KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, March 27, 2014

Uhispania na Barca kumkosa Valdez baada ya kupata jeraha la mguu

Mlinda mlango wa Barcelona na timu ya taifa ya uhispania, Victor Valdes hatashiriki fainali za Kombe la dunia baada ya kupata jeraha kwenye mshipa wa mguu.
Victor mwenye umri wa miaka 32 aliondolewa uwanjani kwa machela wakati wa mechi kati ya Barcelona na Celta Vigo, ambapo Barcelona iliinyuka timu hiyo magoli 3-0 siku ya jumatano.
Klabu ya Barcelona imethibitisha kuwa mchezaji huyo amepata jeraha na kuwa atahitaji kufanyiwa upasuaji.
Inaelezwa kuwa kutokana na hali hii huenda Valdes ukawa ndio mchezo wake wa mwisho akiwa na Barcelona na ataondoka kwenye klabu hiyo mkataba wake utakapomalizika kipindi cha majira ya joto.
Kocha wa Barcelona, Gerardo Martino amesema hakuna mpango wa kumtafuta mlinda mlango mwingine na kuwa atamaliza msimu huu na kikosi alichonacho.
Victor alipata jeraha dakika ya 22 katika dimba hilo lililokuwa Nou Camp, muda mfupi baada ya kupangua mpira wa adhabu wa Celta Vigo.
Valdes, ambaye ambaye ameichezea Barcelona kwa miaka 12, alikuwa akitegemewa kupambana na Iker Casillas kupata nafasi ya kuidakia timu ya taifa ya Uhispania katika michuano ya kombe la dunia
nchini Brazil mwaka huu lakini fursa hiyo imeonekana kuwa finyu kwake.
Valdes amepata jeraha ikiwa ni mara ya pili katika msimu huu mara ya kwanza alipata jeraha kwenye kifundo cha mguu wakati Uhispania ilipocheza mechi ya kirafiki na Afrika kusini mwezi Novemba
mwaka jana na kufungwa 1-0.
Jeraha hilo lilimfanya Valdes kukosa mechi nane ya Barcelona

No comments:

Post a Comment