KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, May 21, 2013

KOCHA WA ZAMANI WA YANGA AENDELEA KUPATA ULAJI AFRIKA MASHARIKI NA KATI.


Uganda imemteua  Sredojevic 'Micho' Milutin kuwa kocha wa timu ya taifa.

Kocha huyo mwenye umri wa miaka  43 anakwenda kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Bobby Williamson ambaye aliondolewa kazini mwezi April ambapo Micho amesaini mkataba wa miaka miwili kuifundisha timu ya taifa ya Uganda ‘The Cranes’.

Micho, ambaye alifukuzwa kazi nchini Rwanda mwezi uliopita amesema amefurahishwa na kurejea nchini humo ambako ndiko alikoaanzia kufundisha soka barani Afrika.
Amenukuliwa akisema.

"Ndoto yangu ilianzia 2001 nchini Uganda nilipokuwa na SC Villa ambapo niliitumiaka kwa miaka mitatu pale. Kwa miaka tisa iliyopita nilikuwa nikifundisha soka nchini Ethiopia, Sudan, South Africa, Tanzania na Rwanda. Sasa nimerejea katika nyumba yangu ya soka.

"Nimefurahia na nitafanya kila niwezalo kufikia malengo ya kuboresha timu.

Rais wa chama cha soka nchini Uganda , Lawrence Mulindwa, amesema jumla ya watu 37 waliomba kazi hiyo na kwamba wanamuhakikishia  Micho kwamba watampa ushirikiano.

Wasaidizi wa zamani wa Cranes Sam Timbe na Kefa Kisala pia wametajwa kumsaidia Micho's assistant coaches, huku Fred Kajoba akisalia katika nafasi ya kocha wa makipa.

Sredojevic alianza kuifundisha Rwanda mwezi November 2011, alipochukua nafasi ya Sellas Tetteh wa Ghana.
Mafanikio makubwa akiwa na Amavubi ni pale alipomaliza katika nafasi ya pili katika michuano ya Cecafa Senior Challenge mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment