KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, January 25, 2013

UNITED HUENDA WAKAPATA NAFUU KUFUATIA IKER CASILLAS KUPATWA NA MAJERAHA MAKUBWA YA MKONO WA KUSHOTO

Iker Casillas
Pigo: Iker Casillas akiugulia maumivu ya mkono ambayo huenda yakamuweka nje dhidi ya Manchester United mwezi ujao.
 Iker Casillas yuko katika mashaka makubwa ya kuwepo katika kikosi cha Real Madrid kitakachoshuka dimbani dhidi ya Manchester United mchezo wa ligi ya vilabu bingwa Ulaya kufuatia taarifa awali kusema kuwa mlinda mlango huyo wa kimataifa wa Hispania kuvunjika mkono.

Casillas amepatwa nadhahma hiyo katika mchezo wa robo fainali dhidi ya Valencia mchezo wa kombe la mfalme 'Copa del Rey' uliopigwa jumatana ya kusukumwa na mchezaji mwenzake Alvaro Arbeloa katika harakati za kuokoa mpira katika eneo la hatari.
Madrid inatarajia kutoa maelezo ya ukubwa wa maumivu ya mlinda mlango huyo na aina ya tiba wakati ambapo Adan Garrido akiwa katika hali ya maandalizi kuziba pengo la mlinda malango huyo mzoefu namba moja wa Hispania.
Iker Casillas
Casillas pia atakosekana katika mchezo wa ligi ya La liga kesho kutwa jumapili dhidi ya Getafe na mchezo wa marudiano wa Copa Del Rey dhidi ya Valencia wiki ijayo.
Pia atakuwa katika vita ya kupigania kurejesha hali yake ya mkono katika kawaida ili kuwemo katika kikosi kitakachokuwa dimbani Februari 13 dhidi ya United katika dimba la Santiago Bernabeu.
Taarifa ya klabu yake imesema baada ya kufanyiwa uangalizi wa awali kupitia kipimo cha 'x-rays' imethibitika kuwa Iker Casillas amepata mpasuko mdogo katika mfupa unaotambuliaka kama metacarpal katika mkono wake wa kushoto.
'hiyo italazimu apate uangalizi mwingine kutoka mtaalamu zaidi leo (yaani jana jioni) na kuamua aina gani ya tiba afanyiwe'
Real Madrid's goalkeeper Iker Casillas
Real Madrid's goalkeeper Iker Casillas
Vita? Casillas na meneja wake Jose Mourinho walikuwa katika vita katika siku za hivi karibuni.
 
Hata hivyo maumivu makubwa kwa mlinda mlango huyo yanakuja katika kipindi nyeti cha kusubiri wiki mbili cha kampeni kubwa ya michuano mikubwa ya vilabu barani ulaya.

 Casillas amerejeshwa katika kikosi cha kwanza baada ya mzozo mkubwa mkubwa baina yake yeye na Mourinho ulioibuka kipindi cha majira ya baridi ambapo Mourinho aliamua kumuweka benchi bila sababu ya kueleweka.

Maamuzi ya Mourinho yaliibua hasira kutoka kwa mashabiki wa klabu hiyo na kutiwa utambi na vyombo vya habari.
Main man: Casillas' injury will be a blow to the Spanish champions ahead of the Champions League last 16

No comments:

Post a Comment