KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, June 26, 2012

Floyd Mayweather amshinda Tiger Woods orodha ya Forbes


Tajiri wa Forbes Floyd Mayweather
 Floyd Mayweather amefanikiwa kumshinda Tiger Woods kutengeneza pesa katika kipindi cha mwaka jana kwa mujibu wa orodha ya inayo andaliwa na jarida la Forbes.
Forbes limekuwa kila mwaka likiandaa orodha ndefu ya wanamichezo wanaolipwa pesa nyingi duniani ambapo kwa mwaka jana jarida hilo limeonyesha kuwa Mayweather amekuwa ni mwenye thamani zaidi na kumshinda mchezaji golf mashuhuri duniani Tiger.
Bondia Mayweather kwasasa anatumikia adhabu ya kifungo cha miaka 3 kwa kutumia lugha ya matusi.
Kwa mujibu wa taarifa zilizo toka hii leo zimearifu kuwa Mayweather ametengeneza kipato cha dolari za kimarekani $85m (£54.25m) kutokana na mafanikio ya kutengeneza promotion ya michezo yake.
Mwasisi katika mchezo wa Golf Tiger Woods ameshuka na kukusanya dolari za kimarekani $59.4m (£37.92m) ilhali bondoa mwingine Manny Pacquiao akipanda kimapato na kufikisha jumla ya dolari $62m (£39.57m).
Tiger Woods
Nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya Uingereza David Beckham kwa mujibu wa orodha hiyo yupo katika nafasi ya nane.
Hata hivyo yeye ndiye mwanasoka anaye tengeneza pesa nyingi zaidi kiasi cha dolari $46m (£29.36m).
Orodha kamili mpaka nafasi ya kumi
1 Floyd Mayweather $85m (£54.25m)
2 Manny Pacquiao $62m (£39.57m)
3 Tiger Woods $59.4m (£37.92m)
4 LeBron James $53m (£33.84m)
5 Roger Federer $52.7m (£33.64)
6 Kobe Bryant $52.3m (£33.38m)
7 Phil Mickelson $47.8m (£30.51m)
8 David Beckham $46m (£29.36m)
9 Cristiano Ronaldo $42.5m (£27.10m)
10 Peyton Manning $42.4m (£27.06m)

Woods amekuwa akiongoza katika orodha ya Forbes tangu mwaka 2001 lakini akashuka kimapato kwa dolari $16m (£10.21m) kuanzia mwaka jana na kushuka kwa kiwango cha nusu ya kipato chake cha mwaka 2009. Taarifa zinasema huenda kashfa ya ngono imechangia.
Nyota wa kikapu wa Miami Heat LeBron James yuko katika nafasi ya nne amekusanya $53m (£33.84m),ikiwa ni zaidi kwa wacheza 13 katika orodha hiyo na mcheza Tennis raia wa Uswiss Roger Federer akiwa katika nafasi ya tano baada ya kuweza kulipwa dolari $52.7m (£33.64m).
Mcheza soka mwingine mchezaji wa Real Madrid na timu ya taifa ya Ureno Cristiano Ronaldo amepanda baada ya kutengeneza dolari $42.5m (£27.10m) .
Fernando Alonso ameingia baada ya mafanikio ya michezo ya mashindano ya magari ya Formula 1 ameshika nafasi ya 19 kwa kuingiza dolari $29.4m (£18.7m).
Mwendesha magari toka MotoGP Valentino Rossi yuko katika nafasi ya 20 na mshindi mara saba wa mashindano ya magari ya Formular 1 Michael Schumacher yeye yuko katika nafasi ya 21wakati ambapo Lewis Hamilton akiwa katika nafasi 24 baada ya kukusanya dolari $17.8m (£11.3m) huku dolari $15.9m (£10.1m) zikitokana na mshahara wa McLaren.
Mshambuliaji wa Manchester United na timu ya taifa ya Uingereza Wayne Rooney yuko katika nafasi ya 37 kutokana na kipato cha dolari $15.5m (£9.8m) ilhali Luke Donald mchezaji golf namba moja kwasasa akiwa katika nafasi ya 48 kufuatia kukusanya dolari $14.17m (£9m).
Wanawake wawili pekee walio katika orodha ni mcheza tenis raia wa Russian Maria Sharapova yuko katika nafasi ya 26 kutokana na kipato cha dolari $27.9m (£17.79m) na mwingine ni Li Na raia wa  China ambaye ni bingwa wa mwaka jana wa michuano ya wazi ya tenis ya French champion yeye yuko katika nafasi ya 81 kutokana na kipato chake kufikia dolari $18.4m (£11.72m) hususani baada ya kuwa mzaliwa wa bara la Asia pekee kushinda taji la mchezo wa tenis la Grand Slam kwa mchezaji mmoja mmoja.

No comments:

Post a Comment