Inaaminika kuwa Frank Lampard yuko katika kuelekea kusaini mkataba mpya wa mwaka mmoja na klabu yake ya Chelsea.
Mkongwe huyo wa 'The Blues' atakuwa nje ya mkataba wakati wa kiangazi kama ilivyo kwa wakongwe wenzake mlinzi wa kati John Terry na mlinzi wa pembeni Ashley Cole.
Lakini inavyoonekana ni kwamba Lampard atakuwa wa kwanza kuingia saini katika makabrasha ya mkataba kwa kipindi cha mwaka mmoja wa kuendelea kusalia Stamford Bridge, na inaarifiwa kuwa alikuwa katika mazungumzo na wakuu wa darajani wiki chache zilizopita.
Taarifa zinaarifu kuwa nyota huyo wa kimataifa wa England angeelekea ligi ya Marekani ya MLS msimu ujao, lakini bosi wa Chelsea Jose Mourinho amekuwa akionekana kutaka kumbakisha kiungo huyo mzoefu katika kikosi chake wakati huu ambapo anapigana kuimarisha kikosi.
No comments:
Post a Comment