KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, March 30, 2013

MURRAY AFIKA FAINALI YA SONY OPEN SASA KUCHEZA DAVID FERRER FAINALI.

 Andy Murray of Great Britain serves against Richard Gasquet of France
Nyota namba moja katika mchezo wa tenisi nchini Uingereza Andy Murray amefanikiwa kushinda pambano lake dhidi ya Richard Gasquet na kupata ushindi wa seti 6-7 (3/7), 6-1, 6-2, na kufanikiwa kuingia fainali ya michuano ya Sony Open ambapo atapambana na David Ferrer.
 
Gasquet ambaye ni namba nane kwa ubora alianza mchezo huo vema na kutawala katika seti ya kwanza ambalo alifanikiwa kupata tie-break, lakini hata hivyo Murray alirejea na kuchukua hatamu ya mchezo katika seti ya pili na ya tatu ya pambano ambalo lilikuwa zuri na la kupendeza la nusu fainali.
 
Wiki ijayo Murray atakuwa akipambana na Ferrer ambaye alimchapa mkongwe kutoka nchini Ujerumani Tommy Haas katika nusu fainali ya kwanza.

Endapo Murray atafanikiwa kushinda pambano hilo basi litampandisha juu kiubora zaidi ya mpinzani wake mkubwaRoger Federer.
Net gains: Andy Murray can still achieve world No 2 status after beating Richard Gasquet
Net gains: Andy Murray can still achieve world No 2 status after beating Richard Gasquet


No comments:

Post a Comment