KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, July 4, 2014

Ronaldo de Lima hana imani na kikosi cha Brazil kutokana na viwango duni vya wachezaji

Nyota bora wa zamani wa dunia Ronaldo de Lima
Aliyekuwa mchezaji bora duniani Ronaldo Luís Nazário de Lima, ameikosoa timu ya taifa ya Brazil kwa kusema bado kuna wachezaji wanacheza chini ya kiwango, hali ambayo inamuogopesha katika kipindi hiki cha michezo ya hatua ya mtoano inayoendelea kwenye michuano ya kombe la dunia.

Ronaldo, ambaye alikuwa mchezaji bora duniani kwa vipindi vitatatu tofauti na hiyo ilikuwa ni mwaka 1996, 1997 pamoja na 2002 amesema mpaka sasa anaona kuna mapungufu makubwa katika safu ya ushambuliaji ambayo haijatumikiwa ipasavyo.

Amesema mshambuliaji wa FC Barcelona, Neymar da Silva Santos Júnior ndiye mchezaji pekee anayempa matumaini kutokana na mchezo mzuri anaoendelea kuuonyesha, lakini kwa washambuliaji wengine kama Jo na Fred bado kuna mashaka kwake.

Katika hatua nyingine de Lima, amesema ana imani kubwa na kocha mkuu wa timu ya taifa ya Brazil Luis Philipe Scolari atafanya mabadiliko kuelekea katika mchezo wa hii leo ambapo The Canarinho watakuwa wakicheza mchezo wa hatua ya robo fainali dhidi ya Colombia.

Mchezo mwingine wa hatua ya robo fainali ya kombe la dunia utakaochezwa hii leo ni kati ya timu ya taifa ya Ujerumani dhidi ya mabingwa wa soka wa dunia mwaka 1998 timu ya taifa ya Ufaransa.

No comments:

Post a Comment