Waswahili wanamsemo wao usemao ukitaka ubaya dai chako, jambo ambalo limeharibu mahusiano baina ya mabingwa wa Bundesliga, Bayern Munich na Borussia
Dortmund, ambao watakutana mwezi ujao katika fainali ya kombe la
Shirikisho la soka la Ujerumani – DFB.
Kwa nini? Siyo usajili wa wachezaji tu, hapana ni kwa sababu ya mzozo wa deni linalotokana na mkopo uliodumu mwongo mmoja.
Timu hizo mbili zimekuwa zikishambuliana kwa maneno kuhusiana na mkopo
wa kiasi cha euro milioni mbili ambao Bayern iliwapa Dortmund wakati
walipokuwa wamekabiliwa na matatizo ya kifedha mwaka wa 2004.
Rais wa Bayern Karl Hopfner anadai Afisa Mkuu Mtendaji wa Dortmund
Hans-Joachim Watzke hakusema ukweli alipodai kuwa Bayern wanadai kupewa
kiasi kikubwa cha riba kutokana na mkopo huo.
Katika misimu minne iliyopita, Dortmund wameibuka kuwa wapinzani wakuu
wa Bayern katika ligi ya nyumbani na Ulaya, huku wakishinda mataji
mawili katika mwaka wa 2012 na ligi 2011 kabla ya kushindwa na mahasimu
hao wa Munich katika fainali ya Champions League msimu uliopita.
Hata hivyo wamewapiga Bayern magoli matatu kwa sifuri katika Bundesliga
hivi majuzi ili kujirejeshea hadhi yao. Afisa Mkuu Mtendaji wa Bayern
Karl Heinz Rummenige anasema Bayern haihitaji mkutano wa kilele wa amani
na wala haihitaji mkutano wowote na Dortmund.
Bayern ambao wanalenga kurudia mafanikio ya msimu uliopita kwa kushinda
mataji matatu, Bundesliga, Champions League na kombe la DFB, wanapambana
na Real Madrid Jumanne ijayo katika pambano la marudiano la nusu
fainali.
No comments:
Post a Comment