Anzhi
Makhachkala wamethibitisha kumsajili kiungo wa Brazil WillianBorges da Silva kutoka
klabu ya Shakhtar Donetsk kwa ada ya uhamisho ya euro milioni €35.
Willian
mwenye umri wa miaka 24 hapo kabla alikuwa akihusishwa na vilabu viwili vya Chelsea
na Tottenham lakini imethibitika kuwa sasa amejiunga na klabu hiyo inayoshiriki
ligi kuu ya nchini Russia kwa mpango wa muda mrefu zikiwa ni taarifa zilizo
andikwa katika mtandao wa klabu hiyo hapo jana.
Anzhi ilikuwa
katika jitihada za mwisho usiku wa alhamisi na imekamilisha uhamisho huo wa
thamani katika dirisha la mwezi Januari.
Taarifa ya
mtandao wa Shakhtar imesomeka:
“FC Shakhtar
na FC Anzhi wamefikia makubaliano juu ya uhamisho wa Willian kuelekaa katika
klabu hiyo ya nchini Russia kwa thamani ya euro milioni 35.
“Shakhtar inamshukuru
Willian kwa utumishi wake ndani ya klabu hiyo, akifunga magoli na kuonyesha uweledi
wake. Tunamtakia kila la kheri katika timu yake mpya”
Tangu ajiunge
na Shakhtar akitokea Corinthians mwaka 2007, Willian ameichezea michezo 221 na
kufunga jumla ya magoli 37.
Anatarajiwa
kujiunga na kambi ya timu yake mpya iliyoko Marbella hii leo. Atakuwa akijiunga
na wachezaji kadhaa wa kibrazil pamoja na wakali kadhaa kama Samuel Eto'o na Lassana
Diarra.
Balotelli: Hakuna cha kukumbuka England
Mario
Balotelli amewashukuru mashabiki wa Manchester City kwa kumuunga mkono lakini
mshambuliaji huyo wa AC Milan amesema hakutakuwa na kitu cha kumfanya ajione
anakikosa kwa kwa kuondoka England.
Mario
Balotelli anamatumaini makubwa ya kuwepo kwa muda katika klabu yake mpya ya AC
Milan
Balotelli
mwenye umri wa miaka 22, amerejea Italia baada ya kuwa na nafasi finyu katika
klabu yake ya zamani ya Manchester City ambako alikuwa katika vita kubwa ya
kuwania namba na wakali wengine kama Sergio Aguero, Carlos Tevez na Edin Dzeko.
Akiongea
katika mkutano wa utambulisho wake kwa waandishi wa habari kama mchezaji wa Milan, mchezaji huyo alikosoa
mambi mengi yanayo husu utamaduni wa kingereza lakini pia hakusita kuonyesha
kusikitishwa kwake kwa kuiacha ligi ya England ‘Premier League’.
Amenukuliwa akisema
"Niseme
ahsante kwa mashabiki wa City kwasababu wamekuwa wakarimu kwangu na wamekuwa
wakinipa sapoti vyote vya shida na raha”
"Na niwashukuru wachezaji wenzangu na
meneja pia, kingine ni kwamna ninafuraha nimeondoka England.
"Kwa
dhati kabisa niseme ‘Premier League’ ni ligi nzuri sana na nadhani ndio ligi
bora, Kwa mashabiki na uwanjani ... it's an amazing league. Si kama
katika siku za usoni nitarejea huko, kwasasa niko hapa"
Odemwingie: West Brom imenivuruga
Peter
Odemwingie ameinyooshea kidole klabu yake ya West Bromwich Albion kwa kushindwa
kufanikisha uhamisho wake wa kuelekea Queens Park Rangers.
Odemwingie
amepewa mapumziko ya siku chache baada ya kuondolewa akiwa mazoezini hapo jana.
Alikuwa kwenye
mpango wa uhamisho wa mwezi januari ambapo alhamisi alielekea maskani ya QPR
iliyoko Loftus Road huku nyuma taarifa ya West Brom ikitoka ambayo ilisema
mchezaji huyo hakuwa na ruhusa na kuongea na QPR licha kuelekea huko.
Dirisha la
usajili wa mwezi Januari limefungwa huku Odemwingie akishindwa kukamilisha
mipango yake yha uhamisho ambapo jana alirejea kufanya mazoezi na klabu yake West
Brom ambapo kulitokea kutokuelewana kabla ya kuondolewa mazoezini na kupewa
mapumziko ya siku chache.
Taarifa
zinasema hapo kabla West Brom ilikuwa katika hali ya kuwa tayari kumruhusu
kuondoka, lakini baada ya kukosa mchezaji mbadala yake ndipo walipo amua kwa
makusudi kusitisha mpango huo.
No comments:
Post a Comment