Shirikisho
la soka nchi TFF liko kwenye hatua za mwisho za mchakato wa Uchaguzi Mkuu uliopangwa 
kufanyika tarehe 26/27 Oktoba 2013 hapa jijini Dar es salaam.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na idara ya mawasiliano ya shirikisho hilo imesema hivi
 sasa, wagombea wanasubiri vyombo vya juu vya uamuzi kwa ajili ya kutoa 
uamuzi wa mwisho kabla ya kuanza kampeni na hatimaye uchaguzi.
Hata
 hivyo, baada ya Kamati ya Maadili kufanya uamuzi dhidi ya kesi nane 
zilizowasilishwa mbele yake, Sekretarieti imeona kuwepo kwa ukakasi 
katika utekelezaji wa uamuzi huo kutokana na ukweli kuwa kuna baadhi ya 
mambo yanaonekana kuwa na ugumu katika kuyatekeleza.
Sekretarieti
 si chombo chenya mamlaka ya kutafsiri uamuzi wa vyombo huru vya 
Shirikisho, kazi yake kubwa ni kupokea uamuzi na kuutekeleza, hivyo kwa 
kuwa kuna ukakasi huo imeamua kuwasilisha uamuzi huo kwenye Kamati ya 
Rufani ya Maadili kwa ajili ya kuufanyia mapitio (revision) na pia kutoa
 mwongozo kabla ya kurejesha uamuzi huo kwenye Kamati ya Uchaguzi kwa 
ajili ya kuendelea na mchakato.
Sekretarieti
 imefanya hivyo kwa lengo la kusaidia wagombea ambao wengi wanaonekana 
kuwa njia panda baada ya kupokea uamuzi wa Kamati ya Maadili na kuiuliza
 Sekretarieti kuwa inakuwaje Kamati ya Maadili iwaone hawana hatia, 
lakini hapo hapo ikubaliane na uamuzi wa kuwaengua, jambo ambalo kwa 
kweli limetufanya tukose majibu sahihi na hivyo kuamua kuomba revision 
na mwongozo.
Pia
 mwongozo utakaotolewa na Kamati ya Rufani ya Maadili utasaidia kuweka 
mwelekeo mzuri wa masuala ya Maadili katika siku zijazo.
Miongoni
 mwa mambo yanayoonekana kuwa na ukakasi ni kuwaona watu wote ambao kesi
 zao ziliwasilishwa kwenye Kamati ya Maadili hawana hatia, lakini hapo 
hapo kukubaliana na uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi wa kuwaengua baadhi yao
 kwa sababu za kinidhamu ikisema haiwezi kuwahukumu mara mbili kwa kuwa 
wameshaadhibiwa kwa kuenguliwa kwenye uchaguzi.
Ili
 haki itendeke na ionekane inatendeka, Sekretarieti imeona ni vizuri 
masuala hayo yakafanyiwa revision (mapitio) na kutolewa mwongozo ili 
kuondoa ukakasi uliojitokeza miongoni mwa wagombea, Shirikisho na wadau 
na hivyo kujenga hisia kuwa kuna mbinu zimefanyika dhidi ya baadhi ya 
wagombea.
Uamuzi
 huu haumaaniishi kuwa Sekretarieti inapingana na uamuzi wa Kamati ya 
Maadili, bali ni utaratibu wa Sekretarieti kuomba ufafanuzi au mwongozo 
kutoka vyombo husika pindi inapotokea ukakasi katika utekelezaji wa 
uamuzi wa vyombo vya uamuzi vya Shirikisho. 
Sekretarieti
 imeshamwandikia Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani za Maadili ili aitishe 
kikao kwa manajiri ya kufanya mapitio na kutoa mwongozo ambao utasaidia 
Shirikisho kuendelea na uchaguzi bila ya ukakasi.

No comments:
Post a Comment