KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, August 28, 2010

BLATTER ANAJIPANGA KWA KIPINDI KINGINE CHA MIAKA MINNE BAADA YA KUKOSA UPINZANI KUONGOZA FIFARais wa shirikisho la kandanda duniani Fifa Sepp Blatteranaelekea kabisa muda wake wa kuliongoza shirikisho la kandanda duniani na sasa akijipanga kuchukua kipindi kingine cha kuliongoza shirikisho hilo kwa kipindi kingine cha miaka minne huku akikabiliwa na ushindani mkubwa kutoka kwa mkuu wa shirikisho la kandanda katika bara la Asia.

Mohamed Bin Hammam mwenye umri wa miaka 61anaonekana kama ndiye mpindani mkubwa kwa mkongwe huyo toka Uswize licha ya taarifa za hivi karibuni kuarifu kuwa Bin Hammam hana mpango na kiti hicho.
Blatter ambaye sasa ana umri wa miaka 74 huku naye akisema hana mpango wa kuendelea kuwania nafasi hiyo katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi June mwakani hata hivyo anaonekana mguu ndani mguu nje.

Akikaririwa Bin Hammam anasema "I will not run for the next Fifa election. I will back Sepp Blatter to remain in office".

Lakini kama Bin Hammam atawania nafasi hiyo basi anatarajia kupata ushindani mkubwa kutoka kwa Rais wa sas
a wa shirikisho la kandanda barani ulaya Uefa Michel Platini.
Mfaransa Platin anaonekana kama ndiye mtu mwenye nafasi kubwa kwa sasa kuchukua nafasi hiyo lakini pia akionekana kuwa katika kinyanganyiro kingine cha kuwania nafasi ya Urais katika bodi ya utawala ya soka la ulaya.

Bin Hammam ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya utendaji ya Fifa anasema pia na yeye anatarajia kuingia katika kinyanganyiro kingine cha kuwania Urais wa shirikisho la kandanda barani Asia (AFC) mwakani.

Baada ya miaka 12 kukalia ofisi ya FIFA Kama Rais , Blatter ameweka wazi kuwa hana mpango wa kuondoka hiyo June 11 2011,huku akisema bado hajamaliza baadhi ya mipango yake.

Kwa mara ya kwanza kuchaguliwa katika shirikisho hilo ilikuwa ilikuwa ni mwaka 1998 na baadaye kushinda tena kiti hicho mwaka 2002 before kisha kufanya hivyo tena katika uchaguzi wa mwaka 2007
.

Bin Hammam huko nyuma aliwahi kupinga Rais wa Fifa kukalia kiti hicho kwa zaidi ya vipindi viwili ili kutoa nafasi kwa Asian kuliongoza shirikisho hilo.
Swali lililopo ni nani atachukua kipindi hicho kingine cha uongozi ndani ya Fifa?
Na je dunia ya kandanda iko radhi kumuachia kiongozi huyu?majibu juni mwakanni

No comments:

Post a Comment