KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, April 2, 2013

Gary Cahill na Ashley Cole kusubiri wiki mbili kufuatia maumivu.Bayern Munich wanasema licha ya Juventus kuwa wagumu lakini mwendo mdundo NA Vilanova anajipanga kurejea kibaruani hii leo dhidi ya PSG..



Bosi wa Chelsea Rafael Benitez amethibtisha kuwakosa Cahill na Ashley Cole ambao wanasumbuliwa kuelekea kwenye michezo ijayo.
 Cole aliumia hii leo wakati akimkimbiza Danny Wellbeck na kutolewa nje ya uwanja katika mchezo wa kwanza wa michuano ya FA dhidi ya Manchester United mchezo ambao Chelsea iliibuka na ushindi wa goli 1-0.
Kwa upande wake Cahill, ambaye aliondolewa katika kikosi cha England kilichokuwa katika kampeni ya kufuzu kombe  la dunia lakini vilevile hakuwepo katika kikosi cha Chelsea kilichochapwa bao 2-1 na Southampton.

Alipoulizwa kuhusina na hali ya Cole, Benitez amesema
"aina hii yamaumivu ina maana atakosekana si chini ya wiki mbili, inaweza kuwa hata michezo au kitu kama hicho''
Cahill inawezekana akakosekana kwa siku 15.

Hiyo ina maanisha kuwa Cahill na Cole watakosekana kwa michezo yote ya robo fainali ya Europa League dhidi ya Rubin Kazan pamoja na mchezo wa nyumbani wa ligi dhidi ya Sunderland.
Wote kuna wasiwasi wa kutokuwepo katika nusu fainali ya FA dhidi ya Manchester City April 14.

Bayern Munich wanasema licha ya Juventus kuwa wagumu lakini mwendo mdundo.
Wachezaji wa Bayern Munich na maafisa wa klabu hiyo wamesema ushindi wa kishindo wa mabao 9-2 katika ligi kuu ya soka nchini Ujerumani Bundesliga dhidi ya Hamburg kamwe hauwafanyi kubweteka hata kidogo na kwamba hiyo ni nguvu ambayo itaelekezwa katika mchezo Juventus hapo kesho.
Bayern inaongoza ligi kuu ya soka nchini humo ikiwa mbele kwa alama 20 dhidi ya Borussia Dortmund na inaelekea kushinda taji la Bundesliga ikiwa itashinda dhidi ya Eintracht Frankfurt wiki ijayo lakini Jupp Heynckes anafikira zaidi Champions League.
"hatuutazami sana mchezo huo tulipata ushindi mkubwa kwakuwa tunakabiliwa na mchezo mgumu Jumanne"

Winga wa klabu Thomas Muller, ambaye alikuwa benchi kabla ya kuingizwa kunako dakika ya 64 anaamini kuwa mchezo dhidi ya Juve utakuwa mgumu "
Amesema kuwa Juventus wanategemea zaidi umoja na na kucheza kitimu zaidi na kwamba ukikutana na timu inayocheza mchezo kwa njia hiyo mchezo huwa mgumu na kwamba inabidi wasahau ushindi wa huo wa 9-2."
Mario Mandzukic pia alipumzishwa na Heynckes alimuanzisha nyota wa kimataifa wa Peru Claudio Pizarro, ambaye alilipa fadhila kwa kufunga magoli manne katika mchezo wa ushindi wa magoli 9-2.
Kiungo Bastian Schweinsteiger, ambaye alistua maumivu ya kifungo cha mguu wake katika dakika za mwisho za mchezo dhidi ya Hamburg anatarajiwa kuwa fiti na kuwepo dimbani katika mchezo dhidi ya Juve.


Vilanova anajipanga kurejea kibaruani hii leo dhidi ya  PSG.
Tito Vilanova sasa anajipanga kurejea katika benchi la klabu yake ya Barcelona ‘blaugrana’ kwa mara ya kwanza tangu mwezi Januari huku Xavi Hernandez na Jodi Alba wakielekea kurejea katika uimara wao kiafya baada ya kusumbuliwa na misuli.

Katika safari yao asubuhi ya jana Messi, aliwaambia mashabiki kupitia mtandao wake wa Tencent Weibo kuwa yeye na kikosi kizima cha klabu hiyo wamejipanga kukabiliana na kikosi cha mmiliki raia wa Qatari ambao wanaongoza ligi Ligue PSG.
Amsema mchezo utakuwa mgumu lakini wanajisikia safi kiushindani.

Kauli ya Messi kupitia mtandao wa kijamii ni majibu ya wasiwasi uliotokana na sare ya mabao 2-2 dhidi ya Celta Vigo mchezo ambao Messi alifunga goli katika michezo 19 aliyofunga mfululizo katika ligi kuu ya nchini Hispania La Liga.

Katika mchezo huo wa Jumamosi huko Balaidos kiwango cha mshambuliaji Cristian Tello kilikuwa juu ambapo alifunga goli la kwanza la Barca na kutengeza bao la pili lililofungwa na Messi.

Wakati  Vilanova akiendelea kubembeleza hali ya afya yake kurejea vema baada ya miezi miwili ya kuendelea na matibabu jijini New York, msaidizi wake Jordi Roura alitarajiwa jioni ya jana kufanya mkutano na waandishi wa habari kabla ya mazoezi huko Parc des Princes.
Mazoezi ya jana ya Barca yalitumika kumsaidia kocha kuunda kikosi cha kwanza kwa ajili ya mchezo wa leo Jumanne.
Huenda Xavi akirejea katika kiungo na Cesc Fabregas na Thiago Alcantara wanaendelea kusalia katika benchi sambamba na Gerard Deulofeu.

David Villa huenda akaanza akiwa na Messi na Tello au Alexis Sanchez, ambaye hakuwa vizuri katika mchezo dhidi ya Celta Virgo na kutolewa kipindi cha pili.
Jumla ya mashabiki 2,300 wa blaugrana wanatazamiwa kushuhudia mchezo huo huko Parc des Princes wakijumuika na takribani wakurugenzi 20  wa Catalans.

No comments:

Post a Comment