KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, January 11, 2013

UKURASA WA HABARI ZA MICHEZO ZA KIMATAIFA:Van Persie mchezaji bora wa mwezi disemba wa Premier League na Shakhtar yaizidi kete Chelsea yamsajili Taison wa Metalist..



Van Persie mchezaji bora wa mwezi disemba wa Premier League.

Mshambuliaji wa Manchester United Robin van Persie ametajwa kuwa mchezaji bora wa mwezi disemba wa ligi kuu ya nchini England ‘Premier League’.

Mdachi huyo amefunga mara tano katika michezo sita aliyoicheza timu ya mashetani wekundu katika cha mwezi huo ambapo ameiwezesha timu hiyo kutengenezwa mwanya wa alama saba ndani mwezi huo ambayo ulikuwa na ratiba ya michezo ya sikukuu za Chrismass na mwaka mpya.

Van Persie, ambaye kwasasa anaongoza katika chati ya ufungaji magoli akiwa na magoli 16 ametanabaisha kuwa anafurahia kupata tuzo hiyo ya mwezi kutoka kwa wadhamini Barclays.

Van Persie alijiunga na United akitokea Arsenal kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni 24 million katika uhamisho wa kipindi cha majira ya kiangazi na tangu wakati amekuwa kicheza katika michuano yote na ameshatia kambani jumla ya magoli 20.

 Shakhtar yaizidi kete Chelsea yamsajili Taison wa Metalist.
 Shakhtar Donetsk imethibtisha kumsajili Taison toka klabu ya Metalist Kharkiv kwa ada ya euro milioni 15 ambapo mchezaji huyo raia wa Brazilian amenguka saini ya mkataba wa miaka mitano.

Taarifa ya klabu hiyo imesema

"Januari 10, Rais wa Shakhtar na Metalist walikuwa na mazungumzo juu ya uhamisho wa Taison kutoka mji wa Kharkiv kuelekea mji mwingine wa Donetsk, Shakhtar imelipa dolari za kimarekani milioni 20 na kwamba tumepata mchezaji ambaye alikuwa anataka kujiunga nasi tumempa mkataba wa miaka 5 "

Mshambuliaji huyo alijiunga na Metalist akitokea Internacional mwaka 2010, na ameitumikia klabu hiyo kwa michezo 57 ambapo alifunga jumla ya magoli 13 goals.

No comments:

Post a Comment