KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, May 10, 2014

Vladmir Klitschko kutetea taji lake la Shirikisho la Kimataifa la Ndondi – IBF dhidi ya Kubrat Pulev wa Bulgaria

Bingwa wa ndondi wa ulimwengu katika uzani wa juu Vladmir Klitschko ameamrishwa kulitetea taji lake la Shirikisho la Kimataifa la Ndondi – IBF dhidi ya Kubrat Pulev wa Bulgaria ambaye hajawahi kushindwa pigano lolote.

Pulev ana rekodi ya kucheza mapambano 20 akishinda yote huku mapambano 11 akishinda kwa KO.
 
Klitschko aliyatetea mataji yake ya WBA na WBO pamoja na mkanda wa IBF wiki mbili zilizopita alipomwangusha sakafuni katika raundi ya tano bondia Alex Leapai wa Australia.

Hilo lilikuwa pigano la lazima la kutetea taji lake la WBO, na sasa Shirikisho la IBF limetangaza Pulev mwenye umri wa miaka 33 kama mpinzano wao wa lazima.

Pulev ameukaribisha uamuzi huo akisema kwamba hiyo ni zawadi yake kubwa ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa. Pulev anasema alishuhudia pigano la Klitschko na Leapai na ni kweli kwamba Klitshcko hakuwa na kibarua chochote dhidi ya mpinzani huyo.

Lakini anasema pigano lake na Mu Ukraine huyo litatimiza ndoto yake na kuuonyesha ulimwengu kuwa Klitschko siyo mashine isiyoweza kushindwa. Promota wa Pulev amesema tayari mazungumzo yameanza kuhusu pigano hilo dhidi ya Klitschko.

No comments:

Post a Comment