KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, July 26, 2014

Wakongwe wa Porto 2004 na wa Barcelona 2006 waenda sare ya bao 4-4 katika mchezo maalumu wa hafla ya kumuaga Deco de Souza



Vilabu viwili vilivyo wahi kuwa mabingwa wa klabu bingwa Ulaya kwa nyakati tofauti vimekutana katika mchezo maalumu wa kumuaga kiungo wa zamani wa vilabu hivyo Anderson Luís de Souza maarufu Deco mchezo ambao ulifanyika jana na kuhitimisha safari ya kiungo huyo mkubwa kabisa aliyewahi kutokea dunia katika karne 21 Deco ambaye rasmi ameachana na mchezo wa soka
Mchezo huo uliwaleta kwa pamoja nyota kama Lionel Messi, Eidur Gudjohnsen, Benni McCarthy na Paulo Ferreira, ulimalizikwa kwa pande hizo mbili ambazo Deco aliwahi kuzichezea kwa mafanikio kumalizika kwa sare ya bao 4-4, ambapo Samuel Eto'o alifunga mabao 2 Deco mwenyewe akifunga goli la 4 na la kusawazisha kwa upande wa Porto ambako alicheza kipindi cha Pili.
Deco alichezea vikosi vyote katika mchezo huo maalum ambapo aliuufanya kuwa mchezo wa kusisimua akifunga dakika ya 89 na kuufanya kuwa mpira wake wa mwisho kuugusa akiwa uwanjani kama mchezaji.


Pals: Samuel Eto'o and Deco greet each other during the pre match pleasantries at the Estadio de Dragao stadium in Porto ahead of the testimonial
Porto ilikuwa na wachezaji: Baia, Ferreira, Costa, Emanuel, Valente, Costinha, Maniche, Mendes, Deco (Jankauskas 46), Derlei, McCarthy.
Wafungaji: Derlei 3; McCarthy 15; Jankauskas 62; Deco 89.

Barcelona:
Jorquera, Oleguer, Belletti, Gerard, Sylvinho, Davids, Van Bommel, Van
Bronckhorst, Giuly (Deco 46), Ezquerro (Eto'0 46), Gudjohnsen (Messi
46).
Wafungaji: Eto'o 54, 68; Deco 57, Messi 81.

Anderson Luís de Souza Deco alizalwia Agosti 27 1977) ambapo mbali ya kuvichezea vilabu hivyo pia aliwahi kuwa mchezaji wa timu ya taifa ya Ureno na amemalizia soka take katika klabu ya Fluminence.

No comments:

Post a Comment