KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, June 14, 2012

ALEX SONG AKUMBANA NA KADHIA YA MASHABIKI WENYE HASIRA



Mwasisi wa kandanda la Cameroon Roger Milla ametaka kuwepo na utulivu baada ya taarifa kuwa kiungo Alex Song alitupiwa maneno machafu na mashabiki wenye hasira nchini kwake.

Hali hiyo imekuja kufuatia Cameroon kuchapwa na Libya katika mchezo wa kuwania tiketi ya kucheza kombe la dunia 2014.
Milla amesema hayo alipokuwa akiongea na redio ya taifa.
Amewataka mashabiki kuwa nyuma ya timu yao kuelekea kwemye mchezo wa kampeni ya kusaka tiketi kucheza fainali ya mataifa ya Afrika dhidi ya Guinea Bissau mwishoni mwa juma hili.
Kumbuka Cameroon ilishinda katika mchezo wa kwanza kwa bao 1-0 mchezo ulipigwa mwezi February.
Soka la nchi hiyo limekuwa katika hali tete baada ya Milla kuvuliwa uongozi wa heshima katika shirikisho la soka la nchi hiyo kufuatia ukosoaji wake kwa wale wanao liongoza soka nchini humo.
Hata baada ya ya ushindi wa nyumbani dhidi ya DR Congo wa kampeni ya kufuzu kombe la dunia 2014 mashabiki wan chi hiyo walipandwa na hasira kiasi kutupa mawe katika basi la wachezaji wakisema ushindi huo ulikuwa wa bahati.
Wachezaji sasa hawapandi basi la timu ya taifa wakati wakisafiri nchini humo kwa tahadhari.
Taarifa za mwanzo ziliarifu kuwa Song alivamiwa na mashabiki katika viunga vya Kennedy Avenue mjini  Yaounde lakini mchezaji huyo alisema alichofanyiwa ni kuzungukwa na kutupiwa maneno ya jazba.

No comments:

Post a Comment