KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, September 20, 2010

RUSSELL BRAND NA KETY PERRY KIZUIZINI LOS ANGELES AIRPORT Russell Brand alijikuta katika matatizo na kuwekwa kizuizini kwa muda katika jaribio lake la kutaka kumfanyia kitu mbaya mpiga picha katika uwanja wa ndege wa Los Angeles pale ambapo British actor/comedian huyo mwenye umri wa miaka 35 akiwa na mchumba wake nyota wa miondoko ya pop Katy Perry walipokuwa katika maandalizi ya kukwea pipa tayari kuelekea Las Vegas.

Tukio hilo la Brand limetokea ijumaa ambapo alizuiliwa kwa muda na kuwekwa sero kufuatia kitendo cha paparazzi huyo kutaka kudaka picha ya “chap chap” toka kwa mastaa hao.

Brand alifunguliwa mashitaka katika kituo kidogo cha LAPD's Pacific Division na kuachiwa kwa dhamana ya dolari za kimarekani $20,000.Aliachiwa baadaye sana ijumaa hasa baada ya kujitambuliasha taarifa zikitolewa na msemaji wa Los Angeles Airport Police Belinda Nettles .

Inaarifiwa kuwa mshindi huyo mara mbili wa tuzo za MTV Video Music Awards alikuwa akizongwa na mapaparazi wakati akijaribu kuingia katika terminal

Kidosho wake Perry ame-comment juu ya hilo kupitia Twitter juu ya sakata hilo akikaririwa akiandika kuwa mpenzi wake alikuwa akimlinda yeye na kamera zilizo kuwa zikimmulika
"If you cross the line & try an put a lens up my dress, my fiancé will do his job & protect me.

No comments:

Post a Comment