KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, November 4, 2014

Aleksandar Kolarov nje mwezi mzima, Eliaquim Mangala kuikabili CSKA Moscow

Meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini amethibitisha kuwa Aleksandar Kolarov atakosekana katika kipindi cha takribani mwezi mzima kufuatia matatizo ya msuli.

Mlinzi huyo alipatwa na majeraha katika maandalizi ya kupasha misuli joto kabla ya mchezo dhidi ya Manchester Jumapili iliyopita na nafasi yake kuchukuliwa na Gael Clichy kabla ya kukabiliana na kikosi cha Louis van Gaal.

Nyota huyo wa kimataifa wa Serbia sasa atakuwa katika kipindi mapumziko ingawa Pellegrini kuwa mlinzi Eliaquim Mangala atakuwa safi katika mchezo dhidi ya CSKA Moscow.

"Kolarov alipatwa na matatizo ya msuli atakuwa nje kwa mwezi mzima" amewambia waandishi wa habari "Mangala atakuwepo katika orodha ya wachezaji katika mchezo wa kesho."

No comments:

Post a Comment