Baraza la
vyama vya soka Afrika mashariki na kati CECAFA limevipongeza vilabu vyote
vilivyo fanikiwa kufikia katika hatua ya robo fainali ya michuano ya Kagame
ambayo inaendelea nchini Tanzania.
Jumla ya
timu nane zimefanikiwa kuingia katika hatua hiyo wakiwemo mabingwa watetezi wa
kombe Yanga ambao waliongoza katika kundi B kwa kumaliza hatua ya makundi
wakiwa wamejikusanyia jumla ya points 6 kufuatia kupata ushindi katika michezo
miwili dhidi ya Salaam Wau ya Sudani kusini na ARP ya Rwanda na kupoteza mchezo
mmoja dhidi ya Atletico ya Burundi.
Timu
nyingine ni Simba, URA na Vita Club toka kundi A na Azam na Mafunzo toka kundi
C.
Katika kundi
la B yanga imeungana na APR na Atletico kucheza hatua ya mtoano.
Akizungumza
hii leo katibu wa CECAFA Nikolaus musonye amesema wao kama CECAFA wameridhishwa
na viwango na nidhamu iliyoonyeshwa na timu zote huku akisifu zaidi mchezo wa
jana kati ya Simba na Vita ambao ulimalizika kwa nidhamu ya hali ya juu pasi na
kuwepo kadi hata moja ya njano wala nyekundu.
Katika hatua
nyingine CECAFA imefanya marekebisho ya siku katika ratiba ya michuano hiyo
kuanzia hatua ya nusu fainali kwa kutenganisha michezo ya hatua hiyo endapo
timu mbili kubwa za Tanzania Simba na Yanga endapo zitafanikiwa kuingia katika
hatua ya nusu fainali.
Musonye
amesema endapo timu hizo mbili za Tanzania zenye mashabiki wengi zitafuzu hatua
hiyo basi mchezo wa nusu fainali ya kwanza itachezwa jumatano na mchezo wa pili
utachezwa alhamisi tofauti na ilivyo sasa ambapo michezo ya nusu fainali yote
inaonekana kwenye ratiba kuchezwa simu moja yaani alhamisi.
Amesema hili
limezingatia hali ya usalama endapo timu moja itaonekana kupoteza mchezo wake.
Timu ambazo
zimeaga michuano ni Ports ya Djibout, Salaam Wau ya Sudan Kusini na Tusker ya
Kenya.
No comments:
Post a Comment