KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, October 24, 2013

EUFA KUCHUNGUZA UBAGUZI DHIDI YA YAYA TOURE.

SHIRIKISHO la soka barani Ulaya EUFA limethibtisha kuwa litazindua upelelezi wake dhidi ya klabu ya CSKA Moscow juu ya vitendo vlivyo ripotiwa vya ubaguzi wa rangi vilivyo fanywa na mashabiki wake hapo jana katika mchezo dhidi ya Manchester City mchezo ambao City Ilishinda bao 2-1.

Kiungo wa City Yaya Toure alilalamika kufanyiwa vitendo hivyo baada ya mchezo na kuitaka Uefa kuchukua hatua dhidi ya Moscow.

CSKA Moscow imekanusha madai hayo dhidi yake kupitia kituom cha Sky Sports ambapo wamenukuliwa wakisema:
 "Hakuna cha kuzumngumza kwani hakuna kilicho tokea."

katika hatua nyingine, Uefa imethibitisha kuzindua uchunguzi dhidi ya mashabiki hao ambako suala hilo litaanza kuzungumzwa mwishoni mwa mwezi huu.

No comments:

Post a Comment