KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, August 23, 2010

MICHUANO YA KUTAFUTA UBINGWA WA KIKAPU DUNIANI MAREKANI TISHIO
Licha ya kukosekana kwa wachezaji wao 12 ambao walikuwepo katika kikosi kilichofanikisha medali ya dhahabu kule china timu ya mpira wa kikapu ya marekani inaonekana kama ndiyo timu yenye uwezo wa kutwaa taji la dunia katika michuano ya 2010 FIBA World Championship.
Kama kikosi cha kocha Mike Krzyzewski kitacheza kama timu basi itakuwa ni nafasi nzuri kwa U.S kufanikisha taji hilo kama ilivyo fanya hivyo mwaka 1994. hata hivyo su jambo rahisi kwani kuna hatua ya mtoano tofauti na ilivyokuwa katika michuano ya Olympics.

Jumla ya timu 24 zimegawanywa katika makundi manne tofauti huku kila kundi likiwa na timu sita na kucheza katika vituo tofauti huko nchini Uturuki . Baada ya kila timu kucheza kila kundi basi timu nne za juu zitakuwa zinafuzu kuingia katika hatua ya mtoano michezo yote ya mtoano ikitarajiwa kupigwa katika jiji la Istanbul.

BILA SHAKA NA HAWA NI MAKADA WA CHAMA CHA MAPINDUZI CHEGE NA TEMBA KATIKA MKUTANO WA KAMPENI WA CHAMA CHA MAPINDUZI KATIKA UWANJA WA CCM KIRUMBA MKONI MWANZA(PICHA NA MICHUZI)

No comments:

Post a Comment