Rooney kuendeleza matibabu yake nchini marekani Manchester United imethibitisha kuwa inampeleka mshambuliaji wake Wayne Rooney nchini Marekani kuenedelea kuponyesha majeraha yake ya ankle.
Wayne Rooney anatarajia kurejea dimbani kama mambo yatamuendea vizuri November 21.
Kuliko kumuacha kuendelea kufanya mazoezi ya msingi ya kurejesha hali yake ya majeraha akiwa katika uwanja wa mazoezi wa klabu hiyo wa Carrington klabu hiyo iliona ni vema ikampelekea katika kituo cha vifaa maarufu duniani cha Nike kilichopo Portland, Oregon nchini Marekani ambapo atakuwa anapigania kurejesha afya yake.
United pia imethibitisha kuwa safari hiyo itamsaidia Rooney kuepukana na dhahma yake ya kuonekana kutokuwa na furaha ndani ya klabu hiyo.
Akikaririwa meneja msaidizi wa klabu hiyo Mike Phelan anasema
"tunacho kidhamiria kukifanya kwa Rooney ni kumpeleka kwenye mji wa Nike Town nchini Mrekani kwa juma zima ili kurejesha hali yake ya kawaida,
"ni maamuzi ya timu ya madaktari na makocha na itakuwa ni jambo la busara kwake
No comments:
Post a Comment