KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, August 7, 2013

Harambee Stars bado lipwa marupurupu ya Cosafa

Wachezaji wa kikosi cha timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, hawajapokea marupurupu yao baada ya kuiwakilisha nchi katika kinyanganyiro cha michuano ya Cosafa kilichoandaliwa Zambia Julai.

Viungo kadhaa wa timu hiyo ambao waliomba wasitajwe majina yao wameeleza tovuti hili kwamba tangu kuwasili kutoka shindano hilo, hawajapokea hela zozote kwa muda waliokuwa wakicheza kama nchi alikwa katika kombe hilo la mataifa ya Afrika kusini.

“Tunahisi kwamba maafisa wa shirikisho la kandanda wametutenga kwani hakuna ambaye amefuatilia marupurupu yetu ya Cosafa na tunahofia kuwa hatutalipwa. Ni muhimu kwa shirikisho kutekeleza matakwa yake,” mchezaji mmoja aliongeza.

Wakati huo huo, mwenyekiti wa shirikisho, Sam Nyamweya, alikanusha madai hayo akisema kwamba wachezaji walipaswa kunyakua fedha za ushindi katika kombe hilo ndio wapate kulipwa.

“Tulituma kikosi chetu katika shindano la Cosafa na makubaliano kwamba watapigania kitita cha ushindi lakini walikosa kufuzu huku wakielewa kwamba tulishiriki kwa mwaliko. Tuliwalipa marupurupu yao ya hapa nyumbani lakini hatuna nia ya kuwakata moyo. 

“Tutatafuta fedha na kuona vile tutawalipa lakini wanafaa kuelewa kuwa jukumu lao lilikua kushinda kombe hilo,”

Harambee Stars waliaga mashindano hayo na kurejea nyumabnai kwa makundi baada ya kupoteza mechi yao ya mwisho dhidi ya Botswana.

No comments:

Post a Comment