Lucas Moura |
Manchester
United inajipanga kumnunua Lucas Moura kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni £32 baada ya
klabu yake ya Sao Paulo kugomea ada ya pauni milioni £27.2m za awali.
Klabu hiyo ya
nchini Brazil imedai kuwa United imeonyesha nia ya kuweka kile ambacho klabu
hiyo ilichokiita offer muhimu ya euro milioni €35 ambayo ni sawa na pauni
milioni £27.2 kwa ajili ya kiungo mshambuliaji huyo kijana kabisa mwenye umri
wa miaka 19.
Vyanzo vya habari
vimeeonyesha kuwa mashetani wekundu wameweka offer hiyo juzi na kwamba Sao
Paulo imesema kiwango hicho kinatosha kukamilisha mipango ya kumuuza mchezaji
huyo.
Lucas, ambaye
alikuwa ni sehemu ya wachezaji wa timu ya taifa ya Brazil ambayo iliichapa Great
Britain katika mchezo wa kujipima nguvu wa maandalizi ya michezo ya Olympics
ijumaa usiku.
Bosi wa
United Sir Alex Ferguson alipata nafasi ya kumuona Moura kupitia mchezo huo na
kuona kuwa anaweza kuziba nafasi ya Eden Hazard ambaye walikuwa wakimtaka huko
nyuma kabla ya kushindwa kunasa saini ambapo Chelsea walifanikisha wakati wa
ufunguzi dirisha la usajili.
Imefahamika
kuwa kiasi hicho cha pesa kipo kwa ajili kumsaini Lucas lakini pia Uinted haiku
tayari kwenda nje ya kiwango hicho kwa maana ya zaidi ya hapo.
United ina
imani mchezaji huyo anayezungumza lugha ya kireno atakapo kuwa na wenzake
wanaozungumza lugha hiyo kama vile Nani, Anderson na Rafael Da Silva atakuwa na
kazi rahisi ya kuelewana na wenzake.
No comments:
Post a Comment