KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, July 4, 2014

Blatter awapoza machungu walioumizwa na adhabu ya Suarez lakini pia adhabu yake yapunguzwa

 Rais wa shirikisho la soka duniani FIFA Joseph Sepp Blatter, amesema anaamini mshambuliaji kutoka nchini Uruguay, Luis Alberto Suarez Diaz atarejea katika kiwango chake cha kawaida licha ya kukabiliwa na adhabu kali ya kufungiwa kwa miezi baada ya kubainika alimng’ata kwa makusudi beki wa timu ya taifa ya Italia Giorgio Chiellini.

Blatter, amesema hayo kwa lengo la kupoza machungu ya baadhi ya mashabiki wa soka duniani ambao wameonyesha kupingana na adhabu iliyotolewa dhidi ya Luis Suarez, ambaye amefungiwa kwa muda wa miezi minne kutojihusisha na masuala ya mchezo wa soka pamoja na kutokucheza michezo tisa ya kimataifa.

Kiongozi huyo wa FIFA pia amepongeza kitendo cha mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 26, cha kutambua makosa yake na kufikia hatua ya kumuomba radhi Giorgio Chiellini.

Amesema Luis Suarez, ameonyesha uungwana mkubwa ambao haukutarajiwa kutoka kwake, hivyo bado anaamini hatua hiyo ya kuomba msamaha itamrejesha katika mustakabali mzuri wa kucheza soka lake mara atakapomaliza adhabu inayomkabili.


Wakati huo huo shirikisho la soka duniani FIFA, limelegeza adhabu ya mshambuliaji Luis Suarez, kwa kumruhusu kujumuika na wachezaji wenzake wa klabu ya Liverpool kwa ajili ya kufanya mazoezi ya kujiandaa kabla ya kurejea tena uwanjani mwanzoni mwa mwezi novemba mwaka huu.

FIFA wamechukua maamuzi ya kumruhusu Suarez kufanya mazoezi ya wachezaji wenzake wa Liverpool baada ya kuona upo umuhimu kwa mshambuliaji huyo, kupewa haki kufanya mazoezi kutokana na mchezo wa soka kuchukua sehemu kubwa ya maisha yake, hivyo kama atakuwa nje kwa muda wa miezi minne huenda kiwango chake kikaporomoka.

Wakati huo huo imeelezwa kwamba uongozi wa FC Barcelona umefikia makubaliano na viongozi wa klabu ya Liverpool, katika mazungumzo ya kutaka kumsajili mshambuliaji Luis Suarez.

Taarifa zilizotangazwa na kituo cha radio cha Cadena Ser zimeripoti kwamba viongozi wa FC Barcelona, wamekubali kutoa kiasi cha paund million 90 kama ada ya usajili wa mshambuliaji huyo ambae msimu uliopita aliibuka kinara katika upachikaji wa mabao nchini Uingereza.

Taarifa za kituo hicho ziliambatana na uthibitisho wa muwakilishi wa viongozi wa FC Barcelona, José Ramón de la Morena ambaye alikuwa safarini kurejea nchini Hispania kitokea jijini London nchini Uingereza ambapo kikao cha pande hizo mbili kilifanyika tangu mwanzoni mwa juma hili.

No comments:

Post a Comment