Rais wa  Real Madrid 'Los Blancos' Florentino Perez ametanabaisha kuwa zinahitajika kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kuuboresha wa klabu hiyo na kutupilia mbali madai ya nahodha wa Barcelona, Gerard Pique.

Madrid wanajipanga kutumia Euro milioni €400 katika kujaribu kuimarisha na kuunogesha uwanja wa Santiago Bernabeu na kuwa mmoja wa viwanja bora duniani.

Perez anatarajiwa kutangaza kampuni itakayopewa kazi ya kuuboresha uwanja huo.

Ananukuliwa akisema,
"Kuundeleza kutagharimu kati ya euro milioni €300 na €400m,".

Hivi karibuni mlinzi wa Barcelona Gerard Pique alikaririwa akisema kuwa benki moja ya Hispania iliikopesha Real kuweza kufanikisha usajili wa Gareth Bale jambo ambalo Perez amelikanusha. 
"It is not true what Pique said."