KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, May 14, 2013

Roberto Mancini alifukuzwa kwasababu hizi..............na David Beckham kusalia PSG.


Imefahamika Kuwa Roberto Mancini alifukuzwa kuwa meneja wa Manchester City kutokana na mawasiliana na mabaya baina yake na matendaji.
Kushindwa kwake kuendeleza wachezaji vijana ilikuwa pia ni sababu ya kuondolewa kwake kibaruani.
City inafikiria kumchukua kocha wa Malaga Manuel Pellegrini licha ya kwamba mpango huo kuonekana haujakamilika bado
Kwasasa meneja msaidizi Brian Kidd atakuwa kibaruani kwa muda kama meneja wa kikosi hicho.
Atakuwepo katika benchi la ufundi katika michezo miwili ya mwisho ya ligi dhidi ya Reading hii leo na mchezo mwingine dhidi ya Norwich Jumapili pamoja na michezo ya safarini nchini Marekani mwishoni mwa mwezi huu wa May wakati huu City ikisaka mbadala wa Mancini.

David Beckham kusalia Paris St-Germain
 Paris St-Germain wanataka kusalia na David Beckham msimu ujao hata kama asipokuwa mchezaji.
Beckham mwenye umri wa miaka 38, aliingizwa katika mchezo wa  Jumapili baina ya PSG na Lyon ambao PSG ilichomoza na ushindi wa bao 1-0 .
Akiongea na L’Equipe Rai wa klabu hiyop Nesser Al-Khalaii amesema
"Ameamua kuchana kucheza soka lakini nina matumaini atasalia kwa kazi nyingine," .
Alipoulizwa juu ya nini mipango yake kiungo huyo wa zamani wa England amesema
"Niko katika furaha usiku huu hilo ndilo la msingi"
PSG inaamini kumpatia Beckham mkataba mwingine wa miezi mitano kama alivyofanya wakati akijunga nayo mwezi Januari baada ya kumaliza mkataba wake wa miaka sita katika klabu ya Los Angeles Galaxy ya nchini Marekani.

No comments:

Post a Comment