KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, June 14, 2012

Redknapp aondoka Tottenham


Harry Redknapp ameamua kuondoka Tottenham, baada ya kuwafundisha vijana wa Spurs kwa muda wa miaka minne.
Redknapp ambaye alichukuliwa kama meneja ambaye angeliweza kuifundisha vyema timu ya taifa ya Uingereza  lakini aliikosa kazi hiyo ambayo chama cha soka cha Uingereza kiliamua kumpa nafasi Roy Hodgson.
Jumanne wiki hii Redknapp alikanusha uvumi kwamba tayari alikuwa amejiuzulu kutoka Tottenham.
Redknapp, mwenye umri wa miaka 65, amesema kuwa amesalia na mwaka mmoja katika mkataba wake na klabu hiyo ya White Hart Lane, na inasemekana huenda ikawa kulikuwa na hali ya kutoelewana kuhusiana na mkataba mpya, baada ya kushauriana na mwenyekiti wa klabu, Daniel Levy.
Meneja huyo wa zamani wa Bournemouth, West Ham, Portsmouth na Southampton, sasa ameachana na klabu hiyo ya mjini London.
Wakati Fabio Capello alipoiacha kazi ya meneja wa timu ya Uingereza Februari 8 , Spurs walikuwa katika nafasi ya tatu katika ligi kuu ya Premier.
Alikuwa ameiacha Arsenal, ambayo ilikuwa inaonekana dhaifu wakati huo, kwa pointi kumi.
Hatimaye waliachwa nyuma kwa pointi nne na Arsenal, na kukosa nafasi ya kufuzu kwa mechi za klabu bingwa barani Ulaya.
Redknapp alipoondoka Portsmouth mwaka 2008, alifanikiwa kuingoza Tottenham hadi katika mashindano ya klabu bingwa, kwa mara ya kwanza, waliposhiriki mwaka 2010.
Baada ya kumaliza ligi kuu katika nafasi ya nne msimu uliopita, Tottenham walishindwa kufuzu, kufuatia Chelsea kupata ushindi katika fainali ya klabu bingwa.
Redknapp alifikiriwa kwanza wakati meneja kutoka Italia, Fabio Capello alipojiuzulu mwezi Februari, lakini hatimaye Hodgson ndiye aliyechaguliwa.
Inasemekana Levy hakufurahishwa na namna Spurs walivyokamilisha msimu, na kupoteza nafasi nzuri, baada ya kuitangulia Arsenal kwa pointi kumi, na ambayo ilimaliza katika nafasi ya tatu.
Redknapp mara kwa mara alikanusha hali hiyo ya kudorora kwa timu yake ni kutokana na kuhusishwa na kibarua cha timu ya taifa.
Wiki iliyopita, aliitaka Spurs kupata suluhu juu ya hatma yake, na kusisitiza kwamba hali ya kutojua kitakachotokea ni jambo ambalo lingeliweza kuwaathiri wachezaji wa Tottenham.
 

No comments:

Post a Comment