KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, December 6, 2012

CHINA YATOA VIFAA VYA NGOMA ZA KITAMADUNI KWA TANZANIA.


Balozi wa China nchini Tanzania Lu Youiquing akumuonyesha waziri wa habari utamaduni na michezo wa Tanzania Dr Fenera Mukangara jinsi ya kupiga moja ya  vifaa vya ngoma za utamaduni .
Balozi wa china nchini Tanzania Lu Youiquing hii leo amemkabidhi vifaa mbalimbali vya ngoma, muziki na filamu waziri wa habari, utamaduni na michezo katika Dr Fenera Mukangara kwa lengo la kuimarisha mahusiano katika nyanja za kitamaduni na filamu nchini.

Akiongea wakati wa mkutano wao na waandishi wa habari Balozi Lu Youiquing amesema vifaa hivyo mbali na kuendeleza sekta nzima ya burudani lakini pia vifaa hivyo vitasaidia kupunguza gharama za utayarishaji wa muziki na uhariri wa picha za filamu kwa wadau wa tasnia hizo.

Kwa upande wake Dr Mukangara amesema wamepokea vifaa vingi ikiwemo ngoma, magitaa na vifaa vingine ambavyo ni adimu nchini ambavyo vitaimarisha ubora wa filamu.

Amesema huo ni muendelezo wa mashirikiano na Uchina katika mipango mbalimbali ya kukuza sekta ya ngoma, muziki na filamu.

Dr Fenera amesema baadhi ya vifaa vitapelekwa chuo cha sanaa na vingine vitapelekwa katika kitengo cha filamu kwa kuwa kuna baadhi ya vifaa ni kwa ajili ya kufanyia editing.
 
BOFYA CHINI

No comments:

Post a Comment