KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, October 15, 2012

Mmiliki wa Liverpool FSG ajipanga kuendeleza uwanja wa Anfield na Cazorla: najaribu kumuiga Iniesta wa Barcelon


Mmiliki wa Liverpool Fenway Sports Group amethibitisha kujipanga kwa ajili ya kuendeleza dimba la Anfield.

Malumbano baina ya klabu hiyo na halmashauri ya mji wa Liverpool juu ya kubomoa nyumba za karibu na uwanja huo yanaonekana kufikia ukingoni licha ya matangazo ya ukarabati wa kuongeza uwezo wake wa watazamaji kuelezwa kuwa utafanyika baadaye.
Mkurugenzi wa klabu hiyo Ian Ayre ametanabaisha kuwa Liverpool imekuwa kifanya kazi bega kwa began a mamlaka ya mji huo ili kufikia makubaliano ambayo yataendeleza eneo lote linalo zunguka Anfield.

Amenukuliwa mkurugenzi huyo akisema
"ujenzi mpya wa Anfield ni kitu ambacho wakaazi na watu wengi mji mzima wamekuwa wakizungumza na wote tumegundua kuwa klabu ya soka ni mwajiri, ni biashara na pia ni mkazi wa eneo hili."

Ayre, pia amezungumzia juu ya kuendelea kuwepo hapo kwa klabu hiyo huku akidai kuwa kujenga uwanja mpya ni jambo la gharama.

Cazorla: najaribu kumuiga Iniesta wa Barcelon
Santi Cazorla amesema nyota Andres Iniesta ambaye ni mchezaji anaye tokea katika taifa moja la Hispania , amesema kuwa mchezaji wa kuigwa na yeye amekuwa kwenye ndoto ya kufikia uwezo wa kiungo huyo.

Cazorla anacheza msimu wake wa kwanza katika ligi kuu ya nchini England na amekuwa akivutia katika uchezaji wake ikiwa ni pamoja na kutoa pasi za mwisho na hata kufunga katika michezo saba ya msimu huu akiwa na Arsenal.

Lakini nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 ambaye ametokea Malaga katika kipindi cha uhamisho wa kiangazi anaamini Iniesta ni mchezaji ambaye kila mtu anapenda kumuangalia.

"Iniesta ni kiwango ambacho mimi nachukulia kama kipimo changu. Kucheza kama yeye ni kitu kingine. Ni mcheza soaka aliyekamilika katika kila kitu"

"najaribu kuiga kila kitu anachofanya lakini ni ngumu sana. Tatizo ni kwamba anapokuwa anafanya jambo unaliona kama rahisi lakini unapokwenda kujaribu unakutana na ugumu. Andres ni ‘role model’ wangu ndani na nje ya uwanja."

No comments:

Post a Comment