabu kingine katika msimu mmoja iwapo kutakuwa na maelewano kati ya klabu chake na kile kinachotaka kumsajili.

5.       Kilabu kinawajibika kuingia mkataba na mchezaji wa kuichezea lakini mkataba huo ni lazima uthibitishwe na TFF. Ada ya kuthibitisha mkataba ni Sh. 50,000/=.

6.       Mchezaji ambaye ameingia mkataba wa zaidi ya msimu mmoja hatoruhusiwa kujisajili na klabu kingine kabla ya klabu yake mpya kuafikiana na klabu yake ya zamani. (kanuni na 44 (3)).

7.       Mchezaji anawajibika kusaini Mkataba na Kilabu ili aweze kuidhinishwa na TFF kuchezea kilabu yake, jina lake litaorodheshwa kwenye Fomu ya Majina (Kanuni ya 40).


KANUNI YA 48
UTHIBITISHO WA USAJILI

TFF itadhibitisha usajili wa timu zote mbili wakubwa na watoto kwa wakati mmoja, kilabu zinatakiwa kukamilisha na kuwasilisha kwa pamoja usajili wa timu zote mbili pamoja na majina na mikataba ya makocha wa timu za wakubwa na vijana katika kipindi cha usajili.

Mchezaji yeyote hataruhusiwa kuchezea kilabu chochote katika michezo ya Ligi hadi usajili wake umethibitishwa na TFF, TFF itatoa siku 14 kuwasilisha malalamiko au pingamizi kimaandishi juu ya usajili tangu kutangazwa majina ya wachezaji wanaombwa kusajiliwa na klabu husika, baada ya hapo uthibitisho utakaotolewa na TFF ndiyo utakuwa wa mwisho. TFF haitapokea rufaa yeyote inayohusu usajili kwa mchezaji ambaye hakuwekewa pingamizi mwanzoni isipokuwa iwapo klabu imefanya udanganyifu wa jina la mchezaji.

KANUNI YA 49
MAJINA YA WACHEZAJI

Mchezaji atalazimika kujaza majina yake kamili matatu katika fomu ya usajili

KANUNI YA 50
IDADI YA WACHEZAJI
Kila Kilabu kitaruhusiwa kusajili wachezaji wasiozidi thelathini (30) na wasiopungua kumi na wanane (18).

KANUNI YA 51
KLABU / WACHEZAJI WANAOSITISHA AU KUMALIZA MIKATABA

Kila Kilabu kitalazimika kuwasilisha TFF kwa maandishi, majina ya wachezaji watakaositisha mikataba yao/kuwa huru katika usajili wa msimu wa Ligi/dirisha dogo unaofuata katika muda wa Uhamisho utakaotangazwa na TFF na kitalazimika kumpa taarifa ya maandishi mchezaji/wachezaji husika.

KANUNI YA 52
WACHEZAJI WALIOPANDISHWA
1.       Kila Kilabu kitaruhusiwa kusajili wachezaji wa timu yake ya pili (B) ambao walithibitishwa na TFF katika msimu uliopita.

2.       Mchezaji yeyote wa timu ya pili ambaye hakusajiliwa na kuthibitishwa na TFF katika msimu uliopita hataruhusiwa kusajiliwa katika timu ya kwanza (A) kama mchezaji aliyepandishwa au huru.

KANUNI YA 53
WACHEZAJI HURU
1.       Mchezaji yeyote ambaye hakusajiliwa na klabu yoyote ya Daraja lolote katika msimu uliopita atakua huru, hahitaji uhamisho bali atalipiwa ada ya usajili TFF.

2.       Mchezaji yeyote ambaye kilabu yake imesitisha mkataba wake/au mkataba wake umemalizika, atakua mchezaji huru na hivyo hatalipiwa ada ya uhamisho isipokuwa ada ya usajili TFF.

Mchezaji aliyerudi nyumbani baada ya kumaliza mkataba wake nje anatakiwa kukamilisha taratibu za uhamisho wa Kimataifa na hatokuwa huru hadi atakapokamilisha uhamisho.
KANUNI YA 54
WACHEZAJI WA KUHAMISHWA

Mchezaji yoyote ambae hajamaliza Mkataba au Mkataba wake haujasitishwa na Kilabu yake, atakapojisajili na Kilabu kingine ni lazima ahamishwe kuanzia ngazi ya Kilabu, Wilaya, Mkoa na TFF.
KANUNI YA 55
WACHEZAJI KUTOKA NJE YA NCHI

Kilabu kinaruhusiwa kusajili wachezaji (wakigeni) wa ngazi ya kimataifa (wachezaji wa timu za taifa/Ligi Kuu) kutoka nje ya nchi wasiozidi wa tano (5). Wachezaji kutoka Ulaya na Marekani ya kusini wanaweza kuwa wa daraja la pili na kuendelea. Kilabu hicho kinaruhusiwa kuchezesha wachezaji wasiozidi watano (5) wa kigeni katika mchezo mmoja(walioorodheshwa). Wachezaji hao watasajiliwa baada ya TFF kuhakikisha usahihi wa taarifa zao na kukamilika kwa  taratibu za uhamisho wa kimataifa.
KANUNI YA 56
NGAZI ZA UTHIBITISHO WA USAJILI

Kamati sheria, maadili na hadhi za wachezaji itathibitisha usajili wa wachezaji wote wa wakubwa na vijana wa kilabu za ligi kuu.

KANUNI YA 57
KUTENGUA UTHIBITISHO WA USAJILI
Uthibitisho wa usajili wa wachezaji wa klabu za ligi kuu unaweza kutenguliwa na Kamati ya sheria, maadili na hadhi za wachezaji endapo itathibitika kuwa usajili huo umekiuka masharti ya Kanuni hizi.

KANUNI YA 58
KATAZO
Haitaruhusiwa kwa mchezaji yeyote kutia saini mikataba ya vilabu zaidi ya kimoja kwa wakati mmoja. Mchezaji atakayesaini mikataba ya timu mbili tofauti kwa wakati mmoja, ataadhibiwa kwa mujibu wa kanuni ya 44 (5).

KANUNI YA 59
UHAMISHO WA MCHEZAJI
Bila ya kuathiri kanuni za uhamisho na usajili wa wachezaji:-

1.       Kilabu kinaweza kumhamisha mchezaji kutoka kilabu kimoja hadi kingine, kwa madhumuni ya kumsajili, baada ya ligi kumalizika na/au katika kipindi cha usajili wa katikati ya msimu.  Kilabu kinachotaka kumsajili mchezaji aliyesajiliwa na kilabu kingine au mwenye mkataba na kilabu kingine, kitalazimika kuafikiana na kilabu chake kabla ya kumsajili mchezaji huyo. Hata hivyo kilabu ambacho kitaruhusiwa kusajili mchezaji katikati ya msimu ni kile tu ambacho hakijatimiza wachezaji 30 au kile ambacho kimempa mchezaji wake ITC ya kwenda kucheza soka nje ya nchi, au kile ambacho mchezaji wake amehamia kilabu kingine cha ndani kwa mujibu wa Kanuni hii.

2.       Endapo kiongozi wa Kilabu anachohama mchezaji amekataa au amekwepa kuidhinisha uhamisho wa mchezaji wa madaraja ya chini (ambaye hawajibiki kuwa na mkataba hivi sasa) ambaye anayetaka kukihama kilabu chake baada ya msimu wa Ligi kwisha; Katibu wa Chama cha Mpira ngazi ya Wilaya husika ataidhinisha uhamisho huo baada ya mchezaji aliyeomba kuhama kumthibitishia kwa maandishi kuwa amehamia Kilabu hicho kipya lakini Katibu wa Kilabu chake cha zamani hataki au anakwepa kuidhinisha uhamisho wake.

3.       Nakala za barua ya uthibitisho wa mchezaji wa daraja la chini (ambaye hawajibiki kuwa na mkataba hivi sasa) kwenda kwa Katibu wa Chama cha mpira ngazi ya  Wilaya husika ni lazima zitumwe pia kwa Katibu wa Chama cha mpira cha Mkoa husika na kwa Katibu Mkuu wa TFF.

4.       Pamoja na kupokea nakala ya barua ya uthibitisho kwa mujibu wa Aya ya (3) ya Kanuni hii, TFF  inaweza kumwita mchezaji huyo na kumhoji kuhusiana na uthibitisho alioutoa kwa Vyama vya mpira vya wilaya na mkoa  na uamuzi wa TFF utakuwa wa mwisho.

5.       Ada za uhamisho wa mchezaji mmoja kutoka Kilabu kimoja hadi kingine kwa madaraja mbalimbali na mgawanyo wake kwa mamlaka zinazohusika zitakuwa kama inavyoonekana kwenye jedwali la kwanza lililopo kwenye viambatanisho vya Kanuni hizi. Ada hizi ni kima cha chini cha ada za uhamisho wa wachezaji kutoka klabu moja kwenda nyingine lakini klabu yenye mkataba na mchezaji ina haki ya kudai malipo zaidi kwa ajili ya uhamisho toka kwa klabu kinachomtaka mchezaji wake. Ada za uhamisho kwa mamlaka zingine hata kwa wachezaji wenye mikataba zitabaki kama zilivyo.

KANUNI YA 60
UHAMISHO KWENDA TANZANIA ZANZIBAR

Pamoja na kufuata utaratibu mzima wa uhamisho wa mchezaji kama ulivyoainishwa katika Kanuni ya 56, ada za uhamisho wa wachezaji wa Tanzania Bara kwenda Tanzania Visiwani itakuwa ni itakuwa ni kwa mujibu wa makubaliano baina ya timu zinazohusika kulingana na masharti yaliyomo ndani ya mkataba wa mchezaji husika na kilabu chake.

SURA YA 11
ADHABU ZINAZOHUSIANA NA USAJILI NA UHAMISHO

KANUNI YA 61
ADHABU ZINAZOHUSU USAJILI NA UHAMISHO
1.       Mchezaji yeyote atakayebadili jina lake halisi kwa madhumuni ya kudanganya ili asajiliwe kinyume cha masharti ya Kanuni hizi atafungiwa kucheza mpira ndani na nje ya nchi kwa kipindi kisichopungua miezi kumi na miwili kuanzia tarehe ya kubainika.

2.       Kilabu iliyomchezesha mchezaji aliyebadili jina kwa nia ya kudanganya kitalipa faini ya TShs 1,000,000/= kwa kila mchezo ambao mchezaji huyo alicheza lakini matokeo ya uwanjani hayatobadilika.

3.       Kilabu kitakachothibitika kumchezesha mchezaji ambaye hajasajiliwa na klabu hiyo kitapoteza michezo husika, kitalipa faini ya shilingi milioni moja (1,000,000/=) na mchezaji husika atafungiwa kwa kwa kipindi kisichopunguwa miezi kumi na miwili (12) bila ya kujali kukatwa au kutokatwa rufaa.

4.       Leseni ya usajili ya mchezaji iliyochafuka, kufutwafutwa au kunjwa kiasi cha kupoteza uhalisia wake na kuleta mashaka hakitakubaliwa.

5.       Kilabu chochote kitakachowasilisha Usajili wake baada ya tarehe itakayotangazwa na TFF hautapokelewa na kitahesabika kuwa kimejiondoa chenyewe kwenye Ligi na kitashuka daraja.

6.       Kiongozi yeyote wa TFF atakayeweka saini inayotofautiana na saini yake halisi kwenye fomu/mkataba ya/wa usajili kwa madhumuni yoyote yale, atafungiwa kuongoza mchezo wa mpira kwa kipindi cha miaka mitano.

7.       Kiongozi yeyote wa FA au Kilabu atakayetoa taarifa za zisizo sahihi na kupotosha Kamati ya Utendaji ya FA ngazi husika katika maamuzi yake, kuhusiana na usajili, atakabiliwa na adhabu ya kufungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi sita.

8.       Kiongozi yeyote wa TFF au Kilabu atakayekataa au atakayekwepa bila sababu ya msingi, kusaini fomu/mkataba ya/wa Usajili kwa madhumuni ya uhamisho atakabiliwa na adhabu ya kufungiwa kwa kipindi kisichopungua miezi sita.

KANUNI YA 62
UHAMISHO NJE YA NCHI
1.       Mchezaji yeyote anaruhusiwa kuhamia Kilabu kingine nje ya Nchi baada ya kupata kibali cha Kimataifa (ITC).
2.       Kabla TFF haijatoa kibali, mchezaji  analazimika kupata idhini ya Kilabu chake cha hapa Nchini.
3.       Maombi ya kibali cha TFF na idhini yeyote itakayotolewa na Kilabu ni lazima vifanywe kwa maandishi.
4.       Kilabu kinachotaka kumhamisha mchezaji na kilabu kinachohusika na mchezaji huyo vitakubaliana kuhusu gharama za uhamisho.
5.       Endapo itatokea kutokubaliana kati ya pande hizo mbili kutokana na sababu yoyote ile TFF itaingilia kati na kutoa uamuzi kwa kuzingatia sheria na kanuni za TFF, CAF na FIFA.
6.       TFF itatambua kumalizika au kuvunjika kwa mkataba wa mchezaji na klabu yake ya nje baada ya kupata ITC kutoka kwa Chama cha Soka cha Nchi alipokuwa akicheza.
7.       Barua ya uthibitisho kutoka kwa Chama cha Soka cha nje ni lazima iwe na Nembo ya Chama husika, jina kamili, cheo na saini ya afisa mhusika katika Chama hicho.
Uhamisho wa kimataifa unaombwa na kutolewa kwa chama cha  cha mpira cha kitaifa pekee kwa niaba ya kilabu, na si kwa mchezaji au kiongozi wa kilabu.




SURA YA 12
MENGINEYO
KANUNI YA 63
MWALIMU WA TIMU

1.       Kila Kilabu kinapaswa kuajiri mwalimu wa timu mwenye ujuzi wa kutosha na anayetambuliwa na TAFCA, na mkataba wake kusajiliwa TFF.
2.       Mwalimu wa klabu ya Ligi kuu anatakiwa awe na Stashahada au cheti cha ngazi pevu ya ufundishaji.
3.       Mwalimu toka nje atathibitishwa kwanza na TFF kabla ya kuingia mkataba na kilabu na kupewa kibali cha kuishi na kufanya kazi nchini.
4.       Mwalimu atatakiwa kuwa na Leseni ya Daraja la A toka TFF kuweza kufundisha kilabu cha ligi kuu.
5.       Mwalimu wa timu ndiye mkuu wa shughuli zote za timu kuanzia usajili wa wachezaji, uandaaji wa timu, usimamiaji katika mashindano na kadhalika.
6.      Kilabu ambacho kitasitisha mkataba wa mwalimu wake wakati ligi inaendelea, kitatozwa faini ya T.sh 500,000/= kwa kila mchezo kitakachocheza bila mwalimu mwenye sifa kwa mujibu kanuni 61 (2) ndani ya kipindi cha mwezi mmoja. Baada ya mwezi mmoja klabu hiyo itapoteza sifa ya kuendelea na michezo ya ligi kuu.

KANUNI YA 64
DAKTARI WA TIMU

Kila Kilabu kinapaswa kuajiri daktari wa timu mwenye ujuzi wa kutosha na anayetambuliwa na TASMA na kuthibitishwa na TFF.

KANUNI YA 65
TIMU ZA PILI NA WATOTO

1.    Kila Kilabu kinatakiwa kusajili na kudumisha timu za pili au za watoto,kuzichezesha katika michezo ya utangulizi timu ikicheza nyumbani na kushiriki katika mashindano ya vijana yanayoandaliwa na TFF, ikiwa ni sharti la kushiriki Ligi na kwa manufaa ya kilabu na kwa maendeleo ya mchezo wa mpira wa miguu kwa ujumla.  Endapo Kilabu itashindwa kutimiza sharti hili atakabiliwa na adhabu zifuatazo;
i.             Faini ya shilingi laki tano itatozwa kwa klabu husika.
ii.           Ikikosa michezo mitatu mfululizo ya Ligi klabu husika itashushwa daraja.

iii.          Kila Kilabu kitaruhusiwa kusajili wachezaji wa timu za watoto/vijana wasiyopungua 18 na wasiyozidi 22 wenye umri usiyozidi miaka 20.

iv.          Kilabu zinatakiwa ziwe zimekamilisha usajili wa timu za watoto katika kipindi cha usajili.

v.            Wachezaji watano tu katika orodha ya wachezaji kumi na nane wa timu za vijana ndiyo watakao ruhusiwa kutumika katika mchezo mmoja Ligi Kuu.

vi.          Usajili na uhamisho wa timu za watoto utazingatia kanuni za Ligi Kuu.

vii.        Waraka maalumu utatolewa kuhusiana na usajili wa wachezaji wa timu za watoto ambao utasomeka pamoja na kanuni hizi.


KANUNI YA 66
ADHABU ZISIZOKATIWA RUFAA
1.    Adhabu zote kwa mujibu wa kanuni zifuatazo za ligi kuu hazitakatiwa rufaa katka ngazi yeyote ya mashindano. Kanuni hizo ni;
(a)  KANUNI: 8 (Utaratibu wa mchezo)
(b) KANUNI: 25 (Udhibiti wa wachezaji) isipokuwa 25. (g) na (h).
(c)  KANUNI: 26 (Udhibiti wa waamuzi) isipokuwa 26. (c)na (e).
(d) KANUNI: 27 (Udhibiti wa makamishina) isipokuwa 27. (c) na (e).
(e)  KANUNI: 28 (Udhibiti wa watathimini wa waamuzi) isipokuwa 28. (c) na (e).
(f)  KANUNI: 29 (Udhibiti wa waalimu) isipokuwa 29. (c),(e),(f) na (g)
(g)  KANUNI: 30 (Udhibiti wa viongozi) isipokuwa 30. (a),(d),(f),(g),(h),(i),(k) na (l).
(h) KANUNI: 31 (Adhabu kwa Vilabu).


KANUNI YA 67
UDHAMINI

TFF itajitahidi kutafuta mdhamini/wadhamini wa Ligi Kuu, kila Kilabu kitalazimika kuheshimu na kuzingatia kikamilifu masharti yote yanayotakiwa kutekelezwa na Kilabu chenyewe, timu yake, wachezaji wake au Viongozi wake.  Yaliyomo ndani ya Mkataba /Mikataba hiyo kama itakavyoelezwa na TFF. Timu itakayoshindwa kutekeleza masharti haya kama itakavyoelezwa na TFF itatozwa faini isiyopungua Tshs. 1,500,000/= na pia inaweza kuchukuliwa hatua nyingine ikiwemo kuondolewa kwenye mashindano na /au kufungiwa.

KANUNI YA 68
LESENI YA KUSHIRIKI LIGI KUU.
Vilabu vya ligi kuu vinatakiwa kuwasilisha maombi ya kupatiwa leseni TFF katika muda utakao tangazwa na Kamati ya Utendaji ya TFF.
1.    Ilikupewa leseni muombaji anatakiwa awe nasifa zifuatazo;
a.    Katiba ya klabu iliyosajiliwa,
b.    Watendaji wa klabu,
c.    Ofisi isiyo hamishika,
d.    Mpango wa maendeleao wa soka la vijana,
e.    Mwalimkuu wa timu aliye na shahada ya daraja B ya CAF
f.     Ripoti ya ukaguzi wa mahesabu ya klabu yake
g.    Uwanja wake wa mazoezi
2.    Kamati ya Sheria, maadili na Hadhi za wachezaji ya TFF ndiyo itakayo toa leseni ya kushiriki ligi kuu.
3.    Iwapo klabu haikuridhika na maamuzi ya kamati ya sheria, maadili na hadhi za wachezaji, klabu inatakiwa kuwasilisha rufaa yake ya kupinga maamuzi hayo kwenye kamati ya rufaa ya TFF katika kipindi kisichozidi siku tatu (3) za kazi baada ya kupokea uamuzi wa kamati ya sheria, maadili an hadhi za wachezaji.
4.    Ada ya kukataa rufaa ni shilingi milioni moja, Tsh. 1,000,000/=
5.    Maamuzi ya kamati ya rufaa juu ya suala la kutoa leseni kwa vilabu vinavyo shiriki ligi kuu ni ya mwisho.


KANUNI YA 69
UTUMIAJI WA MADAWA YA KUONGEZA NGUVU

Mchezaji yoyote atakayetakiwa kufanya vipimo vya dawa za kulevya au kuongeza nguvu, anawajibika kufanya hivyo, endapo atagundulika/atakataa kuwa anatumia madawa ya kulevya au kuongeza nguvu/kufanya hivyo atafungiwa kwa kipindi cha miezi kumi na mbili (12).


KANUNI YA 70
UFAFANUZI

Kwa minajili ya kufafanua Kanuni hizi TFF itakuwa inatoa WARAKA kila inapoonekana inafaaa kufanya hivyo kwa lengo la kuleta ufanisi katika utekelezaji wa Kanuni hizi.

KANUNI YA 71
TAFSIRI

Kikao cha juu kuliko vyote kwa ajili ya tafsiri ya Kanuni hizi kitakuwa kamati ya utendaji ya TFF na uamuzi wake utakuwa wa mwisho

KANUNI YA 72
MAREKEBISHO YA KANUNI

Kamati ya utendaji ya TFF inaweza kurekebisha Kanuni hizi kila inapotokea haja na sababu za kufanya hivyo.


KANUNI YA 73
KUFUTA KANUNI

Kanuni hizi zinaweza kufutwa na Kamati ya Utendaji ya TFF pekee.





KANUNI YA 74
MAMBO YASIYOMO KWENYE KANUNI HIZI

Mambo yote yasiyokuwemo kwenye Kanuni hizi yataamuliwa na Kamati ya Utendaji ya TFF kwa kuzingatia Kanuni za FIFA na CAF.

Kanuni hizi zimepitishwa kwa Azimio la Kamati ya Utendaji ya TFF iliyokutana tarehe 20 Julai 2009.



______________________                                      ___________________          
     L. C.  Tenga                                                                          A. Oseah
          RAIS                                                                       KATIBU MKUU   


____________________
TAREHE


NYONGEZA
JEDWALI LA KWANZA
(KANUNI YA 18 (5) A
FOMU YA MGAWANYO WA MAPATO
KANUNI YA 18 (1), (2), (3), (4) NA (5)


KIASI
JINA
SAHIHI
Toa VAT 18% ya makusanyo



Toa: Posho ya kujikimu, kwa waamuzi na kamisaa 70,000/=x5



Usafiri wa ndani kwa waamuzi wote shs. 20,000/= na kwa kamisaa shs. 20,000/=.



Posho ya mchezo kwa waamuzi wa tatu na kamisaa shs. 100,000/= kila mmoja na mwamuzi wa akiba shs. 50,000/=



Posho ya msimamizi wa kituo shs. 100,000/=



Gharama za tiketi



Baki ya pato



9% Gharama za mchezo: (Rejea fomu ya gharama za mchezo)



(Isizidi 5,000,000/=)



9% TFF (T)



4.5% FDF (T)



15% Uwanja



3.5% FA (M)



29.5% klabu ngeni



29.5% Klabu mwenyeji



JUMLA






JEDWALI LA PILI
(KANUNI YA 18 (B))

FOMU YA MGAWANYO WA GHARAMA ZA MCHEZO LIGI KUU YA VODACOM
KANUNI YA 19 (1), (2) NA (3)


KIASI
JINA
SAHIHI
Gharama za msimamizi wa kituo



(i)     Msimamizi mkazi atalipwa posho 100,000/= na nauli ya 
      ndani 20,000/=



(ii)  Msimamizi kutoka nje ya kituo atalipwa posho shs. 
      100,000/=, nauli ya ndani 20,000/= gharama za kula na
      kulala shs. 70,000/= na nauli kutoka kituo chake na
      kurudi



(iii) Malipo ya ulinzi, ball boys, huduma ya kwanza, vinywaji,
      wasimamizi, wauzaji na wachanaji tiketi.



(vi) Baki ya pato iwapo gharama za mchezo ni pungufu 9%



Klabu ngeni 25%



Klabu mwenyeji 25%



TFF 50%



JUMLA







ADA ZA USAJILI NA UHAMISHO WA WACHEZAJI

Ada za Uhamisho za Wachezaji Kutoka Daraja Lolote Kwenda Ligi Kuu Itakuwa Kama Ifuatavyo;

                                

KLABU
TFF
FA (M)
FA (W)
JUMLA

55,000.00     
25,000.00     
20,000.00      








MGAWANYO WA ADA ZA USAJILI NA UHAMISHO WA WACHEZAJI KUTOKA TANZANIA BARA KWENDA VISIWANI.



KLABU
TFF
FA (M)
FA (W)
JUMLA

300,000.00    
120,000.00     
80,000.00      





















No comments:

Post a Comment