Andre
Villas-Boas ametupilia mbali hoja juu ya madai kuwa Tottenham itarudia yale
iliyofanya msimu uliopita kwa kushindwa kufuzu ligi ya mabingwa ulaya.
Spurs walipanda
katika msimamo wa ligi msimu uliopita wa Premier League mpaka ilipopata kichapo
mwezi februari mchezo wa north London faida waliyokuwa nayo ya alama 10 juu ya Arsenal
kutoweka baada ya kushuka mpaka nafasi ya nne .
Kwakuwa Chelsea
walikuwa ni mabingwa wa Ulaya ubingwa walioupata mwezi May hiyo ilipelekea
vijana hao wa London ya Kaskazini kukosa nafasi ya kushiriki ligi ya Ulaya.
Hata hivyo
licha ya kupokea kichapo kutoka kwa Fulham March 17 , bosi wa Spurs Villas-Boas
hana mashaka na matokeo hayo kwakuwa timu yake haiku katika mbaya za katikati
kiasi kumkatisha tamaa.
Moyes apewa fungu la kuibadilisha Everton na sasa kuongeza mkataba.
David
Moyes amethibitisha kuwa atakuwa ni mwenye furaha kwa kuongeza mkataba wake wa
kusalia Goodison Park, ambapo amesema bodi ya klabu hiyo imempatia fedha
kuipeleka Everton katika kiwango kingine.
Meneja huyo
wa zamani wa Preston amekuwa na klabu hiyo wa miaka 11 ambapo mkataba wake wa
sasa unatarajia kumalizika majira ya kiangazi na Chelsea inaarifiwa kuwa wana mnyemelea bosi huyo.
Amenukuliwa
akisema,
"Nataka
Everton kuwa bora kama watu wanavyosema".
No comments:
Post a Comment