KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, March 3, 2014

Ferguson aomba Moyes apewe muda

Meneja mstaafu wa Manchester United, Sir Alex Ferguson ameeleza imani kuwa miamba hao wa Uingereza watapata mwelekeo chini ya mrithi wake David Moyes.
United wamezorota musimu huu huku Moyes akishindwa kuendeleza ufanisi uliokuwa kawaida chini ya Ferguson.
Mabingwa hao wa ligi ya Premier wamo nafasi ya saba kwenye jadwali na wanakondolea kungolewa kutoka kombe kuu bara Uropa, Champions League, baada ya kupoteza mkondo wa kwanza raundi ya mwondoano 2-0 dhidi ya Olympiakos.
Wengi sasa wanataka United wastahimili hasara na kumtaliki Moyes lakini Ferguson amemtetea raia mwezake wa Scotland aliyekuwa meneja wa Everton akisema ana uwezo wa kuimarisha magwiji hao.
“Watakuwa sawa. Bado ni mapema na kumekuwa na mabadiliko mengi na Moyes anastahili muda. Nilikuwa hapo miaka 27, kwa hivyo itamchukua meneja mpya wakati,” Ferguson alisema.
Chini ya enzi yake, United walizoa mataji 26.

No comments:

Post a Comment