KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, July 6, 2012

ODHIAMBO WA AZAM APATA ITC

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) ya mchezaji George Odhiambo, raia wa Kenya aliyejiunga na klabu ya Azam.
George Odhiambo(blackaberry)
 
Hati hiyo imetolewa na Chama cha Mpira wa Miguu cha Denmark (DBU) ambapo Odhiambo alikuwa akicheza nchini humo kabla ya kutua Azam kwa ajili ya msimu wa 2012/2013.
 
Klabu nyingine zinazosajili wachezaji kutoka nje ya Tanzania zinatakiwa kuhakikisha zinakamilisha uhamisho wao (transfer) kabla ya Julai 30 mwaka huu ambayo ndiyo siku ya mwisho kufanya hivyo.
 
Kanuni ya 41 ya Ligi Kuu kuhusu ITC inasema: “(1) Maombi ya ITC kwa wachezaji wa kigeni wa kulipwa yatawasilishwa kupitia mtandao wa kompyuta kwa kutumia program ya ‘Transfer Matching System-TMS’ baada ya klabu zinazohusika na mchezaji huyo au wachezaji hao kukubaliana nje ya mtandao.
 
(2) Maombi ya ITC kwa wachezaji wa kigeni wasio wa kulipwa yatawasilishwa kwa barua TFF baada ya klabu zinazohusika na mchezaji huyo au wachezaji hao kukubaliana. Chama cha Soka kinachotoa ITC kwa njia hii kitapeleka nakala FIFA. (3) ITC haihitajiki kwa mchezaji mwenye umri chini ya miaka kumi na mbili (12).”
 
Tunapenda kuzikumbusha klabu kuwa kwa mujibu wa Kanuni ya 53 ya Ligi Kuu, wachezaji wa kigeni ni lazima wawe wanachezea timu ya Taifa au klabu za Ligi Kuu huko wanakotoka.
 
Kanuni hiyo inasema: “Klabu inaruhusiwa kusajili wachezaji wa kigeni wa ngazi ya kimataifa ambao ni wa timu za Taifa na Ligi Kuu kutoka nje ya nchi wasiozidi watano (5). Wachezaji kutoka Ulaya na Marekani ya Kusini wanweza kuwa wa daraja la pili na kuendelea, na klabu inaruhusiwa kuchezesha wachezaji walioorodheshwa wasiozidi watano (5) wa kigeni katika mchezo mmoja. Wachezaji hao watasajiliwa baada ya TFF kuhakikisha usahihi wa taarifa zao na kukamilika kwa taratibu za uhamisho wa kimataifa.”
 

No comments:

Post a Comment