KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, January 8, 2013

JINAMIZI LA TAIFA STARS LAENDELEA KUITAFUNA TIMU YA TAIFA YA ZAMBIA CHIPOLOPOLO.

Mshambiliaji Mrisho Ngasa akijiandaa kupiga mpira uliozaa goli dhidi ya Zambia mwezi Disemba uwanja wa Taifa.
Mabingwa wa soka barani Afrika Zambia wamejikuta wakiendelea kuadhibiwa katika mchezo wa tatu mfululizo wa kirafiki ikiwa ni katika muendelezo wake wa kupasha moto misuli kuelekea katika fainali za mataifa ya Afrika AFCON 2013.
Mara hii jumapili wakiwa katika dimba la Dobsonville jijini Johannesburg Chipolopolo walizamishwa tena timu ya taifa ya Angola Palancas Negras kwa mabao 2-0.
Mshambuliaji anayechezea soka katika klabu ya Parana inayoshiriki ligi daraja la pili Geraldo,alianza kufunga goli la kwanza kunako dakika ya 8 na mlinzi Amaro anayechezea Primeiro Agosto ya Angola akifunga goli la pili zikiwa zimesalia dakika 5 mchezo kumalizika.
Zambia ambao ndio watetezi wa taji wataanza fainali za mataifa ya Afrika January 21 dhidi ya Ethiopia katika mji wa kaskazini mashariki nchini Afrika Kusini wa Nelspruit.

Kabla ya mchezo wao wa juzi dhidi ya Angola, mabingwa hao watetezi walianzia michezo yao ya kujipima nguvu nchini Saudi Arabia ambako walifungwa kabla ya kukanyaga ardhi ya Tanzania na kupata kichapo kingine kutoka kwa timu ya taifa ya Tanzania(Taifa Stars) mwezi uliopita.

Katika mchezo huo Herve Renard aliwatumia wachezaji 22 ambapo kipindi cha kwanza aliwatumia 11 kabla ya kubadilisha wote kipindi cha pili kwa lengo la kujaribu wachezaji wake 23 kabla ya fainali za mataifa ya Afrika kuaanza katika kipindi cha wiki mbili zijazo.

Kipindi cha kwanza aliwatumia mlinda mlango Kalililo Kakonje , Davies Nkausu, Stoppila Sunzu, Hichani Himoonde, Joseph Musonda, Mukuka Mulenga, Shadreck Malambo, Isaac Chansa, Rainford Kalaba, Collins Mbesuma na Chris Katongo.

Kipindi cha pili aliwaingiza Kennedy Mweene GK, William Njobvu, Salulani Phiri, Francis Kasonde, Emmanuel Mbola, Nathan Sinkala, Noah Chivuta, Chisamba Lungu, Felix Katongo, James Chmanga na Jonas Sakuwaha.


Hata hivyo matokeo hayo mabaya ya michezo ya kujipima nguvu hayamsumbui kocha mfaransa mwenye umri wa miaka 44 Herve Renard kwa kuwa Zambia pia ilikuwa na matokeo mabaya ya michezo ya kujipima nguvu katika fainali zilizopita kabla ya kushinda taji mbele ya waliokuwa wanapewa nafasi kubwa tembo wa Ivorycoast.
Kumbuka katika jumla ya michezo mitatu waliyocheza hawajafunga goli hata moja kutokana na uwezo mdogo wa washambuliaji walioko kambini hivi sasa huku washambuliaji tegemeo Jacob Mulenga wa FC Utrecht ya Udachi na Emmanul Mayuka wa Southamptom ya England wakitarajiwa kuwasili hii leo. 

Chipolopolo bado ina michezo kadhaa ya kirafiki katika programu yao ambapo inataraji kucheza dhidi ya Morocco, Norway na Namibia kabla ya kulivaa kundi C la michuano ya AFCON 2013 ambalo lina timu za Ethiopia, Nigeria na Burkina Faso.

Hebu tuangalie mchezo wa kesho dhidi ya Morocco wakiwa na wakali hao tuone kama mambo yanaweza kubalidilika.

Angola ambao wako katika kundi A pamoja na wenyeji Afrika Kusini, Morocco na Cape Verde Islands, ikiwa chini ya kocha raia wa Uruguay Gustavo Ferrin kwao huo ulikuwa ni ushindi wa tatu katika mfululizo wa michezo yao ya kujipima nguvu baada ya kutangulia kuzichapa Rwanda na Cameroon.

 Akitoa salamu zake za mwaka mpya kwa watu wa Zambia Rais wa chama cha soka cha Zambia FAZ mbaye aliwahi kuwa mchezaji bora wa Afrika mwaka 1988 ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya utendaji ya shirikisho la soka Afrika Kalusha Bwalya alisema maneno ambayo ni katika kipindi cha siku tano kipindi kifupi tu kabisa tayari watu wa Zambia wameanza kukata tamaa.
 
Katika salamu hizo alisema,
"New Year will be excellent as Chipolopolo attempt to defend her Nations’ Cup crown as well as secure an unprecedented place at the Fifa World Cup finals".

“The Nations Cup finals will be tough but we are toughened and we shall be ready,”

“We also have Fifa World Cup qualifiers to complete. The dream of every Zambian is one day to see our own lads at the finals. It's a long and difficult road which we shall tackle one match at a time and by the turn of the year, we can all hopefully dream of trekking across the Atlantic to Brazil,” 

Kwa heshima ya Kalusha Bwalya nchini Zambia kama ilivyo kwa Leodigar Chila Tenga wa Tanzania, hayo ni maneno mazuri lakini kama yatakwenda na vitendo ambavyo moja kwa moja na matokeo ya uwanjani haijalishi ni mchezo wa kirafiki au wa kimashindano kikubwa ni matokeo yakupendeza kwa wadau wasoka ndani ya Zambia na nje ya mipaka ya Zambia.
  
Ukisoma maoni yao Zambia wenyewe waliotuma kupitia mtandao wa chaka cha soka cha Zambia utapata picha tofauti kwani wapo wanao ona kwamba timu yao itatetea taji lakini kuna wengine wameshakata tamaa.


  NA HAYO HAPO CHINI NI MAONI YA WAZAMBIA WENYEWE KUPITIA MTANDAO WA CHAMA CHA SOKA CHA ZAMBIA JUU YA MWENENDO WA TIMU YAO KABLA YA AFCON KUANZA.


  • Orleans Ngoyi Kaunda · ZCAS
    tell them to get serious before we lose our tempers.

  • Philip Wilson

    Guys lets not worry much about the results of these friendly games. In as much as we all want to see our team win, I think I for 1 I would rather see them loose these friendlies because that will give the technical bench a good and clear picture of where we are lucking before the tournament start. Am sure if they do so and work on those weaknesses, we will be a force to recon with at the tournament. If we win these friendlies I can assure you that we will grow big headed and think we have all done. If there is 1 game I would want us to win of all the lined up games is that for Norway. Not that its a European team but because it will be at home and they guys will be biding farewell to that nation so its better they go win a win. Objective soccer fan.

    • Chewe Mwansa · Dee jay at Darkchild entertaiment dj
      Wilson but they didn't play well.am worried.I was at the stadium.anyway am watching them tommoroa as they play morocco.

    • Henry Sten MK · Solusi University
      you right. I am of the same view. Looking at the team they used, they were trying to avoid Injuries in this time that is so much reduced. My worry is Ethiopia, Those guys scored 5goals against Sudan-which not even Ivory Coast can manage. The policy is avoid injuries and fool the opponent. I know everyone wants us,but the current result works on two sides: First, it shows that there is still a lot of work to be done within the team and second the enemies, Especially Ethiopia and Nigeria will take Zambia as an average team.
      Ayew has been rule out of the AFCON and we want to avoid that bacause we have very few players.
      with Chisamba, Mayuka and Jacob, the volume of the team is increasing.
      Go boys and swallow them up all!

  • Nchi Munya · Training Officer at Ministry of Agriculture
    Great that rainford is getting some game time. Can't wait for the games to begin Im sure we will be a force in the tournament

  • Evans Mulenga · Assistant Internal Auditor at Workers' Compensation Fund Control Board
    I HOPE THIS IS NOT A TRUE REFLECTION OF THE CALIBER OF OUR SOCCER SQUAD THAT IS GOING TO DEFEND THE CUP.

No comments:

Post a Comment