KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, February 11, 2013

SIMBA KUREJEA DAR JUMATANO, TWALIBU HILALI AELEKEA ARUSHA KUONGEZEA NGUVU YA UFUNDI BABU LIEWIG.



 TIMU ya Simba inatarajia kurejea nchini Jumatano ijayo kutoka mjini Arusha ambako imeweka kambi ya kujiandaa na mechi dhidi ya Libolo ya Angola.
Mechi hiyo imepangwa kufanyika Jumapili ijayo (Februari 17) kuanzia saa kumi na nusu jioni. Uongozi unafanya utaratibu wa kuiwezesha timu kufanya mazoezi katika Uwanja wa Taifa walau mara moja kabla ya mechi hiyo ili kutoa nafasi kwa benchi la ufundi kutoa maelekezo mahususi kwa wachezaji kuhusiana na mechi hiyo.
Kocha na mchezaji wa zamani wa Simba, Talib Hilal, anaelekea Arusha leo ili kuongeza nguvu ya benchi la ufundi la Wekundu wa Msimbazi. Hii si mara ya kwanza kwa Talib kuongeza nguvu kwenye benchi la ufundi la Simba kwani alifanya hivyo pia miaka kumi iliyopita wakati klabu hiyo ilipocheza na Zamalek ya Misri na kufanikiwa kuitoa.
Talib Hilal hajaja kuchukua nafasi ya mtu yeyote kwenye benchi la ufundi. Amekuja kwa mapenzi yake kwa Simba na mara zote klabu inamkaribisha kwa vile uwezo wake kitaaluma, uzoefu wake na uwezo wake katika kuhamasisha unakubalika ndani ya klabu.
Simba SC inaomba washabiki na vyombo vya habari waisaidie klabu kwa kutotoa taarifa zenye kuashiria migogoro isiyokuwepo. Simba wanawakilisha heshima na hadhi ya Tanzania katika mashindano haya.
Unachoomba uongozi wa klabu ni uzalendo kwa taifa letu walau katika kipindi hiki ambapo kinachoangaliwa ni utaifa wetu. Uongozi unaomba wadau wake wa vyombo vya habari kuandika habari za kujenga umoja, mshikamano na uzalendo kwa Watanzania wote ili hatimaye Simba ifanye vizuri.

No comments:

Post a Comment