Didier Drogba akiwa amezungukwa na wapiga picha baada ya kuwasili Istanbul hii leo. |
Didier Drogba amepata mapokezi makubwa alipowasili katika jiji la Istanbul baada ya kukubaliwa kujiunga na Galatasaray ya Uturuki katika uhamisho wa dirisha la usaliji la mwezi January.
Kama ilivyopata mapokezi ya aina hiyo kiungo wa zamani wa Inter Milan Wesley Sneijder aliwasili Uturuki mwezi, naye Drogba ameonyesha kufurahishwa kufurahishwa na kujiunga na klabu hiyo ya udachi baada ya kuondoka katika klabu ya uchina ya Shanghai
Shenhua.
Nahodha huyo wa timu ya taifa ya Ivory Coast alichelwa kuwasili nchini Uturuki kutokana na kuwepo nchini Afrika Kusini alikokuwa akiitumikia timu ya taifa lake katika michuano ya mataifa ya Afrika.
Didier Drogba akiwa ameshika bendera ya Galatasaray baada ya kuwasili Istanbul mchana wa leo.
Drogba akiwa ameshika kitambaa ambacho kimeandikwa jina lake.
Drogba mshambuliaji huyo wa zamani wa Chelsea ameelekea Uturuki baada ya ndoto yake ya kutwaa taji la mataifa ya kushindwa kutimia kwa mara nyingine kufuatia Ivory Coast kufungwa na Nigeria katika mchezo wa robo fainali.
Drogba
alishuka katika ndege akiwa ameshikilia kitambaa ambacho kilikuwa na rangi za Galatasaray kabla ya kukutana na kocha Fatih
Terim.
Alipowasili katika uwanja wa mazoezi wa klabu ya Galatasaray aliongea na kituo cha televisheni cha Galatasaray
ambapo alinukuliwa akisema,
'Nimekutana na kocha licha ya kwamba si mara ya kwanza kukutana naye. Ananikumbuka tangu timu ya taifa ya Ivory Coast ilipocheza na Uturuki.
Drogba amepata mapokezi kama aliyopata kiungo Wesley Sneijder alipowasili Uturuki mwezi uliopita.
Mashabikiwa Galatasaray wakiwa wanapunga hewani bendera ya klabu hiyo baada ya mshambuliaji huyo kuwasili uwanja wa ndege wa Ataturk.
'Najisikia furaha kuwa hapa kwangu ni changamoto mpya, sehemu mpya ya maisha yangu, nitatumia uwezo wangu wote kuipa mafanikio klabu.'
Drogba atakuwa anaungana na Emmanuel Eboue, ambaye alijiunga na mabingwa hao wa soka nchini Uturuki kiangazi mwaka 2011 akitokea Arsenal.
Mshambuliaji mwingine wa Chelsea Nicolas Anelka aliondoka Stamford Bridge na kuelekea Uchina kabla ya kurejea Ulaya.
Nicolas
Anelka alijunga na Shenhua mwezi January mwaka jana lakini akaondoka na kujiunga na kigogo cha Italia Juventus mapema mwezi uliopita.
Wesley Sneijder alivyopokelewa baada ya kuwasili uwanja wa ndege huohuo mwezi uliopita.
Namna ambavyo mashabiki walivyojitokeza kumlaki mduchi Snejder akitokea Inter Milan.
Wesley Sneijder akiwa katika vitendo na Galatasaray.
No comments:
Post a Comment