KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, December 4, 2012

Scolari ambebesha Neymar da Silva Santos Júnior zigo la taji kombe la dunia 2014. Man United waonywa kuachana na mpango wa Lewandowski.


 Neymar da Silva Santos Júnior si mdogo kuibeba wa kushindwa kubeba matumaini ya Brazil kushinda kombe la dunia. Hii ni kauli ya kocha mpya wa timu ya taifa ya Brazil Luiz Felipe Scolari.

Mshambuliaji huyo wa klabu ya Santos ambaye kwasasa ana umri wa miaka 20, amekuwa akitazamwa na baadhi ya watu kama bado kinda kuweza kubebeshwa matumaini ya Brazil, lakini Scolari ana matumaini kuwa uwezo wa mchezaji huyo ni chachu ya mafanikio wakati Brazil itakapokuwa mwenyeji wa michuano mikubwa ya kombe la dunia 2014.

Scolari  ametolea mfano kwa mkongwe Edison Arantes do Nascimento 'Pele', kuwa alikuwa kijana mdogo wakati nchi hiyo ilipochukua taji mwaka 1958, kama ilivyokuwa kwa Ronaldo Luís Nazário de Lima
Alipoulizwa juu ya umri Neymar na matumaini ya mchezaji huyo kwenye kikosi amesema mbona Ronaldo alitumiwa kuiongoza Seleção, na alifanya hivyo akiwa na umri wa miaka 19 na 20.

"Pele pia alikuwa na umri wa miaka 17 tu , licha ya kwamba hakuwa na jina kubwa wakati huo na alifanikiwa kutengeneza jina wakati na baada ya kombe la dunia 1958.

Man United waonywa kuachana na mpango wa Lewandowski.
 Matumaini ya Manchester United kumsajili Robert Lewandowski katika usajili wa mwezi januari yameanza kutiwa mashaka baada ya klabu yake ya Borussia Dortmund kuthibitisha kuwa mshambuliaji huyo atasalia Bundesliga.

Lewandowski mwenye umri wa miaka 24, amekuwa akihusishwa kuelekea katika ligi kuu ya nchini England “Premier League” katika klabu ya Manchester.

Bosi wa Dortmund Jurgen Klopp amesisitiza kuwa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Poland bado hajatoa ombi la kutaka kuondoka nchini Ujerumani licha ya kwamba mpango huo uko ndani ya maamuzi yake.

Akikaririwa Klopp amesema
"sina wasiwasi kuwa ataondoka, Manchester United ni moja miongoni mwa timu sinazo mkodolea macho lakini ukweli ni kwamba atasalia na sisi.

"Ahsante mungu, wakati wa klabu kubwa tajiri ya England kujaribu kuchukua wachezaji wetu sasa umekwisha. Wakati wa mzunguko wa pili wa msimu ataendelea kukaa nasi"
Klopp anaamini kuwa Bundesliga kwasasa ni ligi kubwa kuliko Premier League, licha ya kwamba Shinji Kagawa aliondoka Dortmund kiangazi.

Mabingwa hao wa ujerumani hii leo watakuwa wenyeji wa Manchester City katika mchezo wa vilabu bingwa Ulaya ambapo licha ya kuwa tayari klabu hiyo imeshapata nafasi katika hatua ya mtoano, Klopp atashusha kikosi cha nguvu kusaka uongozi wa kundi D.

No comments:

Post a Comment